Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
Juma Linaloanza Januari 12
Dak.10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 4, panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 15 na Amkeni! la Desemba 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Baada ya kila onyesho, kazia baadhi ya mambo mema ya onyesho hilo.
Dak.15: “Ubora wa Hekima ya Mungu.”a Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko yaliyoonyeshwa.
Dak.20: Vichapo Vipya Tulivyofurahia Kupokea! Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Tulifurahi kupokea vichapo vitatu katika Kusanyiko la Wilaya la “Mtukuzeni Mungu.” ‘Ona Nchi Nzuri’ ni kichapo cha pekee sana katika maktaba yetu. Kila unapofungua ukurasa, utaona jambo lenye kuvutia kuhusu Nchi ya Ahadi. Taja baadhi ya mambo yaliyo katika kurasa mbalimbali. Toa madokezo kuhusu njia ambazo kitabu hiki kinaweza kutumiwa. Kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu kitaboresha hali ya kiroho ya watoto wetu. Taja baadhi ya habari za wakati unaofaa ambazo zimezungumziwa, ukionyesha jinsi wazazi na watoto wanavyoweza kufaidika. Tulichochewa kama nini Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika Kiswahili ilipotolewa katika kusanyiko lililopita! Ofisi ya tawi imepokea barua nyingi sana za shukrani. Tafsiri hiyo itaboresha uelewaji wa Maandiko Matakatifu kwa watu wanaosema Kiswahili wanapoendelea na usomaji wao wa Biblia wa kila siku. (Mdo. 17:11) Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi wanavyotumia kwa njia nzuri vichapo hivyo vipya.
Wimbo 186 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 19
Dak.5: Matangazo ya kwenu.
Dak.10: Sanduku la Swali. Hotuba itolewe na mzee.
Dak.15: Mahitaji ya kwenu. Tia ndani habari kutoka katika Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1979, ukurasa wa 2, kuhusu faida ya kutoa ripoti ya utumishi wetu wa shambani kwa ukawaida. Taja jinsi kutaniko linavyoendelea katika kutoa ripoti kwa ukawaida.
Dak.15: “Tunaweza Kuwasaidiaje Wenzi Wasio Mashahidi?”b Mhoji Shahidi mmoja au wawili ambao walianza kumtumikia Yehova kwa sababu ya mfano mzuri wa mwenzi wao wa ndoa aliyekubali kweli.
Wimbo 73 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 26
Dak.12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti ya shambani ya Januari. Ukitumia madokezo kwenye ukurasa wa 4, toa onyesho la jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1 na Amkeni! la Januari 8. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe hata kama ni moja tu litakalozungumziwa. Katika moja la maonyesho hayo, onyesha jinsi unavyoweza kumtolea jirani magazeti.
Dak.15: Tumia Neno la Mungu Katika Maisha Yako Kila Siku. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Watie wote moyo watumie vizuri kijitabu Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2004. Zungumzia maelezo yaliyo katika utangulizi, ukurasa wa 3-4. Waulize wasikilizaji kuhusu saa ambayo wanaona kuwa ni bora zaidi kuchunguza andiko la siku. Zungumzia andiko na maelezo kwa ajili ya siku hiyo pamoja na kutaniko. Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi tunavyoweza kutumia habari hizo. Watie wote moyo wafikirie kwa ufupi jinsi wanavyoweza kutumia habari hizo wanapozungumzia andiko kila siku.
Dak.18: Kusitawisha Urafiki Pamoja na Waamini Wenzetu. (Met. 18:24; 27:9) Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji ikitegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi la Desemba 1, 2000, ukurasa wa 22-23. Moja ya baraka za ibada ya kweli ni kuwa na nafasi ya kupata marafiki wa kweli. Ushirika wetu katika mikutano, utumishi wa shambani, na katika pindi nyingine huandaa kitia-moyo kikubwa sana. Tunaweza kusitawishaje urafiki pamoja na wengine kutanikoni? Pitia sanduku “Hatua Sita za Kuwa na Urafiki wa Kudumu,” na uwaombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu jinsi kila hatua inavyoweza kutumiwa tunaposhughulika na ndugu zetu.
Wimbo 177 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Februari 2
Dak.10: Matangazo ya kwenu. Taja toleo la vichapo la Februari. Pitia maonyesho ya kutoa kitabu Mkaribie Yehova katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2003, ukurasa wa 3. Habari za Kitheokrasi.
Dak.20: “Angalia Sana Jinsi Unavyotumia Wakati.”c Waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu kile wanachofanya ili mambo yasiyo ya lazima yasiingilie miradi yao ya kiroho. Taja mambo yanayopoteza wakati katika eneo lenu.
Dak.15: Mwige Paulo Kama Alivyomwiga Kristo. (1 Kor. 11:1) Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kama vile Yesu, vivyo hivyo Paulo alitumia nafasi ili kuwatolea ushahidi “wale waliokuwapo.” (Mdo. 17:17) Tuna nafasi gani ya kufanya hivyo katika eneo letu? Ni nani ‘waliopo’ tunapoenda dukani, tukiwa kazini au shuleni, au tunaposafiri kwa magari ya umma? Tunaweza kukutana na nani tukiwa nyumbani? Waombe wasikilizaji wasimulie mambo waliyojionea wakiwatolea watu ushahidi katika shughuli zao za kila siku.
Wimbo 151 na sala ya kumalizia.
[Maelezo ya Chini]
a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.
c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.