-
MatangazoHuduma ya Ufalme—2003 | Januari
-
-
Matangazo
◼ Januari: Kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya 1988 chenye kurasa 192 chaweza kutolewa. Makutaniko ambayo hayana vitabu vya zamani vyenye kurasa 192 yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu au Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Februari: Kitabu kipya Mkaribie Yehova. Makutaniko ambayo bado hayana kitabu hiki yanaweza kutumia kitabu Creation au Ufunuo Upeo Wao. Machi: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jitihada ya pekee yapaswa kufanywa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani. Aprili na Mei: Magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Unapowarudia watu waliopendezwa, jitahidi kuwaachia kitabu Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli na kuanzisha funzo la Biblia la nyumbani, hasa ikiwa watu hao tayari wamejifunza kitabu Ujuzi na broshua Anataka.
◼ Kuanzia Februari, na kabla ya Machi 2, kichwa kipya cha hotuba ya waangalizi wa mzunguko kitakuwa “Kukombolewa Kutokana na Ulimwengu Wenye Giza.”
◼ Makutaniko yapaswa kufanya mipango ya kuadhimisha Ukumbusho mwaka huu Jumatano, Aprili 16, baada ya jua kutua. Ingawa hotuba yaweza kuanza mapema, kupitishwa kwa mifano hakupaswi kuanza mpaka jua litue. Chunguzeni vyanzo vya habari vya kwenu ili mjue wakati ambapo jua litatua katika eneo lenu. Mahali ambapo kwa kawaida makutaniko kadhaa hutumia Jumba moja la Ufalme, labda kutaniko moja au makutaniko zaidi yanaweza kutumia jengo jingine jioni hiyo. Inapowezekana, twadokeza kuwe na angalau dakika 40 hivi katikati ya vipindi ili wote wanufaike kikamili na pindi hiyo. Hali za msongamano na maegesho ya magari zapasa kufikiriwa, kutia ndani kusafirisha watu. Baraza la wazee lapaswa kuamua ni mipango gani itafaa kutaniko lenu.
◼ Kuanzia na toleo hili, orodha ya vichapo vipya vinavyopatikana haitachapishwa tena katika Huduma Yetu ya Ufalme. “Tangazo kwa Makutaniko Yote” lenye habari hii litaendelea kutumwa kwa kila kutaniko kila mwezi. Mnakumbushwa kuwa, “Tangazo kwa Makutaniko Yote” likipokewa, mnapaswa kutangaza kwenye Mkutano wa Utumishi utakaofuata vichapo ambavyo huenda kutaniko lenu linavihitaji. Kisha tangazo laweza kuwekwa kwenye ubao wa matangazo. Baada ya hapo, mtumishi wa vitabu anapaswa kuliweka kwenye faili yake.
-
-
Sanduku La SwaliHuduma ya Ufalme—2003 | Januari
-
-
Sanduku La Swali
◼ Kikundi kinachosema lugha ya kigeni kinapaswa kuanzishwa wakati gani?
Eneo la kutaniko linapokuwa na watu wengi wenye kuongea lugha ya kigeni, wazee wanapaswa kufanya yale wanayoweza ili kupanga kazi ya kuhubiri katika lugha hiyo. (km 2/98 uku. 3-4) Huenda ikawa kwamba watu wanaosema lugha ya kigeni wametapakaa kote katika maeneo ya makutaniko mawili au zaidi katika ujirani. Ikiwa hivyo, mwangalizi au waangalizi wa mzunguko watatoa mwelekezo unaohitajiwa, wakisaidia makutaniko yanayohusika yashirikiane katika kazi ya kuhubiri. Mara kwa mara, hotuba ya watu wote au Funzo la Mnara wa Mlinzi laweza kupangwa ili kuona ni watu wangapi wanaohudhuria mikutano ya lugha hiyo ya kigeni.
Kikundi cha lugha ya kigeni chaweza kuanzishwa wakati matakwa yafuatayo yanapotimizwa: (1) Kuna wahubiri au watu wenye kupendezwa ambao wanaelewa habari njema katika lugha ya kigeni. (2) Kuna mzee au mtumishi wa huduma anayestahili ambaye anaweza kuongoza angalau mkutano mmoja kila juma. (3) Baraza la wazee liko tayari kutegemeza kikundi hicho. Matakwa hayo yanapotimizwa, wazee wanapaswa kujulisha ofisi ya tawi ili kikundi hicho kitambuliwe rasmi na maagizo zaidi yatolewe.
Vikundi vingi huanza kwa kufanya Funzo la Kitabu la Kutaniko kila juma. Baadaye, wazee wanaweza kukubali kuongeza mikutano mingine, kama vile Hotuba ya Watu Wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi. Hotuba Namba 2, 3, na 4 za Shule ya Huduma ya Kitheokrasi zaweza kutolewa katika darasa tofauti ikiwa kuna mzee au mtumishi wa huduma anayeifahamu lugha hiyo vizuri na ambaye anaweza kutoa mashauri. Lakini, kikundi hicho kitajiunga na kutaniko kusikiliza hotuba ya sifa ya usemi, hotuba ya maagizo, mambo makuu ya usomaji wa Biblia, na Mkutano wa Utumishi. Pia kikundi hicho kinaweza kuwa na mikutano yao ya utumishi wa shambani.
Wote katika kikundi hicho watashirikiana sana na baraza la wazee. Wazee wanapaswa kutoa mwelekezo na kuchukua hatua ya kutunza mahitaji ya kikundi hicho. Mwangalizi wa mzunguko anapotembelea kutaniko linalotegemeza kikundi hicho, atapanga pia kuhubiri pamoja na kikundi hicho ili kukijenga kiroho. Kwa baraka za Yehova, huenda kikundi hicho cha lugha ya kigeni kikawa kutaniko baada ya muda fulani.
-
-
Madokezo ya Kutoa Kitabu Mkaribie YehovaHuduma ya Ufalme—2003 | Januari
-
-
Madokezo ya Kutoa Kitabu Mkaribie Yehova
◼ Ukiwa na Biblia mkononi, sema: “Watu wengi ambao humwamini Mungu wangependa kumkaribia. Je, ulijua kwamba Mungu anatualika tumkaribie? [Soma Yakobo 4:8.] Kichapo hiki kimekusudiwa kuwasaidia watu watumie Biblia yao wenyewe kumkaribia Mungu.” Soma fungu la 1 kwenye ukurasa wa 16.
◼ Ukiwa na Biblia mkononi, sema: “Leo ukosefu wa haki umezidi. Ni kama tu inavyofafanuliwa hapa. [Soma Mhubiri 8:9b.] Watu wengi wanajiuliza kama kweli Mungu anajali. [Soma sentensi mbili za kwanza za fungu la 4 kwenye ukurasa wa 119.] Sura hii yaelezea ni kwa nini Mungu ameruhusu ukosefu wa haki kwa muda fulani.”
-