Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/04 uku. 1
  • Vijana—Someni Neno la Mungu!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Vijana—Someni Neno la Mungu!
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nini Kinachokuongoza Unapofanya Maamuzi ya Kibinafsi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Vijana, Je, Mnatanguliza Malengo ya Kiroho Maishani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Vijana—Fanyeni Moyo wa Yehova Ushangilie
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Onyesha Imani​—Amua kwa Hekima!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 4/04 uku. 1

Vijana—Someni Neno la Mungu!

1 Ujana ni wakati wa matatizo na wa kufanya maamuzi mazito. Kila siku, ninyi vijana Wakristo hukabili mikazo ya kuvunja kanuni za Mungu za mwenendo. Kabla ya kufanya maamuzi kuhusu elimu, kazi, na ndoa, weka kwanza miradi ya kiroho. Kwa kufanya hivyo, utaweza kufanya maamuzi mengine yatakayokunufaisha maishani. Miradi hususa ya kiroho itakusaidia utende kwa hekima na kufanikiwa maishani. Kusoma na kutafakari Neno la Mungu kwa ukawaida kutakuchochea kufuata shauri lake liliongozwa na roho na hivyo jitihada zako zitafanikiwa.—Yos. 1:8; Zab. 1:2, 3.

2 Utanufaikaje? Ulimwengu wa Shetani umejaa vishawishi vingi vya kufanya mabaya. (1 Yoh. 2:15, 16) Huenda unajua wanashule wenzako au vijana wengine wa rika lako ambao wamepatwa na msiba kwa sababu ya kukubali kushawishiwa na marika zao. Kufuata shauri la Biblia kutakuimarisha kiadili na kiroho ili ukatae mwenendo wenye dhambi. Pia, shauri la Neno la Mungu litakusaidia kuepuka mitego isiyoonekana ya Shetani. (2 Kor. 2:11; Ebr. 5:14) Kutembea katika njia ya Mungu kutakuletea furaha ya kweli na utaridhika na maisha yako.—Zab. 119:1, 9, 11.

3 Kanuni za Neno la Mungu zisizobadilika zinapita hekima ya wanadamu. (Zab. 119:98-100) Kujua kanuni za Biblia na kutafakari makusudi ya Yehova yaliyofunuliwa, pamoja na kusali kutoka moyoni kunaweza kukusaidia kujenga uhusiano wa karibu na Yehova Mungu, Mtungaji wa Biblia aliye na hekima yote. Anaahidi hivi: “Nitakufanya uwe na ufahamu na kukufundisha katika njia unayopaswa kuiendea. Nitakupa shauri jicho langu likiwa linakutazama.”—Zab. 32:8.

4 Panga Wakati wa Kusoma Biblia: Kijana mmoja Mkristo aliweka mradi wa kusoma Biblia nzima, naye alifanya hivyo kwa mwaka mmoja. Alinufaikaje? Anasema: “Nilijifunza mambo mengi kumhusu Yehova. Mambo hayo yalinifanya nimkaribie na kutaka kumwogopa maisha yangu yote.” (Yak. 4:8) Je, umeisoma Biblia nzima? Ikiwa hujafanya hivyo, mbona usiweke mradi huo? Bila shaka Yehova atabariki jitihada zako, na utapata baraka nyingi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki