Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/04 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Aprili 12
  • Juma Linaloanza Aprili 19
  • Juma Linaloanza Aprili 26
  • Juma Linaloanza Mei 3
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 4/04 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Aprili 12

Wimbo 93

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6, panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 15 na Amkeni! la Machi 22. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe ingawa ni moja tu litakalozungumziwa. Katika kila onyesho, onyesha njia tofauti ya kushughulikia kizuia-mazungumzo “Nina shughuli.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 19-20.

Dak. 15: “Kumpa Yehova Kilicho Bora.”a Mnapozungumzia fungu la 4, waombe wasikilizaji waeleze njia hususa za kuwaonyesha watu upendo tunapowahubiria.

Dak. 20: “Mahubiri ya Simu Yenye Matokeo.”b Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Omba maelezo kutoka kwa wale wanaohubiri kupitia simu katika kutaniko lenu. Katika maeneo ambapo haiwezekani kuhubiri kupitia simu, simulia mambo yaliyoonwa katika gazeti la Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1990, ukurasa wa 25-27, kuhusu kuwahubiria watu wa ukoo. Wahoji wahubiri ambao wamefanikiwa kuwahubiria watu wa ukoo kwa maneno na mwenendo wao.

Wimbo 91 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 19

Wimbo 55

Dak. 8: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.

Dak. 17: “Iga Mtazamo wa Akili wa Yesu.”c Tumia maswali yaliyo kwenye makala. Mnapozungumzia fungu la 4, waombe wale wanaofanya upainia msaidizi waeleze baraka ambazo wamepata.

Dak. 20: Kuripoti Utumishi Wetu wa Shambani Kila Mwezi. Ikiwa mtu atakuwa mbali na kutaniko kwa muda, zungumzia njia ambazo anaweza kutumia kuhakikisha kwamba ripoti inamfikia mwandishi kwa wakati. Ripoti inaweza kutumwa kupitia simu ikiwa ipo au kwa njia ya posta. Waangalizi wa Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko wanaweza kuwasaidia wahubiri wote washiriki kwa ukawaida katika huduma. Eleza ukawaida wa kutaniko katika kushiriki huduma ya shambani na ukitumia Ufunuo 7:15 watie moyo wote wahubiri kwa ukawaida.

Wimbo 80 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 26

Wimbo 46

Dak. 12: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi za Aprili. Taja toleo la vichapo la Mei. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6, panga kuwe na maonyesho ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1 na Amkeni! la Aprili 8. Katika kila onyesho, magazeti yote mawili yatolewe, ingawa ni moja tu litakalozungumziwa. Katika onyesho moja, Shahidi anamhubiria mfanyakazi au mwanashule mwenzake.

Dak. 15: Mahitaji ya kwenu na hotuba, “Panda kwa Wingi Lakini kwa Busara.” Kazia mambo ambayo yatafaa eneo lenu.

Dak. 18: Waangalizi wa Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko Wanavyoonyesha Wanapendezwa na Watu Binafsi. Mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko azungumza pamoja na wasikilizaji habari kutoka Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 2002.

Wimbo 38 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 3

Wimbo 48

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Taja kifupi mipango ya kawaida inayofanywa wakati wa likizo: kuhudhuria kusanyiko la wilaya, kufanya upainia msaidizi, kurekebisha vitu nyumbani, na labda kuwa na tafrija. Ikiwa kutaniko lina eneo lisilohubiriwa kwa ukawaida, taja mipango ambayo imefanywa kuhubiri kabisa eneo hilo. Mipango hususa inapaswa kufanywa ili kuhakikisha kwamba funzo la familia, mikutano ya kutaniko, na utumishi wa shambani hazipuuzwi hata kama utasafiri au utendaji mwingine utavuruga mipango yako ya kawaida. (Met. 21:5) Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani, iwe watakuwapo au watasafiri.

Dak. 15: “Vijana—Someni Neno la Mungu!”d Panga mapema kijana mmoja au wawili waeleze kuhusu ratiba yao ya kusoma Biblia na jinsi ambavyo wamenufaika. Watie moyo vijana wawe na mradi wa kuisoma Biblia nzima. Tia ndani maelezo kutoka kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 10, fungu la 4.

Dak. 20: Je, Unatimiza Huduma Yako Kikamili? Hotuba pamoja na mazungumzo na wasikilizaji. Ona Huduma Yetu ya Ufalme, Septemba 2001, ukurasa wa 1. Watie moyo akina ndugu waweke maandishi mazuri ya nyumba kwa nyumba na kuwarudia wale waliopendezwa wakiwa na lengo la kuanzisha mafunzo ya Biblia.

Wimbo 164 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

d Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki