-
Jinsi ya Kuhubiri Katika Eneo la BiasharaHuduma ya Ufalme—2004 | Julai
-
-
Jinsi ya Kuhubiri Katika Eneo la Biashara
1 Je, ungependa kuhubiri katika eneo ambalo watu kwa kawaida huwakaribisha wageni na lina watu nyakati zote? Unaweza kufanya hivyo papo hapo katika eneo la kutaniko lenu. Jinsi gani? Kwa kutembelea maduka ya mahali hapo. Wahubiri wanaohubiri duka kwa duka mara nyingi hufurahia matokeo mazuri.
2 Makutaniko fulani yamegawiwa maeneo ya biashara. Ndugu anayeshughulikia maeneo anaweza kutayarisha kadi za ramani za pekee kwa ajili ya sehemu hizo za biashara zenye watu wengi sana. Kadi zozote za eneo la makao linaloshikana na eneo la biashara zinapasa kuonyesha waziwazi kwamba eneo la biashara halipasi kuhubiriwa pamoja na eneo la makao. Katika maeneo mengine, maeneo ya biashara yanaweza kuhubiriwa pamoja na maeneo ya makao. Ikiwa hujawahi kuhubiri eneo la biashara, anza kwa kuhubiri maduka machache madogo.
3 Tumia Njia Rahisi: Unapohubiri duka kwa duka, ni muhimu uvalie kana kwamba unakwenda mkutanoni kwenye Jumba la Ufalme. Pia inafaa uende wakati ambapo hakuna shughuli nyingi dukani. Kama inawezekana, ingia wakati ambapo hakuna wateja wanaongoja kuhudumiwa. Omba uzungumze na msimamizi. Sema kwa ufupi na utaje kusudi waziwazi. Unaweza kusema nini?
4 Unapoongea na mwenye duka au msimamizi, unaweza kusema hivi: “Wafanyabiashara ni watu wenye shughuli nyingi sana hivi kwamba mara nyingi hatuwapati nyumbani, kwa hiyo tunakutembelea kazini. Magazeti yetu yanazungumzia matukio ya sasa yanayohusu ulimwengu.” Kisha onyesha jambo moja fupi kutoka katika gazeti moja.
5 Au unaweza kujaribu njia hii rahisi: “Watu wengi wangependa kujua mengi zaidi kuhusu Biblia lakini hawana wakati wa kutosha. Trakti hii inaeleza mpango wa kujifunza Biblia bila malipo ambao unaweza kukusaidia kupata majibu ya maswali yako ya Biblia.” Kisha mwonyeshe ukurasa wa 4-5 wa trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia?
6 Ikiwa mwenye duka anaonekana kuwa na shughuli nyingi, unaweza kumpa trakti tu na kusema: “Nitarudi tena wakati shughuli zako zimepungua. Ningependa kujua maoni yako kuhusu trakti hii.”
7 Kuendeleza Upendezi: Hata huenda ukaongoza funzo la Biblia katika eneo la biashara. Painia wa pekee alimpelekea mfanyabiashara mmoja magazeti kwa ukawaida. Mtu huyo alipoonyesha kupendezwa na yale aliyokuwa akisoma, painia huyo alimwonyesha jinsi ya kujifunza, akitumia broshua Anataka. Funzo lilianzishwa hapohapo kazini kwa mtu huyo. Kwa kufikiria hali za mtu huyo, painia huyo alitumia dakika 10 au 15 kila wakati. Sisi pia na twendelee kuwatafuta wanaostahili kwa kuhubiri eneo la biashara.
-
-
Habari Za KitheokrasiHuduma ya Ufalme—2004 | Julai
-
-
Habari Za Kitheokrasi
◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:
Kenya: Athi River, Buhuyi, na Machakos.
Sudan: Port Sudan North.
Tanzania: Iporoto, Kibaha, na Vwawa-Kusini.
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu MagazetiHuduma ya Ufalme—2004 | Julai
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Je, unakubali kwamba ni kazi ngumu kulea watoto katika ulimwengu wa sasa? [Ngoja jibu.] Angalia jinsi tunavyohakikishiwa kwamba wazazi wanaweza kufanikiwa. [Soma Methali 22:6.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linatoa ushauri unaofaa ili kuwasaidia wazazi wakabiliane na ugumu huo.”
Amkeni! Juni 22
“Watu wengine wana maoni kwamba si jambo la kisayansi kumwamini Mungu. Lakini ulijua kwamba kuna wanasayansi wanaosema kwamba kwa kweli sayansi huunga mkono imani katika Muumba? [Ngoja jibu.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia baadhi ya uthibitisho ambao umewafanya wafikie uamuzi huo.” Soma Waroma 1:20.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Wakati wa msiba, wengi hujiuliza kama kweli Mungu anawajali watu na kuona mateso yao. Je, umewahi kujiuliza hivyo? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu anavyotujali leo na jinsi ambavyo ameandaa msingi wa kuondoa mateso yote.” Soma Yohana 3:16.
Amkeni! Julai 8
“Kwa watu wengi, miaka ya utineja ni wakati wa shangwe na magumu, sivyo? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linazungumzia mabadiliko yanayowapata vijana wanaobalehe. Pia linazungumzia ushauri wenye hekima unaoweza kuwasaidia watumie kwa njia bora zaidi miaka yao ya ujanani.” Soma Mhubiri 12:1.
-