Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Je, unakubali kwamba ni kazi ngumu kulea watoto katika ulimwengu wa sasa? [Ngoja jibu.] Angalia jinsi tunavyohakikishiwa kwamba wazazi wanaweza kufanikiwa. [Soma Methali 22:6.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linatoa ushauri unaofaa ili kuwasaidia wazazi wakabiliane na ugumu huo.”
Amkeni! Juni 22
“Watu wengine wana maoni kwamba si jambo la kisayansi kumwamini Mungu. Lakini ulijua kwamba kuna wanasayansi wanaosema kwamba kwa kweli sayansi huunga mkono imani katika Muumba? [Ngoja jibu.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia baadhi ya uthibitisho ambao umewafanya wafikie uamuzi huo.” Soma Waroma 1:20.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Wakati wa msiba, wengi hujiuliza kama kweli Mungu anawajali watu na kuona mateso yao. Je, umewahi kujiuliza hivyo? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu anavyotujali leo na jinsi ambavyo ameandaa msingi wa kuondoa mateso yote.” Soma Yohana 3:16.
Amkeni! Julai 8
“Kwa watu wengi, miaka ya utineja ni wakati wa shangwe na magumu, sivyo? [Ngoja jibu.] Gazeti hili linazungumzia mabadiliko yanayowapata vijana wanaobalehe. Pia linazungumzia ushauri wenye hekima unaoweza kuwasaidia watumie kwa njia bora zaidi miaka yao ya ujanani.” Soma Mhubiri 12:1.