Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Je, unafikiri tunaweza kuwa na furaha ingawa tunakabili matatizo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha chanzo cha mwongozo ambao unaweza kutusaidia kukabiliana kwa njia inayofaa na matatizo ya maisha. Pia linazungumzia jinsi kuwa na tumaini la kweli kunavyoweza kutuimarisha.” Soma Ufunuo 21:3, 4.
Amkeni! Juni
“Je, hukubali kwamba misiba ya hivi karibuni imetuonyesha umuhimu wa kutii maonyo? [Mruhusu ajibu.] Makala hii inazungumzia mambo ambayo waliookoka Tufani Katrina walijifunza. Pia inazungumzia onyo ambalo kila mmoja wetu leo anahitaji kutilia maanani.” Zungumzia makala inayoanza kwenye ukurasa wa 14.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Katika ulimwengu wa leo uliojaa matatizo, watu wengi wanauliza hivi: ‘Kwa nini kuna matatizo mengi sana maishani? Ikiwa kuna Mungu, kwa nini hafanyi jambo lolote kukomesha kuteseka?’ Je, umewahi kujiuliza maswali hayo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia majibu ya Biblia yenye kupendeza kwa maswali hayo.” Soma 2 Timotheo 3:16.
Amkeni! Julai
“Leo ndoa nyingi sana zinakabili hali ngumu. Je, unafikiri wenzi wa ndoa watafaidika kwa kutumia shauri hili la Biblia? [Soma Waefeso 4:32. Kisha mruhusu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia kanuni za Biblia ambazo zimejaribiwa kwa muda mrefu na ambazo zinaweza kutusaidia kuwa na ndoa yenye furaha.”