-
Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha MbalimbaliHuduma ya Ufalme—2003 | Julai
-
-
Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali
1 Maeneo mengi yana watu kutoka nchi nyingine. Wengi wao hujifunza kweli haraka na kuielewa kwa undani wanapofundishwa katika lugha yao wenyewe. Kuna mipango gani ya kuwapa wanaopendezwa vichapo vya Biblia katika lugha wanayoielewa vizuri zaidi?
2 Wakati wa Kutoa Vichapo: Makutaniko mawili au zaidi ya lugha tofauti yanapohubiri eneo lilelile, mabaraza ya wazee yanayohusika yatashirikiana na waangalizi wa utumishi kufanya mipango inayofaa ili kuhakikisha kwamba watu wa kila lugha wamehubiriwa kikamili. Nyakati nyingine huenda hiyo ikatia ndani kubadilishana maeneo fulani mara kwa mara. Unapomwachia mtu anayependezwa vichapo na kumrudia, tafadhali hakikisha kwamba unamwelekeza mwenye nyumba kwenye mikutano ya kutaniko linalotumia lugha anayoelewa vizuri zaidi au anayopenda.—Ona Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1990.
3 Wakati wa Kuweka Vichapo Akibani: Ni nini linaloweza kufanywa ikiwa kuna watu wengi wanaoongea lugha ya kigeni katika eneo fulani lakini hakuna kutaniko la lugha hiyo? Katika hali hizo, makutaniko yanaweza kuwa na vichapo kadhaa vya msingi vya lugha hiyo, kama vile trakti, broshua Anataka, na Rafiki ya Mungu, na kitabu Ujuzi. Wahubiri wanaweza kutoa vichapo hivyo wanapokutana na watu wanaoweza kusoma lugha hiyo.
4 Jinsi ya Kuagiza Vichapo: Ikiwa kutaniko halina akiba ya vichapo vya lugha ambayo mtu mwenye kupendezwa anaweza kusoma, linawezaje kuagiza vichapo hivyo? Mhubiri anapaswa kuwasiliana na mtumishi wa vitabu ili kujua vichapo vilivyopo katika lugha hiyo ili vile vinavyohitajiwa viweze kuagizwa katika ombi la vitabu lifuatalo la kutaniko.
5 Ikiwa vichapo hivyo vinahitajiwa haraka, mhubiri anaweza kumwomba mshiriki wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ikiwa ombi hilo linaweza kutumwa kabla ya ombi la vitabu lifuatalo la kutaniko. Akikubali, mratibu wa vitabu au mtu mwingine aliyeteuliwa naye anaweza kufanya ombi la haraka kupitia barua au kupiga simu kwenye ofisi ya tawi. Vichapo hivyo vitatumwa kwenye kutaniko kwa njia ya kawaida, au mkipenda, vitatumwa mahali pa muda pa kupeleka vitabu. Ikiwa kutaniko linaomba litumiwe vitabu kwa njia ya pekee, litadaiwa malipo ya usafirishaji.
6 Na tutumie ifaavyo vichapo vyetu vya Kikristo kuwasaidia “watu wa namna zote,” licha ya lugha yao, ‘kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli na kuokolewa.’—1 Tim. 2:3, 4.
-
-
Habari za KitheokrasiHuduma ya Ufalme—2003 | Julai
-
-
Habari za Kitheokrasi
◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:
Burundi: Bujumbura Kamenge na Bujumbura Kanyosha/Kinindo.
Kenya: Mukuyuni, Nyahururu Mashariki, Nzaikoni, na Thika Kusini.
Sudan: Gadarif na Shigla.
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu MagazetiHuduma ya Ufalme—2003 | Julai
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Watu wengine huona kwamba Yesu ndiye mtu mkuu zaidi katika historia. Wengine hutilia shaka kama kweli aliwahi kuishi. Je, wafikiri ni muhimu kumwamini? [Baada ya jibu, soma Matendo 4:12.] Kuna uthibitisho gani kwamba kweli Yesu aliwahi kuishi duniani? Gazeti hili lajibu swali hilo.”
Amkeni! Juni 22
“Watu wengi wanahangaika sana kuhusu mazingira. Je, wafikiri kwamba inawezekana kuhifadhi misitu ya mvua ulimwenguni? [Ngoja jibu.] Gazeti hili laeleza jitihada ambazo zimefanywa hivi karibuni ili kuokoa misitu ya mvua. Pia lazungumzia jinsi ahadi hiyo nzuri ya Mungu itakavyotimizwa.” Soma Isaya 11:9.
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Mojawapo ya mahitaji yetu ya msingi tukiwa wanadamu ni kupenda na kupendwa. [Soma maelezo ya picha iliyo kwenye ukurasa wa 4.] Lakini, je umegundua kwamba jamii ya sasa hupenda kutanguliza mambo mengine? [Ngoja jibu.] Gazeti hili lazungumzia upendo wa kweli na jinsi ya kuustawisha.” Soma 1 Wakorintho 13:2.
Amkeni! Julai 8
“Watu wengi wanasumbuliwa na ongezeko la jeuri. [Taja mfano mmoja unaojulikana kwenu, na ungoje jibu.] Gazeti hili lachunguza baadhi ya mambo yanayosababisha jeuri. Pia laeleza jinsi Mungu atakavyokomesha uhalifu na jeuri kabisa.” Soma Zaburi 37:10, 11.
-