Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/03 uku. 4
  • Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Kuwahubiria Watu Wanaozungumza Lugha ya Kigeni
    Huduma ya Ufalme—2009
  • Tumia kwa Hekima Vichapo Vyetu Vinavyotegemea Biblia
    Huduma ya Ufalme—2005
  • Je! Wewe Unathamini Fasihi Yetu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Sanduku La Swali
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 7/03 uku. 4

Kutoa Vichapo Katika Eneo Lenye Lugha Mbalimbali

1 Maeneo mengi yana watu kutoka nchi nyingine. Wengi wao hujifunza kweli haraka na kuielewa kwa undani wanapofundishwa katika lugha yao wenyewe. Kuna mipango gani ya kuwapa wanaopendezwa vichapo vya Biblia katika lugha wanayoielewa vizuri zaidi?

2 Wakati wa Kutoa Vichapo: Makutaniko mawili au zaidi ya lugha tofauti yanapohubiri eneo lilelile, mabaraza ya wazee yanayohusika yatashirikiana na waangalizi wa utumishi kufanya mipango inayofaa ili kuhakikisha kwamba watu wa kila lugha wamehubiriwa kikamili. Nyakati nyingine huenda hiyo ikatia ndani kubadilishana maeneo fulani mara kwa mara. Unapomwachia mtu anayependezwa vichapo na kumrudia, tafadhali hakikisha kwamba unamwelekeza mwenye nyumba kwenye mikutano ya kutaniko linalotumia lugha anayoelewa vizuri zaidi au anayopenda.—Ona Sanduku la Swali katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1990.

3 Wakati wa Kuweka Vichapo Akibani: Ni nini linaloweza kufanywa ikiwa kuna watu wengi wanaoongea lugha ya kigeni katika eneo fulani lakini hakuna kutaniko la lugha hiyo? Katika hali hizo, makutaniko yanaweza kuwa na vichapo kadhaa vya msingi vya lugha hiyo, kama vile trakti, broshua Anataka, na Rafiki ya Mungu, na kitabu Ujuzi. Wahubiri wanaweza kutoa vichapo hivyo wanapokutana na watu wanaoweza kusoma lugha hiyo.

4 Jinsi ya Kuagiza Vichapo: Ikiwa kutaniko halina akiba ya vichapo vya lugha ambayo mtu mwenye kupendezwa anaweza kusoma, linawezaje kuagiza vichapo hivyo? Mhubiri anapaswa kuwasiliana na mtumishi wa vitabu ili kujua vichapo vilivyopo katika lugha hiyo ili vile vinavyohitajiwa viweze kuagizwa katika ombi la vitabu lifuatalo la kutaniko.

5 Ikiwa vichapo hivyo vinahitajiwa haraka, mhubiri anaweza kumwomba mshiriki wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ikiwa ombi hilo linaweza kutumwa kabla ya ombi la vitabu lifuatalo la kutaniko. Akikubali, mratibu wa vitabu au mtu mwingine aliyeteuliwa naye anaweza kufanya ombi la haraka kupitia barua au kupiga simu kwenye ofisi ya tawi. Vichapo hivyo vitatumwa kwenye kutaniko kwa njia ya kawaida, au mkipenda, vitatumwa mahali pa muda pa kupeleka vitabu. Ikiwa kutaniko linaomba litumiwe vitabu kwa njia ya pekee, litadaiwa malipo ya usafirishaji.

6 Na tutumie ifaavyo vichapo vyetu vya Kikristo kuwasaidia “watu wa namna zote,” licha ya lugha yao, ‘kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli na kuokolewa.’—1 Tim. 2:3, 4.

[Maswali ya Funzo]

1. Kwa nini makutaniko mengi yanahitaji vichapo vya lugha za kigeni?

2. Makutaniko mawili au zaidi ya lugha tofauti yanayohubiri eneo lilelile yanapaswa kushirikiana kwa njia gani?

3. Kutaniko linaweza kuweka akiba ya vichapo vya lugha ya kigeni wakati gani?

4. Kutaniko linawezaje kuagiza vichapo vya lugha nyingine?

5. Ni nini kinachoweza kufanywa ikiwa vichapo vinahitajiwa kabla ombi la kutaniko kufika?

6. Tuwe na mradi gani tunapotoa vichapo vya Kikristo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki