Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/05 uku. 3
  • Watu wa Namna Zote Wataokolewa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watu wa Namna Zote Wataokolewa
  • Huduma ya Ufalme—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Je! Wewe Huona Sura ya Nje-Nje Tu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Je, Wewe Huona Tu Sura ya Nje?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Usihukumu kwa Kutazama Sura ya Nje
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Je, Unawaona Wengine Kama Yehova Anavyowaona?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Huduma ya Ufalme—2005
km 4/05 uku. 3

Watu wa Namna Zote Wataokolewa

1 Fadhili zisizostahiliwa za Mungu zimewapa watu fursa ya kupata wokovu. Ni mapenzi ya Yehova kwamba “watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:3, 4) Uhusiano wetu pamoja na Mungu hautegemei rangi, cheo, vipawa, wala sura yetu, bali unategemea imani yetu katika dhabihu ya fidia ya Yesu. (Yoh. 3:16, 36) Kwa kuwa sisi ni wafanyakazi wenzi wa Mungu, ni lazima tuache kabisa ubaguzi ambao unaweza kutushawishi tuwakatae watu ambao Yehova yu tayari kuwakubali.

2 Usihukumu: Yehova anachunguza mioyo ya watu bila chuki wala ubaguzi. (1 Sam. 16:7) Pia, anatambua kwamba wanaweza kubadilika. Kwa hiyo anawaona watu wanaotaka kupata kibali chake kuwa wenye kutamanika. (Hag. 2:7) Je, tunawaona watu kama Mungu anavyowaona?

3 Huenda tukashtuliwa na sura za baadhi ya watu tunaowakuta katika huduma yetu. Labda wamevalia kizembe au isivyofaa, hawajatunza ndevu zao au wana vipuli puani au midomoni. Huenda baadhi yao hawana makao. Wengine wanaweza kuwa wakali tunapowahubiria. Hatupaswi kamwe kuwa na maoni kwamba watu hao hawawezi kuwa waabudu wa Yehova kwa maana “hata sisi wakati mmoja tulikuwa watu wasio na akili, wasiotii, tukipotoshwa.” (Tito 3:3) Tukikumbuka jambo hilo, tutakuwa na hamu ya kumhubiria kila mtu, hata wale wanaoonekana kuwa wasiostahili kwa sababu ya sura zao.

4 Mifano ya Karne ya Kwanza: Yesu Kristo aliwasaidia watu wote hata wale ambao huenda wengine walifikiri kwamba hawangeweza kamwe kuwa waabudu wa Yehova. (Luka 8:26-39) Ijapokuwa hakukubali kamwe mazoea mabaya, alielewa kwamba watu wanaweza kujiingiza katika mwenendo mbaya bila kujua. (Luka 7:37, 38, 44-48) Kwa hiyo, alielewa hali yao na “akawasikitikia, kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji.” (Marko 6:34) Je, tunaweza kuiga mfano wake vizuri zaidi?

5 Mtume Paulo alipigwa kwa mawe na kwa fimbo, na kufungwa gerezani. (Mdo. 14:19; 16:22, 23) Je, magumu hayo yalimfanya audhike na kukata kauli kwamba alikuwa akipoteza wakati kuwahubiria watu wa mataifa na makabila fulani? Hata kidogo. Alijua kwamba watu wenye mioyo myeupe wangepatikana miongoni mwa watu wa makabila yote, naye aliazimia kuwapata. Je, hivyo ndivyo tunavyowaona watu wa malezi na tamaduni mbalimbali katika eneo letu?

6 Kuwakaribisha Watu Leo: Wengi miongoni mwa watu wa Mungu wanashukuru kwamba walikaribishwa katika kutaniko na ndugu na dada bila kujali sura zao. Mtu mmoja mwenye nywele ndefu zilizofika mabegani, ndevu nyingi zisizotunzwa, na mavazi machafu alienda kwenye Jumba la Ufalme fulani nchini Ujerumani. Alikuwa na sifa mbaya. Hata hivyo alikaribishwa kwa uchangamfu mkutanoni. Alivutiwa sana hivi kwamba akarudi juma lililofuata. Muda si muda alianza kuvalia na kujipamba vizuri, akaacha kuvuta sigara, na akafunga ndoa na msichana aliyekuwa rafiki yake. Muda mfupi baadaye, yeye, mke wake, na watoto wao wakaanza kumtumikia Yehova pamoja.

7 Tumwige Mungu wetu asiye na ubaguzi kwa kuwaalika wote waje ili wanufaike na fadhili zisizostahiliwa za Mungu.

[Maswali ya Funzo]

1. Uhusiano wetu pamoja na Mungu unategemea nini?

2, 3. Kwa nini hatupaswi kuwahukumu watu kwa sababu ya sura zao?

4, 5. Mfano wa Yesu na wa Paulo unatufundisha nini?

6. Mtazamo wetu unaweza kuwavutiaje wapya wanaohudhuria mikutano ya kutaniko?

7. Tunawezaje kumwiga Mungu wetu asiye na ubaguzi?

[Blabu katika ukurasa wa 3]

“Mungu hana ubaguzi, bali katika kila taifa mtu ambaye anamwogopa na kutenda uadilifu anakubalika kwake.”—Mdo. 10:34, 35.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki