-
Waangalizi wa Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko Wanavyoonyesha Wanapendezwa na Watu BinafsiHuduma ya Ufalme—2002 | Oktoba
-
-
Waangalizi wa Mafunzo ya Kitabu ya Kutaniko Wanavyoonyesha Wanapendezwa na Watu Binafsi
1 Funzo la Kitabu la Kutaniko limekusudiwa kufanya ‘iwezekane kila mtu apewe msaada wa kibinafsi apate kukua kiroho. . . Huo ni wonyesho wa fadhili za upendo za Yehova na utunzaji wake mpole wa watu wake.’ (om uku. 75; Isa. 40:11) Mwangalizi wa funzo la kitabu hutimiza daraka muhimu kwa kupendezwa na watu binafsi.
2 Kwenye Funzo la Kitabu: Kwa kuwa vikundi vya funzo la kitabu vimekusudiwa kuwa vidogo, mwangalizi wa funzo la kitabu anaweza kujua washiriki wa kikundi chake vizuri. (Mit. 27:23) Kwa kawaida, kuna fursa za kuzungumza kabla au baada ya funzo kila juma. Katika kipindi cha mwezi mmoja, huenda akaweza kuzungumza na kila mtu katika kikundi hicho. Hilo husaidia washiriki wa funzo la kitabu wahisi huru kumfikia wakiwa na majaribu au wakihitaji kutiwa moyo.—Isa. 32:2.
3 Mwangalizi wa funzo la kitabu hujaribu kumtia moyo kila mtu katika kikundi chake ashiriki wakati wa funzo. Njia moja ya kufanya hivyo ni kwa kuongoza funzo kwa fadhili na upole. (1 The. 2:7, 8) Yeye hutafuta njia za kuhusisha kila mtu katika mazungumzo, kutia ndani wachanga. Ikiwa kuna wengine wanaoona haya kutoa maelezo, anaweza kuwasaidia faraghani kwa kupanga mapema ili wasome andiko au watoe maelezo katika fungu hususa. Au huenda akawaonyesha jinsi ya kutoa maelezo kwa maneno yao wenyewe.
4 Ikiwa msaidizi wa mwangalizi wa funzo la kitabu ni mtumishi wa huduma, mwangalizi atapanga ili mtumishi huyo aongoze funzo mara moja baada ya kila miezi miwili. Hiyo itampa fursa mwangalizi kuangalia jinsi msaidizi anavyoliongoza funzo la kitabu na kumpa madokezo muhimu. Huo ni mpango mzuri sana wa kuwasaidia akina ndugu waboreshe ustadi wao wa kufundisha.—Tito 1:9.
5 Katika Huduma ya Shambani: Mojawapo ya madaraka makuu ya mwangalizi wa funzo la kitabu ni kuongoza katika kazi ya kueneza injili. (Hes. 27:16, 17) Yeye hufanya mipango inayofaa ili kikundi kihubiri, naye hujitahidi kusaidia kikundi kipate shangwe katika huduma yao. (Efe. 4:11, 12) Ili kutimiza hilo, yeye huweka mradi wa kuhubiri na kila mshiriki wa kikundi. Pia yeye hupanga na mwangalizi wa utumishi ili kusaidia wale ambao wangetaka kuboresha huduma yao kwa njia fulani wapate msaada kutoka kwa mhubiri mwenye uzoefu.
6 Kama Mchungaji Mwenye Upendo: Mwangalizi wa funzo la kitabu anapendezwa na wale ambao hushiriki kwa kiwango kidogo katika kazi ya kuhubiri kwa sababu ya hali zao. Anahakikisha kwamba wale ambao wamepungukiwa kwa sababu ya umri mkubwa au kwa sababu ya kutojiweza kwa sababu ya ugonjwa au majeraha mabaya zaidi wanajulishwa mipango itakayowaruhusu kuripoti vipindi vya dakika 15 kama hawawezi kuripoti saa nzima-nzima. (Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ndiyo inayoamua ni nani anayestahili mpango huo.) Mwangalizi wa funzo la kitabu la kutaniko anapendezwa na watu wa kikundi hicho ambao huenda si watendaji, akijitahidi kuwasaidia warudie utendaji wao na kutaniko.—Luka 15:4-7.
7 Tunashukuru kama nini kwa sababu ya upendezi wenye upendo ambao waangalizi wa mafunzo ya kitabu wanatuonyesha! Uangalifu wanaotupatia binafsi hutusaidia “sote tuufikie umoja katika imani. . . , na kufikia kipimo cha kimo ambacho ni cha ujao wa Kristo.”—Efe. 4:13.
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu MagazetiHuduma ya Ufalme—2002 | Oktoba
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
“Mamilioni ya watu huamini kwamba ‘watakatifu’ wana nguvu ya pekee na kwamba inafaa kuomba kupitia kwao. Wafikirije? [Ngoja ajibu.] Ona vile Yesu alivyosema. [Soma Yohana 14:6.] Hilo hufanya wengi wajiulize kama inafaa kusali kupitia ‘watakatifu.’ Toleo hili la Mnara wa Mlinzi lazungumzia habari hiyo muhimu.”
Amkeni! Sept. 22
“Watu wengi leo wanahangaishwa na ugaidi, kutia ndani matumizi ya silaha za kibiolojia. Je, wafikiri kwamba serikali za kibinadamu zaweza kukomesha ugaidi katika ulimwengu huu? [Ngoja ajibu.] Biblia huonyesha kile ambacho Mungu anakusudia kufanya. [Soma Ezekieli 34:28.] Gazeti hili la Amkeni! lachunguza baadhi ya masuala yanayohusika.”
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Watu wengi wamejiuliza kama kutakuwako na wakati ambapo matatizo yote tunayoona kama vile vita, uhalifu, na vitendo vya ugaidi vitakoma kabisa. Wafikirije? [Ngoja ajibu.] Biblia yatoa uhakikisho huu wenye kufariji. [Soma Zaburi 37:10, 11.] Gazeti hili laeleza sababu gani Mungu hajakomesha uovu na mateso yanayotokana nao.”
Amkeni! Okt. 8
“Inaonekana kwamba leo kuna ongezeko kubwa zaidi la idadi ya familia zenye mzazi mmoja. Biblia yaonyesha kwamba Muumba wetu anawahurumia. [Soma Zaburi 146:9.] Toleo hili la Amkeni! laonyesha jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kuwasaidia wazazi kulea watoto wao kwa mafanikio.”
-