Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Mlangoni na Kupitia Simu Inapowezekana au Kupitia Barua
    Huduma ya Ufalme—2005 | Agosti
    • Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Mlangoni na Kupitia Simu Inapowezekana au Kupitia Barua

      1 Watu wana shughuli nyingi leo. Hata hivyo, wengi wao wanapendezwa na mambo ya kiroho. Tunawezaje kuwasaidia watosheleze uhitaji wao wa kiroho? (Mt. 5:3) Wahubiri wengi wanaweza kuwafunza watu Biblia mlangoni pao. Wanaweza pia kuwafunza kupitia simu au barua. Je, unaweza kutumia njia hizo kuwahubiria watu wengi zaidi?

      2 Ili kuanzisha mafunzo ya Biblia, tunahitaji kuwa tayari kutumia fursa yoyote tunayopata kumwonyesha mtu jinsi funzo la Biblia linavyoongozwa. Tunaweza kufanya hivyo wapi na jinsi gani?

      3 Mlangoni: Unapokutana na mtu ambaye yuko tayari kuzungumzia Biblia, fungua ukurasa wenye fungu ambalo umetayarisha mapema. Unaweza kutumia fungu la kwanza katika somo la kwanza la broshua Anataka. Soma fungu hilo, uliza swali, kisha uzungumzie andiko moja au mawili. Mara nyingi unaweza kufanya hivyo palepale mlangoni kwa muda wa dakika tano au kumi. Ikiwa mtu huyo anafurahia mazungumzo, fanya mpango wa kuzungumzia fungu moja au mawili wakati mwingine.—Mapendekezo mengine ya kuanzisha mafunzo moja kwa moja yanapatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002, uku. 6.

      4 Tunaweza kutumia njia hiyo kuanzisha mafunzo ya Biblia tunapofanya ziara za kurudia. Kwa mfano, unaweza kumwonyesha mtu broshua Anataka na kuzungumzia jina la Mungu ukitumia somo la 2, fungu la 1-2. Katika ziara inayofuata, unaweza kumwonyesha yale Biblia inayosema kuhusu sifa za Yehova, ukitumia fungu la 3-4. Unapomtembelea tena, unaweza kuzungumzia fungu la 5-6 na kutumia picha iliyo kwenye ukurasa wa 5 kumwonyesha jinsi kujifunza Biblia kunavyotusaidia kumjua Yehova. Tunaweza kufanya hivyo tukiwa tumesimama mlangoni.

      5 Kupitia Simu au Barua: Huenda watu fulani wakakubali kujifunza Biblia kupitia simu badala ya kujifunza uso kwa uso. Fikiria kisa hiki: Dada mmoja alipokuwa akihubiri nyumba kwa nyumba, alikutana na mwanamke mmoja kijana ambaye ni mama na mfanyakazi mwenye shughuli nyingi. Dada huyo alipomkosa nyumbani mara kadhaa, aliamua kumpigia simu. Mwanamke huyo alimwambia kwamba hana wakati wa kuzungumzia Biblia. Dada huyo akamwambia: “Unaweza kujifunza jambo fulani jipya kwa dakika 10 au 15, hata kupitia simu.” Mwanamke huyo akajibu: “Ikiwa ni kupitia simu, ninakubali.” Muda si muda, walikuwa wakijifunza kwa ukawaida kupitia simu. Wahubiri wengine wamefaulu kuongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani kupitia barua. Njia hiyo imewasaidia sana wale wanaoishi mbali sana na kutaniko.

      6 Je, watu fulani unaowatembelea au unaowajua wanaweza kukubali kujifunza kupitia simu au barua? Unaweza kujaribu njia iliyoelezwa hapo juu, au unaweza kusema hivi: “Ukipenda, tunaweza kujifunza Biblia kupitia simu au barua. Je, njia hiyo itakufaa?” Tukiongoza mafunzo ya Biblia kulingana na hali za wengine, tunaweza kuwasaidia ‘wapate kumjua Mungu.’—Met. 2:5; 1 Kor. 9:23.

  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2005 | Agosti
    • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti

      Mnara wa Mlinzi Julai 15

      “Kwa maelfu ya miaka, wanadamu wametunga mafundisho mengi mbalimbali. Je, unafikiri kwamba tunaweza kutofautisha mafundisho ya kweli na ya uwongo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha mahali ambapo unaweza kupata mafundisho ya kweli ambayo yanampendeza Mungu.” Soma 2 Timotheo 3:16.

      Amkeni! Julai 22

      “Inahuzunisha sana kuona mateso yanayosababishwa na misiba ya asili. [Taja msiba fulani unaojulikana kwenu.] Je, unafikiri kwamba misiba kama hiyo inaongezeka? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linajibu swali hilo. Pia linawafariji wale ambao wamefiwa na wapendwa wao katika misiba kama hiyo.” Soma Yohana 5:28, 29.

      MNARA WA MLINZI Ago. 1

      “Watu wengi leo wanahisi kwamba hawafai. Unafikiri wanaweza kusaidiwaje? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Biblia inavyoweza kuwasaidia watu hao wapate shangwe ya kweli.” Kazia maandiko yaliyoandikwa kwa herufi nzito za mlazo katika makala “Biblia Inaweza Kukusaidia Upate Shangwe.”

      Amkeni! Ago. 8

      “Watu wengi huishi kwa woga daima. Unafikiri ni nini kinachosababisha hali hiyo ya woga? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili lina mapendekezo mazuri ya kutusaidia kujilinda tusipatwe na hatari zinazowapata watu wengi. Linazungumzia pia ahadi ya Biblia ya kuwapo kwa ulimwengu ambamo watu wataishi bila woga.” Soma Isaya 11:9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki