Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Msaada Wako Unahitajiwa
    Huduma ya Ufalme—2004 | Desemba
    • Msaada Wako Unahitajiwa

      1 “Asanteni sana kwa yote mnayofanya kwa niaba yetu. Kazi yenu hutunufaisha sana.” Maneno hayo yanaonyesha wazi shukrani zetu kwa wazee na watumishi wa huduma. Kwa kuwa tengenezo la Mungu linaendelea kupanuka, wanaume waliokomaa wanahitajiwa ili kutumikia katika makutaniko 100,000 hivi duniani. Ikiwa wewe ni ndugu aliyebatizwa, msaada wako unahitajiwa.

      2 ‘Kujitahidi’ Kufikia Mapendeleo Zaidi: Unawezaje kujitahidi ufikie mapendeleo zaidi ya utumishi? (1 Tim. 3:1) Unaweza kufanya hivyo hasa kwa kujiendesha vizuri maishani mwako. (1 Tim. 4:12; Tito 2:6-8; 1 Pet. 5:3) Shiriki kikamili katika kazi ya kuhubiri, na kuwasaidia wengine wafanye hivyo. (2 Tim. 4:5) Pendezwa kikweli na hali ya waamini wenzako. (Rom. 12:13) Jifunze Neno la Mungu kwa bidii, na usitawishe ‘ufundi wa kufundisha.’ (Tito 1:9; 1 Tim. 4:13) Shughulikia kwa bidii na kwa makini migawo unayopewa na wazee. (1 Tim. 3:10) Ikiwa wewe ni kichwa cha familia, ‘simamia nyumba yako mwenyewe kwa njia nzuri.’—1 Tim. 3:4, 5, 12.

      3 Ili kuwekwa kuwa mtumishi wa huduma au mzee, unahitaji kuwa mwenye bidii na mwenye roho ya kujitolea. (1 Tim. 5:17) Kwa hiyo, unapojitahidi kufikia mapendeleo hayo, zingatia kuwatumikia wengine kwa unyenyekevu. (Mt. 20:25-28; Yoh. 13:3-5, 12-17) Tafakari juu ya mwelekeo wa Timotheo, na ujitahidi kuuiga. (Flp. 2:20-22) Kama yeye, acha mwenendo wako mzuri ukupendekeze. (Mdo. 16:1, 2) Unapositawisha sifa za kiroho zinazohitajiwa ili kushughulikia madaraka mbalimbali, na pia kufuata ushauri wowote unaopewa ili kuboresha sifa hizo, ‘maendeleo yako yatakuwa wazi kwa watu wote.’—1 Tim. 4:15.

      4 Wazazi, Zoezeni Watoto Kusaidia: Watoto wanaweza kujifunza kusaidia wakiwa na umri mdogo. Wazoezeni kusikiliza kwenye mikutano, kuhubiri, na kuwa na mwenendo mzuri wanapokuwa kwenye Jumba la Ufalme na shuleni. Wazoezeni kuwatumikia wengine, kwa kusaidia kusafisha Jumba la Ufalme, kuwasaidia waliozeeka, na kadhalika. Acheni wapate furaha inayotokana na kutoa. (Mdo. 20:35) Mazoezi hayo yanaweza kuwasaidia wawe mapainia, watumishi wa huduma, na wazee wakati ujao.

  • Sehemu ya 4: Kuwazoeza Wanafunzi Kujitayarisha
    Huduma ya Ufalme—2004 | Desemba
    • Sehemu ya 4: Kuwazoeza Wanafunzi Kujitayarisha

      Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

      1 Kwa kawaida, mwanafunzi anayejitayarisha mapema kwa ajili ya funzo, anayepiga mistari kwenye majibu, na anayefikiria jinsi ya kutoa majibu hayo katika maneno yake mwenyewe, atafanya maendeleo ya kiroho haraka. Kwa hiyo, unapoanzisha funzo, tayarisha somo fulani pamoja na mwanafunzi ili kumwonyesha jinsi ya kufanya hivyo. Kuhusiana na wanafunzi walio wengi, itafaa kutayarisha somo au sura nzima pamoja.

      2 Kupiga Mistari na Kuandika Pambizoni: Mweleze jinsi ya kutafuta majibu ya maswali yaliyo kwenye kitabu. Mwonyeshe mwanafunzi nakala yako ya kichapo cha funzo ambacho umepiga mistari maneno au vifungu muhimu pekee. Mnapozungumzia habari hiyo, huenda mwanafunzi akataka kufuata kielelezo chako, kwa kupiga mistari maneno au vifungu muhimu katika nakala yake, ambavyo vitamsaidia kukumbuka jibu. (Luka 6:40) Kisha mwombe atoe jibu kwa maneno yake mwenyewe. Jambo hilo litakusaidia kujua kama mwanafunzi ameelewa vizuri habari mnayozungumzia.

      3 Mwanafunzi anapojitayarisha kwa ajili ya funzo, ni muhimu achunguze kwa makini maandiko yaliyotajwa bila kunukuliwa. (Mdo. 17:11) Msaidie atambue kwamba kila andiko lililotajwa bila kunukuliwa linaunga mkono jambo fulani katika fungu. Mwonyeshe jinsi ya kuandika maelezo mafupi kuhusu maandiko pambizoni mwa kichapo cha funzo. Mweleze waziwazi kwamba Biblia ndiyo msingi wa yale anayojifunza. Mtie moyo atumie maandiko mengi iwezekanavyo anapotoa maelezo wakati wa funzo.

      4 Kupitia Habari kwa Ufupi na Kurudia Mambo Makuu: Kabla ya mwanafunzi kuanza kutayarisha habari mtakayojifunza, itafaa aipitie kwa ufupi. Mtajie kwamba anaweza kufanya hivyo kwa kuchunguza kichwa kikuu cha habari, vichwa vidogo, na picha. Mweleze kwamba kabla hajamaliza kutayarisha, ingefaa arudie mambo makuu katika funzo, labda kwa kutumia sanduku la pitio ikiwa lipo. Kufanya hivyo kutamsaidia kukumbuka habari anayojifunza.

      5 Kumzoeza mwanafunzi kutayarisha vizuri kwa ajili ya funzo lake kutamsaidia atoe maelezo yenye kujenga kwenye mikutano ya kutaniko. Pia kutamsaidia kusitawisha mazoea mazuri ya kujifunza hata baada ya kumaliza funzo lake la Biblia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki