Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 6—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma ya Ufalme—2005 | Februari
    • Sehemu ya 6—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

      Mwanafunzi Anapouliza Swali

      1 Baada ya kuanzisha funzo la Biblia na kuliongoza kwa muda, kwa kawaida ni vizuri kuzungumzia mafundisho ya Biblia kwa utaratibu, badala ya kuzungumzia mambo mengi tofauti-tofauti. Jambo hilo humsaidia mwanafunzi kuelewa mafundisho ya msingi kwa usahihi na kufanya maendeleo kiroho. (Kol. 1:9, 10) Hata hivyo, mara kwa mara wanafunzi huuliza maswali kuhusu mambo mbalimbali wakati wa funzo. Maswali hayo yashughulikiweje?

      2 Uwe Mwenye Utambuzi: Maswali yanayohusiana na habari mnayojifunza yanaweza kujibiwa mara moja. Kama swali litazungumziwa baadaye katika kichapo mnachojifunza, huenda ikatosha tu kumweleza mwanafunzi jambo hilo. Hata hivyo, ikiwa swali halihusiani na habari mnayojifunza au linahitaji kufanyiwa utafiti ili kujibiwa ifaavyo, huenda ikafaa kulizungumzia jambo hilo baada ya funzo au wakati mwingine. Baadhi ya wahubiri huona kwamba kuandika swali hilo humhakikishia mwanafunzi kwamba swali lake halipuuzwi na huwasaidia wahubiri wasikengeuke kutoka katika habari wanayojifunza.

      3 Mafundisho mengi ya Biblia huzungumziwa kifupi tu katika vichapo vyetu vya funzo. Namna gani ikiwa mwanafunzi ana tatizo la kukubali fundisho fulani au anashikilia sana imani fulani ya uwongo? Huenda ikafaa kutumia kichapo kingine kinachozungumzia kinaganaga yale ambayo Biblia inasema kuhusu jambo hilo. Ikiwa mwanafunzi hasadikishwi, basi liache jambo hilo hadi wakati mwingine na uendelee na funzo lenu la kawaida. (Yoh. 16:12) Anapoendelea kujifunza Biblia na kufanya maendeleo kiroho, huenda akaelewa fundisho hilo la Biblia.

      4 Usitoe Maoni Yako: Ikiwa huna hakika kuhusu jibu la swali fulani, usishawishike kutoa maoni yako. (2 Tim. 2:15; 1 Pet. 4:11) Mweleze mwanafunzi kwamba utafanya utafiti kuhusu swali hilo na kumjibu baadaye. Hata unaweza kutumia nafasi hiyo kumwonyesha mwanafunzi jinsi ya kufanya utafiti. Mwonyeshe hatua kwa hatua jinsi anavyoweza kufanya utafiti kwa kutumia vifaa mbalimbali vilivyoandaliwa na tengenezo la Yehova. Kwa njia hiyo, hatimaye yeye mwenyewe ataweza kupata majibu kwa maswali yake.—Mdo. 17:11.

  • Wasaidie Wapate Ushahidi Zaidi
    Huduma ya Ufalme—2005 | Februari
    • Wasaidie Wapate Ushahidi Zaidi

      1 Tunapohubiri habari njema, mara kwa mara sisi hukutana na watu ambao hawaishi katika eneo letu au wanaozungumza lugha ya kigeni, kutia ndani lugha ya ishara. Huenda wengine ambao tumekuwa tukizungumza nao kuhusu Biblia wakahamia eneo lingine. Tunawezaje kufanya mpango ili watu hao wapate ushahidi zaidi? Tunaweza kufanya hivyo kwa kutumia fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43-SW).

      2 Mara nyingi, watu husikiliza habari njema kwa makini zaidi wanapohubiriwa katika lugha yao wenyewe. (Mdo. 22:1, 2) Hivyo, kwa kawaida tunapokutana na mtu anayezungumza lugha ya kigeni, tunapaswa kujaza fomu hiyo hata kama mtu huyo hapendezwi na ujumbe wa Ufalme. Hata hivyo, katika maeneo ambako kuna watu wengi wanaozungumza lugha ya kigeni na ambao huhubiriwa kwa ukawaida katika lugha yao, huenda isiwe lazima kujaza fomu hiyo isipokuwa tu upate mtu anayependezwa.

      3 Kujaza Fomu Hiyo: Tumia busara unapomwuliza mtu huyo jina lake, anwani yake, na namba yake ya simu. Onyesha amependezwa kwa kadiri gani, wakati anapoweza kupatikana, kichapo alichoachiwa au alichoomba, na lugha anayoielewa vizuri. Baada ya kuijaza fomu hiyo, mpe mwandishi wa kutaniko bila kukawia, naye ataituma kwenye kutaniko au kikundi kinachoweza kumsaidia mtu huyo.

      4 Kutuma Fomu Hiyo: Ikiwa mwandishi hana anwani au hajui kutaniko au kikundi kinachopaswa kupelekewa fomu hiyo, anaweza kupiga simu kwenye ofisi ya tawi na kuzungumza na Idara ya Utumishi inayoshughulikia maeneo ili apate habari anazohitaji. Si lazima kumjulisha mwangalizi wa jiji fomu hiyo inapotumwa.

      5 Kutaniko au kikundi fulani kinapopokea fomu ya Tafadhali Fuatia Upendezi iliyojazwa, mipango inapaswa kufanywa bila kukawia ili kumtembelea mtu huyo. Tunapotimiza sehemu yetu kwa bidii, tunaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atafungua mioyo ya wale wenye “mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.”—Mdo. 13:48.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki