Wimbo 99
“Kusudi la Milele” la Mungu Linalofunuka
1. Zidi kusonga mbele,
Mahali pako tu.
Na mwendo wetu Yehova
Anatuwekea.
Naye amerudisha
Ibada ya kweli.
Umati mukubwa upo
Na unamwendea.
2. Bwana Mungu atupa
Tumaini hai.
Giza la akili, hofu,
Hatunayo tena.
Ndilo kusudi lake
Kuwe na amani.
Kwa utawala wa Kristo,
Vita vitakoma.
3. Kusudi lafunuka
Sisi tujikaze
Twende njia ya uzima
Na akili chonjo.
Kusudi la Yehova
Litafanikiwa.
Tubariki jina lake
Na kusonga mbele.