Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/08 uku. 1
  • Je, Familia Yako Inajitayarisha Kuokoka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Familia Yako Inajitayarisha Kuokoka?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Habari Zinazolingana
  • “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Igeni Imani Yao
  • Je! Wewe Walaani Vikali Ulimwengu Kupitia Imani Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • “Alitembea Pamoja na Mungu wa Kweli”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Noa Auhukumu Ulimwengu kwa Imani Yake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 6/08 uku. 1

Je, Familia Yako Inajitayarisha Kuokoka?

1 Unabii wa Biblia uliotimizwa unathibitisha kwa njia yenye kusadikisha kwamba mwisho wa ulimwengu huu mwovu unakaribia haraka. Sasa tunaishi katika nyakati ngumu zinazofanana sana na zile zilizotangulia Gharika. (Mt. 24:37-39) Noa aliokoka uharibifu wa ulimwengu huo wa zamani kwa sababu “alitembea pamoja na Mungu wa kweli.” (Mwa. 6:9) Ni wazi kwamba Noa aliifundisha familia yake njia za Yehova kwa sababu wao pia waliokolewa. Tunaweza kumwigaje Noa na kujitayarisha tukiwa familia kuokoka mwisho wa mfumo huu mwovu wa mambo?

2 Mhubiri wa Uadilifu: Noa alistahimili kwa miaka 40 hadi 50 akiwa “mhubiri wa uadilifu.” (2 Pet. 2:5) Inaonekana majirani wake walidhihaki kazi yake ya kuhubiri wakichochewa na malaika waasi waliovaa miili ya kibinadamu au wao wenyewe waliamua kufanya hivyo. Mara nyingi, huduma yetu haipendwi au inadhihakiwa, na hilo linathibitisha kwamba mwisho wa mfumo huu wa mambo uko karibu. (2 Pet. 3:3, 4) Hata hivyo, tofauti na watu wa siku za Noa, watu wengi leo wanaitikia jitihada zetu na ‘wanamiminika’ katika ibada ya Yehova. (Isa. 2:2) Tutajiokoa ‘sisi wenyewe na wale wanaotusikiliza pia’ ikiwa tu tutavumilia. (1 Tim. 4:16) Ni muhimu sana kwa wazazi kuwafundisha watoto wao uharaka wa kazi ya kuhubiri kwa maneno na mfano wao!—2 Tim. 4:2.

3 Alifanya “Vivyo Hivyo”: Noa na familia yake waliokolewa tu kwa sababu walifuata maagizo ya Yehova kwa uangalifu. (Mwa. 6:22) Ni muhimu kwetu leo pia kuwa “tayari kutii” mwongozo kutoka katika Biblia na kutoka kwa mtumwa mwaminifu. (Yak. 3:17) Watoto wa familia moja ambao sasa ni watu wazima wanakumbuka jinsi baba yao alivyofuata mapendekezo kutoka kwa tengenezo la Yehova. Kwa mfano, aliongoza funzo la familia kila juma na kwenda na familia yake katika huduma kila mwisho wa juma kama ilivyopendekezwa. Kila juma, alijitahidi kuhubiri na mtoto wake mmoja. Jitihada zake za kufanya “vivyo hivyo” ziliwachochea sana watoto wake, na mwishowe watoto wote sita wakawa watumishi washikamanifu wa Yehova.

4 Mwisho wa mfumo huu wa mambo utakuja ghafula. (Luka 12:40) Tukimwiga Noa na kuwa na imani ya kwamba tutaokolewa, bila shaka tutakuwa tayari kuokolewa pamoja na familia yetu!—Ebr. 11:7.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki