Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/08 uku. 2
  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba ya Mkutano wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 9
  • Juma Linaloanza Juni 16
  • Juma Linaloanza Juni 23
  • Juma Linaloanza Juni 30
  • Juma Linaloanza Julai 7
Huduma Yetu ya Ufalme—2008
km 6/08 uku. 2

Ratiba ya Mkutano wa Utumishi

TAARIFA: Mkutano wa Utumishi wa kila juma utapangwa katika Huduma Yetu ya Ufalme wakati wa miezi ya kusanyiko la wilaya. Makutaniko yanaweza kufanya mabadiliko yanayohitajiwa katika ratiba ili kuhudhuria Kusanyiko la Wilaya la “Kuongozwa na Roho ya Mungu.” Ikiwezekana, tumieni dakika 15 katika Mkutano wa Utumishi juma moja kabla ya kusanyiko ili kurudia mashauri na vikumbusho vinavyofaa hali zenu vilivyo katika nyongeza ya mwezi huu. Mwezi mmoja au miwili baada ya kusanyiko lenu, tumieni kati ya dakika 15 na 20 za Mkutano wa Utumishi (mnaweza kutumia sehemu ya mahitaji ya kwenu) kupitia mambo makuu ya kusanyiko ambayo yamewasaidia wahubiri katika huduma. Mwangalizi wa utumishi ashughulikie pitio hilo. Waombe wasikilizaji waeleze jinsi ambavyo wanatumia au wanapanga kutumia habari hizo katika huduma yao.

Juma Linaloanza Juni 9

Wimbo 121

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia mapendekezo yaliyo kwenye ukurasa wa 6 au mapendekezo mengine yanayofaa eneo lenu, panga kuwe na maonyesho ya jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 1 na Amkeni! la Mei.

Dak. 20: Jinsi ya Kujitayarisha Kuongoza Funzo la Biblia. Hotuba inayotegemea Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 2004, ukurasa wa 1. Mwishoni mwa mazungumzo, panga onyesho la mhubiri ambaye anajaribu kujitayarisha haraka-haraka kuongoza funzo la Biblia. Kisha, panga onyesho la mhubiri mwingine anayejitayarisha kwa kuchunguza baadhi ya mapendekezo yaliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme.

Dak. 15: “Hubiri Bila Kuacha.”a Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.

Wimbo 201

Juma Linaloanza Juni 16

Wimbo 90

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma Yetu ya Ufalme. Wakumbushe wasikilizaji waje na gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1 na Amkeni! la Juni kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma lijalo na wajitayarishe kuzungumzia njia zinazofaa wanazopanga kutumia kutoa magazeti hayo.

Dak. 15: Kazia Faida za Habari Njema. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Shule ya Huduma, ukurasa wa 159. Waombe wasikilizaji waeleze mambo ambayo yanawahangaisha watu sasa katika eneo lenu. Waombe wapendekeze njia za kushughulikia mahangaiko kama hayo tunapohubiri.

Dak. 20: “Je, Familia Yako Inajitayarisha Kuokoka?”b Kadiri wakati unavyoruhusu, waombe wasikilizaji watoe maelezo kuhusu maandiko ambayo hayakunukuliwa.

Wimbo 54

Juma Linaloanza Juni 23

Wimbo 140

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Soma ripoti ya hesabu na taarifa ya shukrani. Taja toleo la Julai, na upange kuwe na onyesho moja.

Dak. 20: Boresha Maisha Yako kwa Kufanya Upainia wa Kawaida. Hotuba inayotegemea Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 2008, ukurasa wa 17-19. Unaweza kuwahoji mapainia wawili wa kawaida ikiwa wapo, mmoja mpya na mwingine aliyetumikia kwa miaka mingi. Waombe waeleze jinsi ambavyo utumishi huu wenye thamani umeboresha maisha yao.

Dak. 15: Jitayarishe Kutoa Magazeti ya Karibuni. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Baada ya kuzungumzia kwa ufupi mambo makuu ya gazeti la Mnara wa Mlinzi la Juni 1 na Amkeni! la Juni, waombe wasikilizaji waeleze makala ambazo zinaweza kuwavutia watu katika eneo lenu na kwa nini wanaona zitawavutia. Waombe wataje mambo hususa ambayo wanapanga kuwaonyesha watu katika makala hizo. Ni swali gani linaloweza kuulizwa ili kuanzisha mazungumzo? Ni andiko gani katika makala linaloweza kusomwa? Ukitumia mapendekezo mbalimbali yaliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme au mengine yaliyotolewa na wasikilizaji, panga onyesho la jinsi ya kutoa kila moja ya magazeti hayo.

Wimbo 82

Juma Linaloanza Juni 30

Wimbo 97

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wahubiri wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Juni.

Dak. 20: Jinsi ya Kuboresha Stadi za Mazungumzo. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Shule ya Huduma, kutoka ukurasa wa 62, fungu la 4, mpaka fungu la mwisho la ukurasa wa 64. Zungumzieni habari hiyo mkizingatia eneo lenu. Mhoji kwa ufupi mhubiri ambaye ana ustadi wa kuanzisha mazungumzo pamoja na watu katika huduma ya nyumba kwa nyumba au anapohubiri kwa njia isiyo rasmi.

Dak. 15: Je, Unakumbuka? Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea gazeti la Mnara wa Mlinzi, la Aprili 15, 2008, ukurasa wa 29.

Wimbo 179

Juma Linaloanza Julai 7

Wimbo 125

Dak. 5: Matangazo ya kwenu.

Dak. 25: “Pindi ya Kulishwa Kiroho na Kushangilia.” Ishughulikiwe na mwandishi wa kutaniko. Taja kusanyiko la wilaya ambalo kutaniko lenu limegawiwa kuhudhuria. Pitia sanduku lenye kichwa “Vikumbusho vya Kusanyiko la Wilaya.”

Dak. 15: “Mwenye Nyumba Anapozungumza Lugha ya Kigeni.”c Ishughulikiwe na mwangalizi wa utumishi. Mnapozungumzia fungu la 2, julisha kutaniko vikundi au makutaniko mbalimbali ya lugha za kigeni ambayo yanahubiri katika eneo lenu. Eleza mipango yoyote hususa ambayo mmefanya ya kusaidia makutaniko au vikundi hivyo vishiriki katika kazi ya kuhubiri.

Wimbo 188

[Maelezo ya Chini]

a Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

b Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

c Toa utangulizi usiozidi dakika moja, kisha uendeleze mazungumzo kwa maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki