Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rs uku. 311-uku. 319
  • Ufalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufalme
  • Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mtu Akisema—
  • Kutabiri Wakati Wetu Ujao
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Ufalme “Ambao Hautaangamizwa Milele”
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Utawala wa Haki Wafanya Dunia kuwa Paradiso
    Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele
Pata Habari Zaidi
Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
rs uku. 311-uku. 319

Ufalme

Maana: Ufalme wa Mungu huwakilisha enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote kuelekea viumbe wake, au njia anayoitumia kuonyesha enzi hiyo. Neno hili linatumiwa hasa kurejelea enzi kuu ya Mungu kupitia serikali inayoongozwa na Mwana wake, Yesu Kristo. Neno “ufalme” linaweza kurejelea utawala wa yule aliyetiwa mafuta awe Mfalme, au linaweza kurejelea dunia inayotawaliwa na serikali hiyo ya mbinguni.

Je, Ufalme wa Mungu ni serikali halisi?

Au ni hali iliyo katika mioyo ya wanadamu?

Luka 17:21, UV: “Wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama ufalme wa Mungu umo ndani yenu [pia ZSB, NAJ; lakini “kati yenu,” BHN, VB; “katikati yenu,” NW].” (Ona kwamba, kama vile mstari wa 20 unavyoonyesha, Yesu alikuwa akizungumza na Mafarisayo, ambao pia aliwashutumu kuwa wanafiki, kwa hiyo, hangeweza kumaanisha kwamba Ufalme ulikuwa katika mioyo yao. Lakini Ufalme kama unavyowakilishwa na Kristo ulikuwa katikati yao.)

Je, kweli Biblia inasema kwamba Ufalme wa Mungu ni serikali?

Isa. 9:6, 7, UV: “Kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme [“mamlaka ya kutawala,” BHN; “utawala,” NW, ZSB] utakuwa begani mwake; naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani hayatakuwa na mwisho kamwe.”

Watawala wa Ufalme huo ni nani?

Ufu. 15:3: “Matendo yako ni makuu na ya ajabu, Yehova Mungu, Mweza-Yote. Njia zako ni za uadilifu na za kweli, Mfalme wa umilele.”

Dan. 7:13, 14: “Mtu fulani kama mwana wa binadamu [Yesu Kristo; ona Marko 14:61, 62] alikuwa anakuja na mawingu ya mbingu; naye akaja kwa Mzee wa Siku [Yehova Mungu], nao wakamleta karibu mbele zake Yule. Naye [Yesu Kristo] akapewa utawala na heshima na ufalme, ili vikundi vyote vya watu, vya mataifa na lugha vimtumikie yeye.”

Ufu. 5:9, 10; 14:1-3: “[Wewe Yesu Kristo] ulichinjwa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa, nawe ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu, nao watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia.” (Katika Ufunuo 14:1-3, hao ambao “wamenunuliwa kutoka duniani” wakatawale pamoja na Mwana-Kondoo juu ya Mlima Sayuni wa mbinguni wanatajwa kuwa watu 144,000.)

Ufalme huo utazitendeaje serikali za wanadamu?

Dan. 2:44: “Katika siku za wafalme hao, Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote. Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote, nao utasimama mpaka wakati usio na kipimo.”

Zab. 2:8, 9: “Niombe, ili nikupe mataifa yawe urithi wako na miisho ya dunia iwe miliki yako mwenyewe. Utawavunja kwa fimbo ya chuma ya enzi, utawavunja vipande-vipande, kama chombo cha mfinyanzi.”

Ufalme wa Mungu utatimiza nini?

Kutakasa jina la Yehova na kutegemeza enzi yake kuu

Mt. 6:9, 10: “Basi, ninyi msali hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, jina lako na litakaswe. Ufalme wako na uje.’” (Hapa kutakaswa kwa jina la Mungu kunahusianishwa na kuja kwa ufalme wake.)

Eze. 38:23: “Nami hakika nitajitukuza mwenyewe na kujitakasa mwenyewe na kujijulisha mwenyewe mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” (Jina la Mungu litaondolewa lawama zote; litaonwa kuwa takatifu na lenye kustahili heshima, na wote wanaoishi watakuwa watu wanaotegemeza enzi kuu ya Yehova kwa hiari, wanaopenda kufanya mapenzi yake. Amani na hali njema ya ulimwengu wote inategemea kutakaswa huko kwa jina la Yehova.)

Kuukomesha utawala wa Shetani ulimwenguni

Ufu. 20:2, 3: “Naye [Mfalme wa mbinguni, Yesu Kristo] akamkamata yule joka mkubwa, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, na kumfunga kwa miaka elfu. Naye akamtupa ndani ya abiso na kuifunga na kuitia muhuri juu yake, ili asipotoshe mataifa tena mpaka ile miaka elfu itakapokwisha. Baada ya mambo hayo yeye atafunguliwa kwa muda kidogo.” (Kwa hiyo, wanadamu watawekwa huru kutokana na uvutano wa Shetani ambao umefanya maisha yawe magumu sana kwa watu wanaotaka kufanya yaliyo sawa. Uvutano wa kishetani ambao umesababisha ukatili wenye kupita kiasi na uvutano wa roho waovu ambao umefanya watu wengi waishi kwa woga, utatoweka.)

Kuunganisha uumbaji wote umwabudu Mungu wa pekee wa kweli

Ufu. 5:13; 15:3, 4: “Na kila kiumbe kilicho mbinguni na juu ya dunia na chini ya dunia na juu ya bahari, na vitu vyote vilivyo ndani ya hivyo, nikasikia vikisema: ‘Kwake Yule anayeketi juu ya kile kiti cha ufalme [Yehova Mungu] na kwa Mwana-Kondoo [Yesu Kristo] kuwe na baraka na heshima na utukufu na nguvu milele na milele.’” “Matendo yako ni makuu na ya ajabu, Yehova Mungu, Mweza-Yote. Njia zako ni za uadilifu na za kweli, Mfalme wa umilele. Ni nani ambaye kwa kweli hatakuogopa wewe, Yehova, na kulitukuza jina lako, kwa sababu wewe peke yako ni mshikamanifu? Kwa maana mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa sababu amri zako za uadilifu zimefunuliwa.”

Kuwapatanisha tena wanadamu pamoja na Mungu

Rom. 8:19-21: “Uumbaji [wanadamu] unangojea na kutazamia kwa hamu kufunuliwa kwa wana wa Mungu [uthibitisho wa kwamba wale watakaofufuliwa ili waishi mbinguni pamoja na Yesu Kristo wameanza kutawala]. Kwa maana uumbaji ulitiishwa chini ya ubatili, si kwa mapenzi yake wenyewe bali kupitia yeye aliyeutiisha hivyo, juu ya msingi wa tumaini kwamba uumbaji wenyewe [wanadamu kwa ujumla] pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.”

Kuwaweka huru wanadamu kutokana na matisho yote ya vita

Zab. 46:8, 9: “Njooni, tazameni matendo ya Yehova, jinsi ambavyo ameweka matukio ya kushangaza duniani. Anakomesha vita mpaka kwenye mwisho wa dunia.”

Isa. 2:4: “Watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu. Taifa halitainua upanga juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.”

Kuwaondoa watawala wafisadi na wakandamizaji duniani

Zab. 110:5: “Yehova mwenyewe akiwa upande wako wa mkono wa kuume hakika atawavunja vipande-vipande wafalme katika siku ya hasira yake.”

Zab. 72:12-14: “[Masihi, Mfalme aliyewekwa na Yehova] atamkomboa maskini anayelilia msaada, pia mwenye kuteseka na yeyote ambaye hana msaidizi. Atamsikitikia mtu wa hali ya chini na maskini, naye ataziokoa nafsi za maskini. Ataikomboa nafsi yao kutoka katika ukandamizaji na katika jeuri, nayo damu yao itakuwa na thamani machoni pake.”

Kuwaandalia wanadamu wote chakula kingi

Zab. 72:16: “Kutakuwa na wingi wa nafaka duniani; juu ya milima kutakuwa na mafuriko.”

Isa. 25:6: “Yehova wa majeshi hakika atavifanyia vikundi vyote vya watu, katika mlima huu [katika Mlima Sayuni wa mbinguni, kiti cha Ufalme wa Mungu, raia wake wataandaliwa mahitaji], karamu ya vyakula vinono vilivyotiwa mafuta, karamu ya divai iliyowekwa kwenye machicha, ya vyakula vinono vilivyotiwa mafuta vilivyojazwa urojorojo, ya divai iliyowekwa kwenye machicha, iliyochujwa.”

Kuondoa magonjwa na ulemavu wa aina zote

Luka 7:22; 9:11: “Nendeni, mkamwambie Yohana yale mliyoona na kusikia: vipofu wanaona, vilema wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa na viziwi wanasikia, na wafu wanafufuliwa, maskini wanaambiwa ile habari njema.” “Naye [Yesu Kristo] akawapokea kwa fadhili na kuanza kuwaambia juu ya ufalme wa Mungu, naye akawaponya wale wanaohitaji kuponywa.” (Kwa njia hiyo, Yesu aliyaonyesha yale ambayo atawatendea wanadamu akiwa Mfalme mbinguni.)

Kuwaandalia watu wote nyumba nzuri

Isa. 65:21, 22: “Hakika wao watajenga nyumba na kukaa ndani yake; na hakika wao watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatajenga na mtu mwingine akae ndani yake; hawatapanda na mtu mwingine ale.”

Kuhakikisha wote wana kazi yenye kuridhisha

Isa. 65:23: “Hawatafanya kazi ya bure, wala hawatazaa kwa ajili ya kupata usumbufu; kwa sababu wao ni uzao wa watu wa Yehova waliobarikiwa, na wazao wao pamoja nao.”

Kuhakikisha kuna usalama kwa mtu na mali zake

Mika 4:4: “Nao wataketi, kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake, wala hakutakuwa na mtu yeyote anayewatetemesha; kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema hivyo.”

Zab. 37:10, 11: “Bado muda kidogo tu, na mtu mwovu hatakuwako tena; nawe hakika utapaangalia mahali pake, naye hatakuwapo. Bali wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”

Kueneza uadilifu na haki

2 Pet. 3:13: “Kulingana na ahadi yake tunangojea mbingu mpya na dunia mpya, na humo uadilifu utakaa.”

Isa. 11:3-5: “Na [Masihi Mfalme] hatahukumu kulingana na sura inayoonekana kwa macho yake tu, wala kukaripia kulingana tu na jambo lililosikiwa na masikio yake. Naye atawahukumu kwa uadilifu watu wa hali ya chini, atakaripia kwa unyoofu kwa ajili ya watu wapole wa dunia. . . . Na uadilifu utakuwa mshipi wa viuno vyake, na uaminifu mshipi wa viuno vyake.”

Kuwalinda wanadamu wasipatwe na madhara yoyote kwa sababu ya nguvu za asili

Marko 4:37-41: “Sasa kukatokea dhoruba kubwa ya upepo wenye nguvu nyingi, na mawimbi yakawa yakiipiga mashua kwa nguvu, hivi kwamba karibu mashua ifunikwe na maji. . . . Ndipo [Yesu] akaamka, akaukemea upepo na kuiambia bahari: ‘Nyamaza, utulie!’ Na upepo ukapunguka, kukawa utulivu mkubwa. . . . Lakini wakaogopa isivyo kawaida, nao wakawa wakiambiana: ‘Kwa kweli huyu ni nani, kwa sababu hata upepo na bahari zinamtii?’” (Kwa hiyo, Kristo alionyesha uwezo alio nao akiwa Mfalme wa mbinguni atakaotumia kudhibiti nguvu hizo za asili.)

Kufufua wafu

Yoh. 5:28, 29: “Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake [sauti ya Kristo Mfalme] na kutoka.”

Ufu. 20:12: “Nami nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya kile kiti cha ufalme, na vitabu vya kukunjwa vikafunguliwa. Lakini kitabu kingine cha kukunjwa kikafunguliwa; hicho ni kitabu cha uzima. Na wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika vile vitabu kulingana na matendo yao [yale watakayofanya baada ya kufufuliwa kwao; linganisha na Waroma 6:7].”

Kuondoa kifo kinachotokana na dhambi ya Adamu tuliyorithi

Isa. 25:8: “Kwa kweli atameza kifo milele, na Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova hakika atafuta machozi katika nyuso zote.”

Ufu. 21:4: “Naye atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.”

Kutokeza ulimwengu ambamo watu watapendana kikweli

Yoh. 13:35: “Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu [wenye tazamio la kutawala pamoja na Yesu katika Ufalme wa mbinguni au kuwa raia wa Ufalme huo hapa duniani], mkiwa na upendo kati yenu wenyewe.”

Kuwafanya wanyama na wanadamu wawe na uhusiano mzuri

Isa. 11:6-9: “Mbwa-mwitu kwa kweli atakaa pamoja na mwana-kondoo kwa muda fulani, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi, na ndama na mwana-simba mwenye manyoya shingoni na mnyama aliyelishwa vizuri wote pamoja; na mvulana mdogo atakuwa kiongozi juu yao. Na ng’ombe na dubu watakula pamoja; watoto wao watalala pamoja. Na hata simba atakula majani kama ng’ombe. Na mtoto anayenyonya hakika atacheza juu ya shimo la nyoka; na mtoto aliyeachishwa kunyonya atatia mkono wake juu ya tundu la kupitishia nuru la nyoka mwenye sumu. Hawatasababisha madhara yoyote wala kusababisha uharibifu wowote katika mlima wangu wote mtakatifu.” (Ona pia Isaya 65:25)

Hos. 2:18: “Kwa ajili yao hakika nitafanya agano siku hiyo na mnyama wa mwituni na kiumbe kinachoruka cha mbinguni na kitu kinachotambaa cha nchi, . . . nami nitawafanya walale salama salimini.”

Kuifanya dunia kuwa Paradiso

Luka 23:43: “Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.”

Zab. 98:7-9: “Bahari na ingurume na vyote vinavyoijaza, nchi yenye kuzaa na wanaokaa humo. Mito na ipige makofi; milima yote pamoja na ipige vigelegele kwa shangwe mbele za Yehova, kwa maana amekuja kuihukumu dunia. Ataihukumu nchi yenye kuzaa kwa uadilifu na vikundi vya watu kwa unyoofu.”

Linganisha na Mwanzo 1:28; 2:15; Isaya 55:11.

Ufalme wa Mungu ulipaswa kuanza kutawala wakati gani?

Je, ulipaswa kuanza kutawala katika karne ya kwanza?

Kol. 1:1, 2, 13: “Paulo, mtume wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu kwa watakatifu [wale waliokuwa warithi wa Ufalme wa mbinguni] . . . Yeye [Mungu] alitukomboa kutoka katika mamlaka ya giza, akatuhamisha [watakatifu, washiriki wa kutaniko la Kikristo] na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa upendo wake.” (Kwa kweli, Kristo alikuwa ameanza kutawala kutaniko la Kikristo katika karne ya kwanza, kabla ya mambo hayo kuandikwa, lakini Ufalme ungeanza kutawala dunia yote wakati ujao.)

1 Kor. 4:8: “Ninyi tayari mmepata shibe yenu, sivyo? Ninyi tayari ni matajiri, sivyo? Mmeanza kutawala mkiwa wafalme bila sisi, sivyo? Nami ningalipenda kwamba muwe mmeanza kutawala mkiwa wafalme, ili sisi pia tutawale pamoja nanyi tukiwa wafalme.” (Ni wazi kwamba mtume Paulo anawakaripia kwa sababu ya kuwa na maoni yenye makosa.)

Ufu. 12:10, 12: “Sasa kumekuwa na wokovu na nguvu na ufalme wa Mungu wetu na mamlaka ya Kristo wake, kwa sababu mshtaki wa ndugu zetu ametupwa chini, anayewashtaki mchana na usiku mbele za Mungu wetu! Kwa sababu hiyo furahini, enyi mbingu nanyi mnaokaa ndani yake! Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na hasira kali, akijua kwamba ana kipindi kifupi cha wakati.” (Kusimamishwa kwa Ufalme wa Mungu hapa kunahusianishwa na kutupwa kwa Shetani kutoka mbinguni. Hilo halikutukia wakati wa uasi katika Edeni, kama inavyoonyeshwa katika Ayubu sura ya 1 na ya 2. Kitabu cha Ufunuo kiliandikwa mwaka wa 96 W.K., nalo andiko la Ufunuo 1:1 huonyesha kwamba kitabu hicho kinashughulikia matukio ambayo yangetimia wakati ujao.)

Je, ni lazima watu ulimwenguni pote wageuzwe imani kabla ya Ufalme wa Mungu kuanza kutawala?

Zab. 110:1, 2: “Neno la Yehova kwa Bwana wangu [Yesu Kristo] ni: ‘Keti kwenye mkono wangu wa kuume mpaka niwaweke adui zako kuwa kiti cha miguu yako.’ Yehova ataituma fimbo ya nguvu zako kutoka Sayuni, akisema: ‘Nenda ukitiisha katikati ya adui zako.’” (Kwa hiyo, kungekuwa na adui ambao angewatiisha; si wote ambao wangeukubali utawala wake.)

Mt. 25:31-46: “Mwana wa binadamu [Yesu Kristo] atakapofika katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu. Na mataifa yote yatakusanyika mbele yake, naye atawatenganisha watu, mmoja kutoka kwa mwenzake, kama vile mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi. . . . Na hawa [ambao hawakuwapenda ndugu zake watiwa-mafuta] watakatiliwa mbali milele, lakini waadilifu wataingia katika uzima wa milele.” (Si wanadamu wote wangegeuzwa imani kabla ya Kristo kuanza kutawala; si wote wangekuwa waadilifu.)

Je, Biblia inaonyesha wakati ambapo Ufalme ungeanza kutawala?

Ona ukurasa wa 397-399, chini ya kichwa “Vipindi vya Wakati,” na ukurasa wa 284-289, chini ya kichwa “Siku za Mwisho.”

Mtu Akisema—

‘Ufalme hautakuja nikiwa hai’

Unaweza kujibu hivi: ‘Lakini utakapokuja, watu fulani watakuwa hai, sivyo? . . . Je, mtu yeyote anaweza kujua ikiwa kizazi chake ndicho kilichopaswa kuuona? Mitume wa Yesu walitaka kujua, na jibu alilowapa ni muhimu sana kwetu leo. (Mt. 24:3-14)’

Au unaweza kusema: ‘Watu wengi wanaamini hivyo. Lakini Mashahidi wa Yehova wanaamini kabisa, wakitegemea Biblia, kwamba Ufalme wa Mungu tayari unatawala mbinguni na kwamba ni juu yetu sisi kuonyesha kama tunataka kuendelea kuishi duniani chini ya serikali hiyo ya Mungu yenye uadilifu au hatutaki. Ndiyo sababu nimekutembelea leo. Ona mambo yanayosemwa hapa katika Mathayo 24:14.’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki