Wimbo Na. 75
Sababu za Kuwa na Shangwe
1. Tuna sababu nyingi sana,
Kuwa na shangwe halisi.
Vitu vyenye kutamanika,
Vinajiunga na sisi.
Tunashangilia moyoni,
Neno linaeleweka.
Tunajifunza kila siku;
Imani yaongezeka.
Nayo shangwe yetu yazidi,
Kama moto uwakao.
Ingawa tuna matatizo,
Kwetu Yehova ni ngao.
(KORASI)
Yehova ni shangwe yetu,
Kazi zake za ajabu.
Mawazo yake yapita yetu,
Mungu mwema na mukuu!
2. Tunaziona kazi zake,
Mbingu, bahari, na dunia.
Anastahili kusifiwa,
Kwa kazi za uumbaji.
Sasa twatangaza ushindi,
Wa Ufalme wa Yehova.
Ujumbe wa baraka zake,
Kotekote twatangaza.
Siku mupya yakaribia,
Sikuzote kuwe shangwe.
Dunia nazo mbingu mupya,
Milele tushangilie.
(KORASI)
Yehova ni shangwe yetu,
Kazi zake za ajabu.
Mawazo yake yapita yetu,
Mungu mwema na mukuu!
(Ona pia Kum. 16:15; Isa. 12:6; Yoh. 15:11.)