Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • jr sura 3 kur. 32-42
  • “Uwaambie Neno Hili”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Uwaambie Neno Hili”
  • Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • ‘YEHOVA ALINIGUSA KINYWA’
  • “UMENIPUMBAZA, EE YEHOVA”
  • “LABDA WATASIKILIZA NA KURUDI, KILA MMOJA”
  • “Siwezi Kunyamaza Kimya”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • “Nimeyatia Maneno Yangu Katika Kinywa Chako”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • Je, Kila Siku Unauliza, “Yehova Yuko Wapi?”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • Utachagua Marafiki wa Aina Gani?
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
Pata Habari Zaidi
Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
jr sura 3 kur. 32-42

SURA YA TATU

“Uwaambie Neno Hili”

1. (a) Kuna ulinganifu gani kati ya Yesu na Yeremia? (b) Kwa nini tunapaswa kumwiga Yeremia katika huduma yetu?

YESU KRISTO ndiye mfano bora tunaoiga katika kazi yetu ya kuhubiri habari njema. Katika karne ya kwanza watu fulani walidhani kwamba Yesu ni nabii Yeremia. (Mt. 16:13, 14) Sawa na Yesu, Yeremia aliagizwa na Mungu ahubiri. Kwa mfano, pindi moja Mungu alimwambia: “Uwaambie neno hili, ‘Yehova Mungu . . . amesema hivi.’” (Yer. 13:12, 13; Yoh. 12:49) Na katika huduma yake, Yeremia alionyesha sifa kama za Yesu.

2. Kuna ulinganifu gani kati ya hali za watu leo na katika siku za Yeremia?

2 Huenda Mashahidi fulani wakasema: ‘Leo, hali ni tofauti na siku za Yeremia. Wengi tunaowahubiria hawamjui Yehova lakini Yeremia alimwakilisha Mungu katika taifa lililokuwa wakfu.’ Ni kweli. Hata hivyo, katika siku za Yeremia, Wayahudi wengi walikuwa wameacha kutenda kwa “hekima” nao walikuwa wamemwacha Mungu wa kweli. (Soma Yeremia 5:20-22.) Ili wamwabudu Yehova kwa njia inayokubalika, walihitaji kufanya mabadiliko. pia, iwe mtu ni Mkristo au hapana, anapaswa kujifunza kumwogopa Yehova na kujiunga na ibada ya kweli. Mfano wa Yeremia unaweza kutusaidia jinsi gani katika utumishi wetu kwa Mungu wa kweli na katika kazi yetu ya kuhubiri? Acheni tuone.

Picha katika ukurasa wa 33

‘YEHOVA ALINIGUSA KINYWA’

3. Yehova alifanya jambo gani lisilo la kawaida mwanzoni mwa utume wa Yeremia, naye Yeremia alihisi namna gani?

3 Kumbuka kwamba mwanzoni wa huduma yake, Yeremia aliambiwa: “Kwa wale wote nitakaokutuma kwao, unapaswa kwenda; na kila jambo nitakalokuamuru, unapaswa kusema. Usiogope kwa sababu ya nyuso zao, kwa maana ‘mimi niko pamoja nawe ili kukukomboa,’ asema Yehova.” (Yer. 1:7, 8) Kisha Mungu akafanya jambo lisilo la kawaida. Yeremia asema: “Yehova akanyoosha mkono wake na kunigusa kinywa changu. Ndipo Yehova akaniambia: ‘Nimeyatia maneno yangu katika kinywa chako. Tazama, nimekupa utume leo.’” (Yer. 1:9, 10) Tangu wakati huo na kuendelea, Yeremia alijua kwamba anazungumza kwa niaba ya Mungu Mweza-Yote.a Kwa msaada wa Mungu, bidii ya Yeremia kwa ajili ya utumishi mtakatifu iliongezeka.—Isa. 6:5-8.

Picha katika ukurasa wa 34
Picha katika ukurasa wa 34
Picha katika ukurasa wa 34

4. Simulia mifano ya watu wenye bidii ya pekee katika kazi ya kuhubiri.

4 Leo, Yehova hawagusi kihalisi watumishi wake. Hata hivyo, kupitia roho yake, anawachochea kuwa na tamaa ya kuhubiri habari njema. Wengi wao wana bidii sana. Kwa mfano, fikiria kisa cha Maruja nchini Hispania. Amepooza mikono na miguu kwa zaidi ya miaka 40. Hawezi kuhubiri nyumba kwa nyumba, na kwa hiyo, yeye hutafuta njia nyingine za kuhubiri. Njia moja ni kuandika barua. Maruja humtumia binti yake kuandika. Wakati wa kampeni ya mwezi mmoja, Maruja na binti yake walituma barua zaidi ya 150, kila moja ikiambatana na trakti. Kwa kufanya hivyo, habari njema iliwafikia wengi wa watu katika kijiji jirani. Maruja alimwambia binti yake: “Yoyote kati barua zetu ikimfikia mtu mnyoofu, Yehova atatubariki kwa funzo la Biblia.” Mzee mmoja katika kutaniko lao aandika: “Namshukuru Yehova kwa kutupa akina dada kama Maruja, ambao huwafundisha wengine wathamini mambo yaliyo ya maana.”

5. (a) Ni nini kilichomsaidia Yeremia kuendelea kuwa na bidii katika mgawo wake? (b) Unaweza kudumisha jinsi gani bidii ya kuhubiri habari njema?

5 Katika siku za Yeremia, wakaaji wengi wa Yerusalemu ‘hawakupendezwa’ na kweli ya Mungu. Je, aliacha kuhubiri? Hapana! Yeremia alisema: “Nimejawa na ghadhabu ya Yehova. Nimechoka kujizuia.” (Yer. 6:10, 11) Ni nini kinachoweza kukusaidia kuendelea kuwa na bidii kama hiyo? Siri moja ni kutafakari pendeleo la pekee la kumwakilisha Mungu wa kweli. Unajua kwamba watu mashuhuri katika ulimwengu huu wameliletea suto jina la Mungu wa kweli. Pia, fikiria jinsi viongozi wa kidini wamewadanganya watu katika eneo lenu, kama vile makuhani walivyofanya katika siku za Yeremia. (Soma Yeremia 2:8, 26, 27.) Kwa upande mwingine, habari njema ya Ufalme wa Mungu unayohubiri inaonyesha kwamba Mungu anawapenda wanadamu. (Omb. 3:31, 32) Kutafakari hayo kutakusaidia kuendelea kuwa na bidii katika kutangaza habari njema na kuwasaidia walio mfano wa kondoo.

6. Yeremia alikabili hali gani ngumu?

6 Bila shaka si rahisi kuendelea kuwa na bidii katika huduma ya Kikristo sikuzote. Alipokuwa akimtumikia Yehova, Yeremia pia alikabili hali ngumu, kutia ndani manabii wa uwongo. Kisa kimoja kinasimuliwa katika Yeremia sura ya 28. Wengi hawakusikiliza ujumbe wake, na nyakati nyingine alihisi kana kwamba ametengwa. (Yer. 6:16, 17; 15:17) Isitoshe, nyakati nyingine uhai wake ulikuwa hatarini.—Yer. 26:11.

Kwa nini tunaweza kumtegemea Yehova atusaidie kushinda hali ngumu tunapohubiri habari njema?

“UMENIPUMBAZA, EE YEHOVA”

7, 8. Mungu ‘alimpumbaza’ Yeremia kwa njia gani?

7 Wakati mmoja Yeremia alipokuwa akidhihakiwa na kutukanwa siku baada ya siku, alimweleza Mungu hisia zake. Unafikiri ni kwa njia gani Yehova ‘alimpumbaza’ nabii wake mwaminifu, kama inavyotajwa katika Yeremia 20:7, 8?—Soma.

8 Yehova hakumdanganya wala kumhadaa Yeremia kwa hila au ujanja fulani. Badala yake, Mungu “alimpumbaza” kwa njia nzuri, ambayo ingemnufaisha. Yeremia aliuona upinzani kuwa mkubwa sana hivi kwamba akiwa peke yake asingeweza kuutimiza mgawo aliopewa na Mungu. Hata hivyo, kwa msaada wa Mweza-Yote, aliutimiza. Kwa hiyo basi, ni kana kwamba Yehova alimshinda Yeremia akionyesha kwamba ana nguvu nyingi zaidi. Yeremia alipofikiri kwamba amefika mwisho kabisa naye hawezi kuendelea, ni kana kwamba Yehova ‘alimpumbaza’ kwa kutumia nguvu zenye kusadikisha. Nguvu za Mungu zilikuwa nyingi kuliko udhaifu wa nabii Yeremia. Aliendelea kuhubiri licha ya upinzani, kutopendezwa kwa watu, na jeuri.

9. Kwa nini maneno ya Yeremia 20:11 ni yenye kutia moyo?

9 Yehova alikuwa pamoja na Yeremia “kama mwenye nguvu anayetisha,” akimtegemeza. (Yer. 20:11) Mungu anaweza kukuimarisha wewe pia ili uendelee kuwa na bidii katika ibada ya kweli na kusonga mbele hata ikiwa kuna matatizo makubwa. Unaweza kumwona Yehova kama anavyoitwa katika tafsiri nyingine, “shujaa aliye hodari.”—Verbum Bible.

10. Ukipata upinzani, utafanya nini?

10 Mtume Paulo alikazia jambo hilo alipokuwa akiwatia moyo Wakristo waliopata upinzani. Aliandika: “Jiendesheni kwa namna inayostahili habari njema juu ya Kristo, ili . . . nisikie . . . kwamba mnasimama imara katika roho moja, kwa nafsi moja mkikazana pamoja kwa ajili ya imani ya habari njema, nanyi msiwaogope hata kidogo wapinzani wenu.” (Flp. 1:27, 28) Kama Yeremia na Wakristo wa karne ya kwanza, unaweza na unapaswa kumtegemea Mungu Mweza-Yote katika huduma yako. Ukidhihakiwa au kushambuliwa, kumbuka kwamba Yehova yuko pamoja nawe, naye atakupa nguvu. Alimsaidia Yeremia. Amewasaidia wengi kati ya ndugu zako. Kwa hiyo, anaweza kukusaidia wewe pia. Mwombe msaada, na uwe na hakika kwamba atajibu sala zako. Mungu anapokupa nguvu za kushinda vipingamizi kwa mafanikio, nawe utende kwa ujasiri badala ya kujikunyata kwa woga, huenda wewe pia ukahisi kana kwamba Mungu ‘amekupumbaza.’ Ndiyo, huenda ukafanya mengi zaidi kuliko ulivyofikiri ungeweza.—Soma Matendo 4:29-31.

11, 12. (a) Unaweza kufanya nini ili kuwahubiria watu wengi zaidi? (b) Kama picha kwenye ukurasa wa 39 inavyoonyesha, ni wapi pengine unapoweza kuhubiri?

11 Yale tunayosoma kuhusu utumishi wa Yeremia yanaweza kutusaidia kwa njia mbalimbali kuwa wahudumu wenye matokeo zaidi wa habari njema. Baada ya kumtumikia Yehova akiwa nabii kwa zaidi ya miaka 20, alisema: “Nikaendelea kusema nanyi, nikiamka mapema na kusema, lakini hamkusikiliza.” (Yer. 25:3) Ndiyo, alikuwa akianza asubuhi na mapema. Je, kuna lolote tunaloweza kujifunza kutokana na mfano wake? Katika makutaniko mengi, kuna wahubiri ambao huamka mapema ili kuwahubiria watu kwenye vituo vya mabasi na magari-moshi. Katika maeneo ya vijijini, Mashahidi wengi hutumia saa za asubuhi na mapema kuwatembelea wakulima na wengine ambao huwa kazini wakati huo. Je, kuna njia nyinginezo ambazo wewe binafsi unaweza kufuata mfano huo wa Yeremia? Je, unaweza kuamka mapema vya kutosha ili uwepo mkutano wa utumishi wa shambani unapoanza?

12 Ni kweli kwamba kuhubiri nyumba kwa nyumba saa za alasiri na jioni mara nyingi huwa na matokeo katika sehemu nyingi. Wahubiri fulani hata huhubiri usiku, wakiwatembelea watu katika vituo vya petroli, mikahawa, na sehemu nyingine za biashara zinazofanya kazi saa 24. Je, unaweza kubadili ratiba yako ili uhubiri wakati na mahali ambapo unaweza kuwapata watu?

Unajua jinsi gani kwamba Yehova yuko pamoja nawe unapotangaza ujumbe wake?

13, 14. (a) Kuhusu ziara za kurudia, mfano wa Yeremia unatusaidia jinsi gani? (b) Kwa nini tunapaswa kuwa wenye kutegemeka tunapoahidi kufanya ziara za kurudia?

13 Pindi kadhaa, Yehova alimwamuru Yeremia atangaze ujumbe wa kinabii akiwa amesimama katika malango ya hekalu au ya Yerusalemu. (Yer. 7:2; 17:19, 20) Kwa kufanya hivyo, Yeremia aliweza kuwafikia watu wengi na neno la Yehova. Kwa kuwa watu wengi, kutia ndani watu mashuhuri wa jiji na wafanyabiashara walipita hapo mara nyingi, huenda alizungumza na baadhi yao tena na tena akijaribu kuwasaidia kuelewa mambo waliyokuwa wamesikia. Tunaweza kufuata jinsi gani mfano huo tunapowarudia watu wanaopendezwa?

14 Yeremia alijua kwamba ujumbe aliokuwa nao ungeweza kuokoa uhai. Pindi moja, wakati ambapo hangeweza kuwaambia watu maagizo ya Mungu, alimtuma rafiki yake, Baruku, amwakilishe. (Soma Yeremia 36:5-8.) Tunaweza kufuata jinsi gani mfano wa Yeremia? Tukimwahidi mwenye nyumba kwamba tutarudi, je, sisi hufanya hivyo? Ikiwa hatuwezi, je, tunapanga mtu mwingine amrudie? Yesu alisema: “Neno lenu Ndiyo limaanishe Ndiyo.” (Mt. 5:37) Ni muhimu kutimiza ahadi, kwa kuwa tunamwakilisha Mungu wa kweli mwenye utaratibu.—1 Kor. 14:33, 40.

Picha katika ukurasa wa 39

Umebadili ratiba yako na njia zako za kuhubiri ili uweze kuwafikia watu wengi zaidi?

15, 16. (a) Wengi wamefuata mfano wa Yeremia jinsi gani katika huduma yao? (b) Tunaweza kujifunza nini kutokana na jambo lililoonwa nchini Chile, kama picha katika ukurasa wa 40 inavyoonyesha?

15 Yeremia aliwatia moyo Wayahudi walioishi Babiloni kwa kuwaandikia barua yenye ‘neno jema’ la Yehova kuhusu kurudishwa. (Yer. 29:1-4, 10) Leo, ‘neno jema’ kuhusu yale ambayo Yehova atafanya hivi karibuni linaweza kuenezwa kwa barua au simu. Je, unaweza kutumia njia hizo kuwasaidia watu wa ukoo au wengine wanaoishi mbali au wale ambao hawawezi kufikiwa kwa urahisi?

16 Kwa kufuata mfano wa Yeremia wa kutimiza huduma yake kikamili, wahubiri wa Ufalme leo hupata matokeo mazuri. Shahidi mmoja huko Chile alianzisha mazungumzo na mwanamke aliyekuwa akitoka katika kituo cha gari-moshi. Mwanamke huyo alipendezwa sana na ujumbe wa Biblia naye akakubali kujifunza Biblia nyumbani kwake. Hata hivyo, Shahidi huyo, hakuandika mahali ambapo mwanamke huyo anaishi. Baadaye, akiwa na nia ya kuendeleza hamu ya mwanamke huyo ya kujifunza kweli, dada yetu alimwomba Yehova msaada katika sala. Siku iliyofuata, alirudi kwenye kituo kilekile. Alikutana na mwanamke yule tena. Wakati huo, aliandika mahali anapoishi na baadaye akamtembelea nyumbani kwake ili kumsaidia kuelewa Maandiko. Karibuni Mungu atatekeleza hukumu dhidi ya ulimwengu wa Shetani. Lakini wale wanaotubu na kuwa na imani katika habari njema wana tumaini. (Soma Maombolezo 3:31-33.) Basi, na tuonyeshe kwamba tunatambua hilo kwa kulihubiri eneo letu kwa bidii.

Picha katika ukurasa wa 40

Je, wewe hufanya yote uwezayo ili kuwarudia watu wanaopendezwa?

“LABDA WATASIKILIZA NA KURUDI, KILA MMOJA”

17. Ni mfano gani wa Yeremia unaoweza kufuata katika eneo lenu?

17 Yehova hakutaka watu wafe. Miaka kumi hivi kabla ya uharibifu wa Yerusalemu, Yehova alimtumia Yeremia kutangaza ujumbe wenye tumaini kwa wale waliokuwa uhamishoni Babiloni. Tunasoma: “Nitaweka jicho langu juu yao kwa njia nzuri, na hakika mimi nitawarudisha katika nchi hii. Nami nitawajenga, wala sitawabomoa; nami nitawapanda, wala sitawang’oa.” Yeremia aliwaambia watu hao: “Kuna tumaini kwa ajili ya wakati wako ujao.” (Yer. 24:6; 26:3; 31:17) Yeremia aliwaona watu hao kama vile Mungu alivyowaona. Aliwajali kikweli katika huduma yake, na kuwapa ujumbe huu wenye kuwahimiza kutoka kwa Yehova: “Tafadhali rudini, kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya, nanyi fanyeni matendo yenu kuwa mema.” (Yer. 35:15) Je, kuna njia nyingine ambazo unaweza kuonyesha kwamba kwa kweli unapendezwa kibinafsi na watu katika eneo lenu?

18, 19. (a) Tunapaswa kuepuka maoni gani tunapohubiri habari njema? (b) Kama Yeremia, tunapaswa kuwa na maoni gani?

18 Yeremia hakuacha kamwe kuwapenda watu kikweli. Hata Yerusalemu lilipokuwa likiharibiwa, bado aliendelea kuwahurumia. (Soma Maombolezo 2:11.) Wayahudi hawangeweza kumlaumu yeyote kwa msiba uliowapata. Hata hivyo, Yeremia hakuwaambia, ‘Shauri yenu.’ Badala yake, alihuzunishwa sana na yaliyowapata. Vivyo hivyo, huduma yetu haipaswi kamwe kuwa ya kidesturi, kwa kuwa tu tuna wajibu. Jitihada zetu za kutoa ushahidi zinapaswa kuthibitisha kwamba tunampenda sana Mungu wetu na pia wanadamu ambao wameumbwa kwa mfano wake.

Picha katika ukurasa wa 42

Je, wewe huwaonyesha watu kwamba unapendezwa nao kibinafsi?

19 Hakuna pendeleo au cheo katika ulimwengu huu kinachoweza kupita pendeleo la kumwakilisha Mungu wa kweli. Yeremia alihisi hivyo alipoandika: “Maneno yako yalipatikana, nami nikayala; na neno lako linakuwa kwangu furaha na kushangilia kwa moyo wangu; kwa maana jina lako limeitwa juu yangu, Ee Yehova.” (Yer. 15:16) Tunapoendelea kuhubiri habari njema, wengi watapata kumjua na kumpenda Yule ambaye amewapa uhai. Tukitumikia kwa bidii na upendo, tunaweza kuwasaidia wengi, kama Yeremia alivyofanya.

Kwa kufuata mfano wa Yeremia, ni njia gani nyingine za kutangaza ‘neno jema’ la Yehova unazoweza kutumia wakati ujao?

a Katika kisa hiki, kama ilivyo katika visa vingine vingi, Yehova aliwakilishwa na malaika aliyezungumza kana kwamba ni Yehova mwenyewe.—Amu. 13:15, 22; Gal. 3:19.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki