Wimbo Na. 42
“Mwasaidie Wale Walio Dhaifu”
Makala Iliyochapishwa
1. Kila mumoja wetu
Dhambi hutenda.
Hata hivyo,
Yehova Anatupenda.
Ni mwenye rehema,
Upendo fadhili.
Tusaidie wote,
Wastahimili.
2. Paulo kakazia,
Sote dhaifu.
Mungu katoa
Mwana Mukamilifu.
Walio dhaifu
Ni wa Mungu pia.
Twawahangaikia,
Wapate njia.
3. Tusiwe wachambuzi,
Wafarijike.
Tuonyeshe fadhili,
Waimarike.
Tuwe na bidii,
Tuwatie moyo;
Na kuwategemeza,
’Siwe wachoyo.
(Ona pia Isa. 35:3, 4; 2 Kor. 11:29; Gal. 6:2.)