Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mapenzi ya Mungu Ni Nini?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
    • Mapenzi ya Mungu Ni Nini?

      Mungu anataka tuishi milele kwa amani na furaha katika paradiso duniani!

      Huenda ukajiuliza, ‘Inawezekanaje?’ Biblia inasema kwamba Ufalme wa Mungu utafanya jambo hilo liwezekane, na ni mapenzi ya Mungu kwamba watu wote wajifunze kuhusu Ufalme huo na kusudi lake.—Zaburi 37:11, 29; Isaya 9:7.

      Mungu anataka tunufaike.

      Kama vile baba mzuri anavyowatakia watoto wake mema, Baba yetu wa mbinguni anataka tuishi milele kwa furaha. (Isaya 48:17, 18) Ameahidi kwamba yule “anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”—1 Yohana 2:17.

      Mungu anataka tutembee katika njia zake.

      Biblia inasema kwamba Muumba wetu anataka ‘kutufundisha njia zake’ ili ‘tutembee katika vijia vyake.’ (Isaya 2:2, 3) Amewapanga “watu kwa ajili ya jina lake” ili watangaze mapenzi yake duniani kote.—Matendo 15:14.

      Mungu anataka tumwabudu kwa umoja.

      Badala ya kuwagawanya watu, ibada safi ya Yehova huwaunganisha pamoja katika upendo wa kweli. (Yohana 13:35) Ni nani leo ambao wanawafundisha wanaume na wanawake kila mahali jinsi ya kumtumikia Mungu kwa umoja? Tunakutia moyo usome broshua hii ili upate jibu.

      PATA KUJUA MENGI ZAIDI

      Jifunze Biblia pamoja nasi. Je, umeanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova? Ikiwa bado, je, ungependa kujifunza Biblia? Utafundishwa bila malipo. Utaona kwamba hiyo ni njia bora ya kumkaribia Mungu.

      Omba machapisho bila malipo. Unaweza kwenda kwenye Jumba la Ufalme lililo karibu nawe au uzungumze na Shahidi wa Yehova ili kupata chapisho la lugha yako ambalo litakusaidia kuilewa Biblia.

      Jifunze kutuhusu kupitia Intaneti. Tembelea tovuti rasmi ya Mashahidi wa Yehova. Hapo unaweza kusoma Biblia na vilevile kusoma au kuchapisha machapisho yetu katika lugha zaidi ya 750.

  • Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina gani?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
    • SOMO LA 1

      Mashahidi wa Yehova Ni Watu wa Aina Gani?

      Shahidi wa Yehova nchini Denmark

      Denmark

      Mashahidi wa Yehova nchini Taiwan

      Taiwan

      Mashahidi wa Yehova nchini Venezuela

      Venezuela

      Mashahidi wa Yehova nchini India

      India

      Unawajua Mashahidi wa Yehova wangapi? Baadhi yetu ni majirani, wafanyakazi, au hata wanafunzi wenzako. Huenda tumewahi kuzungumza nawe kuhusu Biblia. Sisi ni akina nani, na kwa nini tunawaeleza watu kuhusu imani yetu hadharani?

      Sisi ni watu wa kawaida. Tumetoka katika malezi na jamii tofauti-tofauti. Baadhi yetu walikuwa wafuasi wa dini mbalimbali na hata wengine hawakuamini kuna Mungu. Hata hivyo, kabla ya kuwa Mashahidi, sote tulichunguza kwa makini mafundisho ya Biblia. (Matendo 17:11) Tuliamini mambo tuliyojifunza, kisha tukaamua sisi wenyewe kumwabudu Yehova Mungu.

      Tunafaidika kwa kujifunza Biblia. Kama watu wengine, sisi pia tunakabiliana na matatizo na udhaifu wetu wenyewe. Lakini kwa kujitahidi kutumia kanuni za Biblia katika maisha yetu ya kila siku, tunajionea mabadiliko makubwa maishani. (Zaburi 128:1, 2) Hiyo ndiyo sababu moja inayofanya tuwaeleze wengine kuhusu mambo mazuri ambayo tumejifunza katika Biblia.

      Tunaishi kulingana na viwango vya Mungu. Viwango hivyo tunavyojifunza katika Biblia vinatusaidia kuwa na hali njema na kuwaheshimu wengine, kutia ndani kuwa na sifa kama vile unyoofu na fadhili. Viwango hivyo vinatusaidia pia kuwa watu wazuri na wenye manufaa katika jamii. Isitoshe, vinasaidia familia kuwa na umoja na mwenendo mzuri. Kwa sababu tuna uhakika kwamba “Mungu hana ubaguzi,” sisi ni familia kubwa ya ulimwenguni pote ambayo haina ubaguzi wa kijamii wala wa kisiasa. Ingawa sisi ni watu wa kawaida tu, kuna tofauti kati yetu na vikundi vingine.—Matendo 4:13; 10:34, 35.

      • Ni mambo gani yanayoonyesha kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu wa kawaida tu?

      • Mashahidi wamejifunza viwango gani katika Biblia?

  • Kwa Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
    • SOMO LA 2

      Kwa Nini Tunaitwa Mashahidi wa Yehova?

      Noa

      Noa

      Abrahamu na Sara

      Abrahamu na Sara

      Musa

      Musa

      Yesu Kristo

      Yesu Kristo

      Watu wengi wanafikiri kwamba Mashahidi wa Yehova ni jina la dini mpya. Hata hivyo, zaidi ya miaka 2,700 iliyopita, watumishi wa Mungu wa pekee wa kweli waliitwa “mashahidi” wake. (Isaya 43:10-12) Kabla ya mwaka wa 1931, tulikuwa tukiitwa Wanafunzi wa Biblia. Kwa nini basi tulianza kutumia jina Mashahidi wa Yehova?

      Jina hilo linamtambulisha Mungu wetu. Kulingana na maandishi ya kale, jina la Mungu, Yehova, linapatikana mara elfu kadhaa katika Biblia. Katika tafsiri nyingi jina hilo limeondolewa na badala yake majina ya cheo, kama vile Bwana au Mungu, yametumiwa. Hata hivyo, Mungu alijifunua kwa Musa akitumia jina lake binafsi, Yehova, na kusema: “Hilo ndilo jina langu milele.” (Kutoka 3:15) Jina hilo linamtofautisha na miungu yote ya uwongo. Tunajivunia kuitwa kwa jina takatifu la Mungu.

      Jina hilo linafafanua kazi yetu. Watu wengi katika nyakati za kale, kuanzia Abeli aliyekuwa mwadilifu, walitoa ushahidi kuhusu imani yao katika Yehova. Kwa muda mrefu, Noa, Abrahamu, Sara, Musa, Daudi, na wengineo walijiunga na hilo “wingu kubwa . . . la mashahidi.” (Waebrania 11:4–12:1) Kama vile mtu anavyoweza kutoa ushahidi mahakamani ili kumtetea mtu asiye na hatia, sisi pia tumeazimia kutangaza ukweli kumhusu Mungu.

      Tunapotumia jina hilo tunamwiga Yesu. Biblia inamwita “shahidi mwaminifu na wa kweli.” (Ufunuo 3:14) Yesu mwenyewe alisema kwamba ‘alilijulisha jina la Mungu’ naye akaendelea ‘kutoa ushahidi kuhusu kweli.’ (Yohana 17:26; 18:37) Hivyo, wafuasi wa kweli wa Kristo, wanaitwa kwa jina la Yehova, nao huwajulisha watu jina hilo. Hilo ndilo jambo ambalo Mashahidi wa Yehova wanajitahidi kufanya.

      • Kwa nini Wanafunzi wa Biblia walianza kuitwa Mashahidi wa Yehova?

      • Yehova amekuwa na mashahidi duniani kwa muda gani?

      • Ni nani aliye Shahidi mkuu wa Yehova?

      PATA KUJUA MENGI ZAIDI

      Unapokutana na washiriki wa kutaniko, jitahidi kuwafahamu vizuri zaidi. Waulize: “Kwa nini uliamua kuwa Shahidi wa Yehova?”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki