Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Utaona Mambo Gani Katika Mikutano Yetu ya Kikristo?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
    • SOMO LA 5

      Utaona Mambo Gani Katika Mikutano Yetu ya Kikristo?

      Mashahidi wa Yehova wakiwa katika Jumba la Ufalme nchini Argentina

      Argentina

      Mkutano wa Mashahidi wa Yehova Nchini Sierra Leone

      Sierra Leone

      Mkutano wa Mashahidi wa Yehova Nchini Ubelgiji

      Ubelgiji

      Mkutano wa Mashahidi wa Yehova Nchini Malasia

      Malasia

      Watu wengi wameacha kwenda katika dini zao kwa sababu hawapati mwongozo au faraja ya kiroho. Kwa nini basi uhudhurie mikutano ya Kikristo ya Mashahidi wa Yehova? Utaona mambo gani huko?

      Shangwe ya kuwa miongoni mwa watu wenye upendo na wanaojali. Katika karne ya kwanza, Wakristo walipangwa katika makutaniko, nao walikutanika ili kumwabudu Mungu, kujifunza Maandiko, na kutiana moyo. (Waebrania 10:24, 25) Wakiwa wamekusanyika pamoja na watu wenye upendo, walihisi kwamba wako miongoni mwa marafiki wa kweli, ndugu zao wa kiroho. (2 Wathesalonike 1:3; 3 Yohana 14) Tunafanya vivyo hivyo leo, nasi tunapata shangwe kama yao.

      Faida ya kujifunza jinsi ya kutumia kanuni za Biblia. Kama ilivyokuwa katika nyakati za Biblia, leo pia, wanaume, wanawake, na watoto hukutanika pamoja. Walimu wanaostahili huitumia Biblia kutusaidia kuelewa jinsi ya kutumia kanuni za Biblia maishani. (Kumbukumbu la Torati 31:12; Nehemia 8:8) Wote wanaweza kushiriki katika mazungumzo na kuimba. Kufanya hivyo hutupa nafasi ya kutangaza tumaini letu la Kikristo.—Waebrania 10:23.

      Imani yako katika Mungu itaimarishwa. Mtume Paulo aliliambia hivi kutaniko moja: “Ninatamani kuwaona ninyi ili . . . tutiane moyo, kila mmoja kupitia imani ya mwenzake, yenu na yangu pia.” (Waroma 1:11, 12) Tunaposhirikiana kwa ukawaida na waamini wenzetu katika mikutano, imani yetu na azimio letu la kuendelea kuishi kulingana na kanuni za Kikristo huimarika.

      Tunakualika uhudhurie mikutano yetu ili ujionee mwenyewe mambo hayo. Utakaribishwa kwa uchangamfu. Hakuna kiingilio katika mikutano yetu wala sadaka hazitolewi.

      • Mikutano yetu inafuata mfano gani?

      • Tunawezaje kufaidika kwa kuhudhuria mikutano ya Kikristo?

      PATA KUJUA MENGI ZAIDI

      Ikiwa ungependa kuona jinsi Jumba la Ufalme lilivyo ndani kabla ya kuanza kuhudhuria mikutano, mwombe mmoja wa Mashahidi wa Yehova akutembeze na kukuonyesha jinsi lilivyo.

  • Tunafaidikaje kwa Kushirikiana na Wakristo Wenzetu?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
    • SOMO LA 6

      Tunafaidikaje kwa Kushirikiana na Wakristo Wenzetu?

      Mashahidi wa Yehova wakifanya tafrija

      Madagaska

      Mashahidi wa Yehova wakishirikiana mkutanoni

      Norway

      Shahidi wa Yehova akimsaidia Mkristo mwenzake

      Lebanoni

      Wazee Wakristo wamemtembelea Mkristo mwenzao

      Italia

      Hata ikitulazimu kusafiri kupitia msitu mkubwa au hali ya hewa ikiwa mbaya, tunahudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida. Kwa nini Mashahidi wa Yehova wanajitahidi sana kushirikiana na waamini wenzao, licha ya kwamba huenda wakawa na hali ngumu maishani au uchovu baada ya kufanya kazi siku nzima?

      Ni kwa faida yetu. Paulo, alipokuwa akizungumzia wale tunaoshirikiana nao katika kutaniko, alisema “tufikiriane.” (Waebrania 10:24) Neno hilo linamaanisha ni lazima tujuane vizuri. Hivyo, tunatiwa moyo tuwajali wengine. Tunapoendelea kuwafahamu Wakristo wenzetu, tunatambua kwamba baadhi yao wamekabili na kushinda hali fulani ngumu kama yetu na wanaweza kutusaidia ili sisi pia tufaulu.

      Hufanya tuwe na urafiki wa kudumu. Akina ndugu na dada ambao tunakutanika pamoja nao katika mikutano yetu ni rafiki zetu wa karibu, si watu tunaowafahamu tu. Pindi nyingine, tunashirikiana nao katika tafrija. Tunapata faida gani kwa kushirikiana nao kwa njia hizo? Tunajifunza kuwathamini wengine hata zaidi, na jambo hilo linaimarisha upendo kati yetu. Kisha, wenzetu wanapokumbwa na matatizo, tunakuwa tayari kuwasaidia kwa sababu tayari tumejenga urafiki wenye upendo kati yetu. (Methali 17:17) Kwa kushirikiana na wote kutanikoni, tunaonyesha kwamba ‘tunatunzana.’—1 Wakorintho 12:25, 26.

      Tunakutia moyo uchague marafiki wanaofanya mapenzi ya Mungu. Utapata marafiki hao miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Usiruhusu kitu chochote kikuzuie kushirikiana nasi.

      • Kwa nini ni muhimu kwetu kushirikiana pamoja kwenye mikutano?

      • Ungependa kuanza lini kuhudhuria mikutano yetu?

  • Mikutano Yetu Hufanywaje?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
    • SOMO LA 7

      Mikutano Yetu Hufanywaje?

      Mkutano wa Mashahidi wa Yehova nchini New Zealand

      New Zealand

      Mkutano wa Mashahidi wa Yehova nchini Japani

      Japani

      Mvulana akisoma Biblia nchini Uganda

      Uganda

      Mashahidi wawili wakifanya onyesho kuhusu habari fulani ya Biblia nchini Lithuania

      Lithuania

      Sehemu kuu ya mikutano ya Wakristo wa karne ya kwanza ilikuwa kuimba, kusali, hali kadhalika kusoma na kuzungumzia Maandiko. Nayo haikuhusisha desturi za kidini. (1 Wakorintho 14:26) Hivyo ndivyo tunavyofanya mikutano yetu leo.

      Mafundisho yanategemea Biblia na yanatunufaisha. Mwishoni mwa juma, kila kutaniko hukutana ili kusikiliza hotuba ya Biblia kuhusu jinsi Maandiko yanavyohusiana na maisha yetu na nyakati tunamoishi. Sote tunahimizwa kuambatana na msemaji anapokuwa akisoma Maandiko. Baada ya hotuba, kuna Funzo la “Mnara wa Mlinzi” kwa muda wa saa moja. Funzo hilo hutegemea makala ya toleo la funzo la Mnara wa Mlinzi, na wote wako huru kutoa maelezo. Mazungumzo hayo yanatusaidia kuona jinsi tunavyoweza kutumia mwongozo wa Biblia katika maisha yetu. Makutaniko zaidi ya 110,000 ulimwenguni hujifunza habari ileile.

      Tunasaidiwa kuboresha ustadi wa kufundisha. Pia, katikati ya juma sisi hukusanyika kwa ajili ya mkutano wenye sehemu tatu unaoitwa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo ambao hutegemea habari zinazochapishwa kila mwezi katika Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu. Sehemu ya kwanza ya mkutano huo, Hazina za Neno la Mungu, hutusaidia kuelewa sura kadhaa za Biblia ambazo wote katika kutaniko wamezisoma mapema. Kisha, sehemu ya pili, Boresha Huduma Yako, huwa na maonyesho ya jinsi ya kuzungumzia Biblia na wengine. Mshauri hutoa maelezo mafupi yanayotusaidia kuboresha ustadi wetu wa kusoma au kuzungumza. (1 Timotheo 4:13) Sehemu ya mwisho, Maisha ya Mkristo, huzungumzia jinsi tunavyoweza kutumia kanuni za Biblia maishani. Ni sehemu ya mazungumzo ya maswali na majibu ambayo huboresha uelewaji wetu wa Biblia.

      Utakapoanza kuhudhuria mikutano yetu, utafurahia kuona kwamba unaweza kujifunza mengi kuhusu Biblia.—Isaya 54:13.

      • Unaweza kutazamia kusikia mambo gani katika mikutano ya Mashahidi wa Yehova?

      • Ni mkutano gani unaofanywa kila juma ambao ungependa kuhudhuria?

      PATA KUJUA MENGI ZAIDI

      Soma baadhi ya habari zitakazozungumziwa katika mikutano michache inayofuata. Unaposoma, chunguza mambo unayojifunza katika Biblia ambayo yanaweza kukusaidia maishani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki