Wimbo Na. 96
Tafuteni Wanaostahili
Makala Iliyochapishwa
1. Bwana alitufunza kuhubiri,
Akatupa maagizo:
‘Popote mwingiapo, tafuteni,
Wastahilio, wenye njaa.
Wasalimuni na kuwatakia,
Amani wenye kustahili.
Wengine wasipowasikiliza,
Wakung’utieni mavumbi.’
2. Wale wanaowapokea ninyi,
Wanamupokea Yesu.
Tumaini la uzima
Litawachochea wajiunge nanyi.
Musihangaikie la kusema,
Yehova atawawezesha.
Maneno ya fadhili, yenye chumvi,
Yatawavutia wapole.
(Ona pia Mdo. 13:48; 16:14; Kol. 4:6.)