HAZINA ZA NENO LA MUNGU | AYUBU 6-10
Ayubu Mwaminifu Aeleza Jinsi Alivyoteseka Sana
Ayubu alipoteza mali zake zote, akafiwa, akawa mgonjwa sana, lakini bado aliendelea kuwa mwaminifu. Kwa hiyo, Shetani alijaribu kumvunja moyo Ayubu ili avunje utimilifu wake. “Rafiki” watatu walimtembelea. Mwanzoni, walionyesha kana kwamba wanamsikitikia. Kisha wakaketi kimya pamoja na Ayubu kwa siku saba, bila kuongea naye hata neno moja la kumfariji. Walipoanza kuongea naye walimlaumu sana na kumshutumu vikali.
Ayubu aliendelea kudumisha ushikamanifu wake kwa Yehova licha ya kukabili hali ngumu sana
Huzuni iliyopita kiasi ilisababisha Ayubu awe na mtazamo usiofaa. Alifikia mkataa kimakosa kwamba Mungu hakujali ikiwa angebaki mwaminifu
Kwa sababu alikuwa amevunjika moyo, Ayubu hakufikiri kwamba huenda kulikuwa na sababu nyingine zilizomfanya ateseke
Licha ya huzuni nyingi, Ayubu aliwaeleza washtaki wake jinsi anavyompenda Yehova