Wimbo Na. 119
Njooni! Mburudishwe
Makala Iliyochapishwa
1. Leo ulimwengu umepotoka;
Haumutambui Mungu.
Mwongozo ufaao twahitaji,
Peke yetu hatuwezi.
Mikutano yetu huburudisha;
Imani huimarisha.
Inatuchochea kutenda mema,
Inatufariji sana.
Hatutaacha amri za Yehova;
Wala kumutumikia.
Twafunzwa mema kwenye mikutano;
Ili tuipende kweli.
2. Mungu ajua mahitaji yetu;
Shauri lake tutii.
Tununue wakati wa kuwapo,
Kwenye mikutano yote.
Wanaume wamwogopao Mungu,
hutufunza njia zake.
Ndugu na dada zetu wa kiroho,
Hututegemeza sana.
Twatazamia wakati ujao,
Kuona wapendwa wetu.
Twafundishwa maisha yafaayo,
Kwa hekima toka juu.
(Ona pia Zab. 37:18; 140:1; Met. 18:1; Efe. 5:16; Yak. 3:17.)