Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • fg somo la 9 maswali 1-5
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha
  • Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa Yenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kufanikisha Maisha ya Jamaa
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
fg somo la 9 maswali 1-5

SOMO LA 9

Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha

1. Kufunga ndoa kunachangiaje furaha ya familia?

Wenzi wa ndoa wakiandikisha ndoa yao kisheria

Habari njema hutoka kwa Yehova, Mungu mwenye furaha, ambaye anataka familia ziwe na furaha. (1 Timotheo 1:11) Yeye ndiye aliyeanzisha ndoa. Ndoa halali kisheria ni muhimu ili familia iwe yenye furaha kwa sababu inaandaa mazingira salama ambayo watoto watalelewa. Wakristo wanapaswa kuheshimu sheria za nchi zao zinazohusu kuandikisha ndoa.​—Soma Luka 2:1, 4, 5.

Mungu anaionaje ndoa? Anataka ndoa iwe muungano wa kudumu kati ya mume na mke. Yehova anataka waume na wake wawe waaminifu kwa wenzi wao wa ndoa. (Waebrania 13:4) Anachukia talaka. (Malaki 2:16) Hata hivyo, anamruhusu Mkristo kutaliki na kuoa au kuolewa tena ikiwa tu mwenzi wake amefanya uzinzi.​—Soma Mathayo 19:3-6, 9.

2. Mume na mke wanapaswa kutendeana jinsi gani?

Wenzi wa ndoa wenye furaha

Yehova aliwaumba wanaume na wanawake ili wakamilishane katika ndoa. (Mwanzo 2:18) Akiwa kichwa cha familia, mume anapaswa kuiandalia familia yake mahitaji ya kimwili na kuifundisha kumhusu Mungu. Anapaswa kumpenda mke wake na kujidhabihu kwa ajili yake. Waume na wake wanapaswa kupendana na kuheshimiana. Kwa kuwa hakuna mume au mke aliye mkamilifu, ni muhimu kujifunza kusameheana ili ndoa iwe yenye furaha.​—Soma Waefeso 4:31, 32; 5:22-25, 33; 1 Petro 3:7.

3. Ikiwa ndoa yenu haina furaha, je, umwache mwenzi wako wa ndoa?

Ikiwa mna matatizo katika ndoa yenu, nyote wawili mnapaswa kujitahidi kutendeana kwa upendo. (1 Wakorintho 13:4, 5) Neno la Mungu halipendekezi kutengana kama njia ya kutatua matatizo ambayo ni ya kawaida katika ndoa.​—Soma 1 Wakorintho 7:10-13.

4. Watoto, Mungu anataka muwe na maisha ya aina gani?

Wazazi wakiwasaidia watoto wao nyumbani

Yehova anataka muwe wenye furaha. Anawapa mashauri bora kuhusu jinsi mnavyoweza kufurahia ujana wenu. Anataka mnufaike na hekima na uzoefu wa wazazi wenu. (Wakolosai 3:20) Pia, Yehova anataka mpate shangwe inayotokana na kumtumikia Yeye na Mwana wake.​—Soma Mhubiri 11:9–12:1; Mathayo 19:13-15; 21:15, 16.

5. Wazazi, watoto wenu wanahitaji nini ili wawe wenye furaha maishani?

Mzazi akiongea na mtoto wake

Mnapaswa kufanya kazi kwa bidii ili kuwaandalia watoto wenu chakula, makao, na mavazi. (1 Timotheo 5:8) Lakini ili watoto wenu wawe wenye furaha, mnahitaji pia kuwafundisha wampende Mungu na wajifunze kutoka kwake. (Waefeso 6:4) Kielelezo chenu cha kumpenda Mungu kinaweza kuwachochea sana watoto wenu. Mkitegemea Neno la Mungu, maagizo mnayowapa yanaweza kuwasaidia wawe na mtazamo unaofaa.​—Soma Kumbukumbu la Torati 6:4-7; Methali 22:6.

Watoto hunufaika mnapowatia moyo na kuwapongeza. Wanahitaji pia kurekebishwa na kutiwa nidhamu. Kuwazoeza kwa njia hiyo kutawasaidia waepuke mwenendo unaoweza kuwafanya wakose furaha. (Methali 22:15) Hata hivyo, nidhamu haipaswi kamwe kutolewa kwa ukali au kwa ukatili.​—Soma Wakolosai 3:21.

Mashahidi wa Yehova wamechapisha vitabu kadhaa ambavyo vimekusudiwa hasa kuwasaidia wazazi na watoto. Vitabu hivyo vinategemea Biblia.​—Soma Zaburi 19:7, 11.

Unaweza kupata habari zaidi katika sura ya 14 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki