Wimbo Na. 115
Kufanikisha Maisha Yetu
Makala Iliyochapishwa
1. Twapenda Neno la Mungu,
Tusome daima.
Kila siku maishani,
Na kutafakari.
Lituongoze milele,
Kwa neno na tendo.
(KORASI)
Someni, mutafakari.
Mupate baraka.
Mukitembea na Mungu,
Mutafanikiwa.
2. Wafalme wa Israeli,
Waliamuriwa:
‘Jiandikie nakala,
Sheria ya Mungu.’
Daima na waisome,
Wasikengeuke.
(KORASI)
Someni, mutafakari.
Mupate baraka.
Mukitembea na Mungu,
Mutafanikiwa.
3. Tusomapo Neno Lake,
Twapata faraja.
Linatuliza mioyo;
Lajenga imani.
Tukitii tusomayo,
Tutasonga mbele.
(KORASI)
Someni, mutafakari.
Mupate baraka.
Mukitembea na Mungu,
Mutafanikiwa.
(Ona pia Kum. 17:18; 1 Fal. 2:3, 4; Zab. 119:1; Yer. 7:23.)