HAZINA ZA NENO LA MUNGU | ISAYA 58-62
“Kutangaza Mwaka wa Nia Njema Upande wa Yehova”
“Mwaka wa nia njema upande wa Yehova” si mwaka halisi
Ni kipindi cha wakati ambacho Yehova anawapatia wapole nafasi ya kukubali tangazo lake la uhuru
Katika karne ya kwanza, mwaka wa nia njema ulianza Yesu alipoanza huduma yake mwaka wa 29 W.K. na uliendelea mpaka “siku ya kisasi” ya Yehova wakati Yerusalemu lilipoharibiwa mwaka wa 70 W.K.
Katika siku zetu, mwaka wa nia njema ulianza Yesu alipoanza kutawala mbinguni mwaka wa 1914 na utakwisha wakati wa dhiki kuu
Yehova amewabariki watu wake kwa kuwapa “miti mikubwa ya uadilifu”
Mara nyingi miti mirefu zaidi duniani hukua pamoja katika misitu, mahali ambapo miti hutegemezana
Mizizi mikubwa ya miti inaweza kujisokota, kwenda chini sana ili kuilinda miti hiyo dhidi ya dhoruba
Miti mikubwa hutoa kivuli kinacholinda miti michanga, na majani yake yanapoanguka yanarutubisha ardhi
Washiriki wote wa kutaniko la Kikristo ulimwenguni pote wananufaika kutokana na utegemezo na ulinzi wa “miti mikubwa ya uadilifu,” yaani, mabaki ya watiwa-mafuta