HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 1 WAKORINTHO 10-13
Yehova Ni Mwaminifu
Huenda Yehova akachagua kutuondolea jaribu; hata hivyo, mara nyingi yeye huandaa “njia ya kutokea” kwa kutupa kile tunachohitaji ili tuweze kuvumilia jaribu.
Anaweza kutuliza akili, moyo, na hisia zetu kupitia Neno lake, roho yake takatifu, na chakula cha kiroho anachoandaa.—Mt 24:45; Yoh 14:16, maelezo ya chini; Ro 15:4
Anaweza kutuongoza kupitia roho yake takatifu, ambayo inaweza kutusaidia tukumbuke masimulizi na kanuni za Biblia, kisha tutambue hatua za hekima tunazopaswa kuchukua.—Yoh 14:26
Anaweza kutumia malaika kutusaidia.—Ebr 1:14
Anaweza kutusaidia kupitia waabudu wenzetu.—Kol 4:11