Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ratiba ya Juma Linaloanza Machi 25
    Huduma ya Ufalme—2013 | Machi
    • Ratiba ya Juma Linaloanza Machi 25

      JUMA LINALOANZA MACHI 25

      Wimbo 76 na Sala

      □Funzo la Biblia la Kutaniko:

      jr sura ya 7 ¶1-6 (Dak. 30)

      □ Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:

      Usomaji wa Biblia: Luka 4-6 (Dak. 10)

      Na. 1: Luka 4:22-39 (Isizidi dak. 4)

      Na. 2: Jamii Mbalimbali Zilitoka Wapi?—rs uku. 95 ¶1-4 (Dak. 5)

      Na. 3: Kuna Uthibitisho Gani Kwamba Yesu Alifufuliwa?—1 Kor. 15:3-7 (Dak. 5)

      □ Mkutano wa Utumishi:

      Wimbo 111

      Dak. 5: Kuanzisha Funzo la Biblia Katika Jumamosi ya Kwanza. Ukitumia mapendekezo yaliyo katika ukurasa wa 8, panga kuwe na onyesho la jinsi funzo la Biblia linavyoweza kuanzishwa katika Jumamosi ya kwanza ya mwezi wa Aprili. Watie moyo wote washiriki.

      Dak. 25: “Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!” Maswali na majibu. Panga kuwe na maonyesho mawili ambayo yatafanywa unapozungumzia fungu la 6.

      Wimbo 97 na Sala

  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013 | Machi
    • 3. Broshua hii inatofautianaje na machapisho mengine ya funzo?

      3 Jinsi Ilivyo: Mengi ya machapisho yetu ya funzo yameandikwa ili mtu aweze kuyasoma na kuelewa kweli hata bila kusaidiwa na mtu mwingine. Broshua hii ni tofauti. Imechapishwa ili mtu ajifunze Biblia akiwa pamoja na mwalimu. Kwa hiyo, unapomtolea mtu broshua hiyo, ni vyema kusoma na kuzungumzia fungu moja au mawili. Mafungu ni mafupi, hivyo yanaweza hata kuzungumziwa mlangoni mwa mwenye nyumba au mahali anapofanyia kazi. Ingawa inafaa kuanza na somo la 1, tunaweza kuanzisha funzo kwa kutumia somo lolote katika broshua hiyo.

      4. Broshua Habari Njema hutusaidiaje kufundisha moja kwa moja kutoka katika Biblia?

      4 Katika mengi ya machapisho yetu, majibu ya maswali yaliyochapwa yanaweza kupatikana kwenye mafungu. Hata hivyo katika chapisho hili, majibu yanapatikana hasa kwenye Biblia. Watu wengi hutaka kujifunza kutoka kwenye Biblia badala ya machapisho yetu. Hivyo, maandiko mengi hayajanukuliwa. Yanapaswa kusomwa moja kwa moja kutoka kwenye Biblia. Hilo huwasaidia wanafunzi kutambua kwamba mambo wanayojifunza yanatoka kwa Mungu.—Isa. 54:13.

      5. Kwa nini ni muhimu kwa mwalimu kujiandaa vizuri kwa ajili ya kila kipindi cha funzo?

      5 Broshua hiyo haifafanui maandiko yote. Kwa nini? Imekusudiwa kumtia moyo mwanafunzi aulize maswali na kumpa mwalimu nafasi ya kutumia uwezo wake wa kufundisha. Kwa hiyo, ni muhimu kujitayarisha vizuri kwa ajili ya kila kipindi cha funzo. Tahadhari: Usiongee kupita kiasi. Tunapenda kufafanua Maandiko. Lakini kwa kawaida tunatimiza mengi zaidi kwa kumwomba mwanafunzi aeleze maoni yake kuhusu maana ya andiko fulani. Kwa kutumia maswali kwa busara, tunaweza kumsaidia apate maana ya kila andiko.—Mdo. 17:2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki