Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr20 Julai kur. 1-5
  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2020
  • Vichwa vidogo
  • JULAI 6-12
  • JULAI 13-19
  • JULAI 20-26
  • JULAI 27–AGOSTI 2
Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2020
mwbr20 Julai kur. 1-5

Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

JULAI 6-12

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 6-7

“Sasa Utaona Mambo Nitakayomtendea Farao”

it-2 436 ¶3

Musa

Waisraeli walikuwa wamebadili mtazamo wao kabisa. Mwanzoni walikuwa wamemkubali Musa, lakini baada ya kukabili hali ngumu za kazi kutokana na amri ya Farao walimlalamikia Musa hivi kwamba akamsihi Yehova akiwa amevunjika moyo. (Kut 4:29-31; 5:19-23) Pindi hiyo, Aliye Juu Zaidi alimwimarisha kwa kumfunulia kwamba angetimiza kile ambacho Abrahamu, Isaka, na Yakobo walitazamia, yaani, angefunua kikamili maana ya jina lake Yehova kwa kuwakomboa Waisraeli na kuwafanya kuwa taifa kubwa katika nchi ya ahadi. (Kut 6:1-8) Ingawa hivyo bado Waisraeli hawakumsikiliza Musa. Lakini sasa, baada ya pigo la tisa, walimuunga mkono kabisa na kushirikiana naye hivi kwamba baada ya pigo la kumi, alifaulu kuwapanga na kuwaongoza kutoka Misri kwa utaratibu, “wakiwa wamejipanga kivita.”—Kut 13:18.

it-2 436 ¶1-2

Musa

Mbele ya Farao wa Misri. Sasa Musa na Haruni walikuwa wahusika wakuu katika “pambano kati ya miungu.” Akitumia makuhani wachawi, ambao inaelekea wakuu wao walikuwa Yane na Yambre (2Ti 3:8), Farao aliagiza nguvu za miungu yote ya Misri zitumiwe kupambana na nguvu za Yehova. Muujiza wa kwanza ambao Haruni alifanya mbele ya Farao alipoagizwa na Musa ulionyesha kwamba Yehova ni mkuu kuliko miungu ya Misri, ingawa Farao aliendelea kuwa mkaidi. (Kut 7:8-13) Kisha baada ya pigo la tatu kutokea, hata makuhani wachawi walilazimika kusema “Ni kidole cha Mungu!” Waliathiriwa sana na pigo la majipu hivi kwamba hawangeweza kwenda mbele ya Farao ili kupambana na Musa wakati wa pigo hilo.—Kut 8:16-19; 9:10-12.

Mapigo yalilainisha mioyo fulani na kufanya mioyo mingine iwe migumu. Musa na Haruni ndio waliotangaza kila moja kati ya yale Mapigo Kumi. Mapigo yalitokea kama walivyotangaza, na kuthibitisha kwamba Musa alikuwa mwakilishi wa Yehova. Jina la Yehova lilitangazwa na kuzungumziwa sana huko Misri, hilo lilifanya mioyo fulani ilainike huku mingine ikiwa migumu kuelekea jina hilo—mioyo ya Waisraeli na baadhi ya Wamisri ililainika; lakini mioyo ya Farao, washauri, na wafuasi wake ikawa migumu. (Kut 9:16; 11:10; 12:29-39) Badala ya kuamini kwamba walikuwa wameikasirisha miungu yao, Wamisri walijua kwamba Yehova ndiye aliyekuwa akihukumu miungu yao. Kufikia wakati ambapo mapigo tisa yalikuwa yametokea, Musa pia alikuwa “mtu anayeheshimiwa sana na watumishi wa Farao na watu wengine nchini Misri.”—Kut 11:3.

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-1 78 ¶3-4

Mweza-Yote

Yehova alitumia jina la cheo “Mungu Mweza-Yote” (ʼEl Shad·daiʹ) alipokuwa akimtolea Abrahamu ahadi kuhusu kuzaliwa kwa Isaka, ahadi ambayo ingehitaji Abrahamu awe na imani kubwa katika nguvu za Mungu za kutimiza ahadi hiyo. Baadaye jina hilo la cheo lilitumiwa Mungu alipotajwa kuwa yule ambaye angembariki Isaka na Yakobo wakiwa warithi wa agano alilofanya pamoja na Abrahamu.—Mwa 17:1; 28:3; 35:11; 48:3.

Kupatana na hilo, baadaye Yehova angeweza kumwambia hivi Musa: “Nilikuwa nikimtokea Abrahamu, Isaka, na Yakobo kama Mungu Mweza-Yote [beʼElʹ Shad·daiʹ], lakini kwa jina langu Yehova sikujitambulisha kwao.” (Kut 6:3) Hilo halimaanishi kwamba wazee hao wa ukoo hawakulijua jina Yehova, kwa sababu walilitumia mara kwa mara na lilitumiwa pia na watu wengine walioishi kabla yao. (Mwa 4:1, 26; 14:22; 27:27; 28:16) Katika kitabu cha Mwanzo ambacho kina masimulizi ya wazee hao wa ukoo, jina la cheo “Mweza-Yote” linapatikana mara sita tu, lakini jina la kibinafsi Yehova liliandikwa mara 172 katika maandishi ya awali ya Kiebrania. Ingawa wazee hao wa ukoo walikuwa wameelewa kwamba Mungu anastahili kuitwa kwa jina la cheo “Mweza-Yote,” hawakupata nafasi ya kuelewa maana kamili na matumizi ya jina lake la kibinafsi, Yehova. Kuhusiana na hilo, kitabu The Illustrated Bible Dictionary (Buku la 1, uku. 572) kinasema hivi: “Wazee wa Ukoo, walifunuliwa mwanzoni jina hilo kuhusiana na ahadi ambazo zingetokea muda mrefu wakati ujao; inaonekana kufunuliwa huko kulikusudiwa kuwahakikishia kwamba Yeye, Yahweh, alikuwa Mungu (ʼel) mwenye uwezo (mojawapo ya maana ya neno sadday) wa kuzitimiza. Kufunuliwa kulikotokea kwenye kichaka kulikuwa na maana kubwa zaidi, kwa kuwa nguvu za Mungu na uwepo wake wa kuendelea ulihusianishwa na jina Yahweh ambalo walilifahamu.”—Imehaririwa na J. D. Douglas, 1980.

it-2 435 ¶5

Musa

Musa hakukataliwa kwa sababu ya kutojiamini. Musa hakujiamini, alitoa kisingizio kwamba hangeweza kuzungumza kwa ufasaha. Musa alikuwa amebadilika, alikuwa tofauti kabisa na Musa ambaye kwa hiari alikuwa amejitolea kuwakomboa Waisraeli miaka 40 hapo awali. Aliendelea kumsisitizia Yehova na kumwomba amwondolee jukumu hilo. Ingawa hilo lilimfanya Yehova akasirike, hakumkataa Musa bali alimchagua Haruni ndugu yake Musa awe msemaji wake. Kwa kuwa Musa angekuwa mwakilishi wa Mungu, basi Musa akawa “Mungu” kwa Haruni, ambaye alizungumza kwa niaba yake. Katika mkutano waliofanya pamoja na wanaume wazee wa Israeli na walipoenda mbele ya Farao, inaonekana Mungu alimpa Musa maagizo na amri, kisha Musa akamjulisha Haruni, naye Haruni akazungumza na Farao (mrithi wa Farao ambaye Musa alikuwa amemkimbia miaka 40 hapo awali). (Kut 2:23; 4:10-17) Baadaye, Yehova alimtaja Haruni kuwa “nabii” wa Musa, akimaanisha kwamba kama vile Musa alivyokuwa nabii wa Mungu, akiongozwa naye, vivyo hivyo Haruni angefuata mwongozo wa Musa. Vilevile Musa aliambiwa kwamba angefanywa kuwa “kama Mungu kwa Farao,” yaani, angekuwa na nguvu na mamlaka ya Mungu juu ya Farao, hivi kwamba hangemwogopa mfalme wa Misri.—Kut 7:1, 2.

JULAI 13-19

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 8-9

“Farao Mwenye Kiburi Atumiwa Kutimiza Kusudi la Mungu”

it-2 1040-1041

Ukaidi

Katika kushughulika na wanadamu, Yehova Mungu ameonyesha subira kwa kuruhusu watu mmoja-mmoja wanaostahili kufa na mataifa yanayostahili kuangamizwa, yaendelee kuwepo. (Mwa 15:16; 2Pe 3:9) Ingawa baadhi ya watu na mataifa wameitikia vizuri kwa kuchukua hatua inayofaa ili kuonyeshwa rehema (Yos 2:8-14; 6:22, 23; 9:3-15), wengine wameonyesha ukaidi kwa kiwango kikubwa zaidi kumwelekea Yehova na kuelekea watu wake. (Kum 2:30-33; Yos 11:19, 20) Kwa kuwa Yehova hawazuii watu kuwa wakaidi, inasemekana kwamba ‘anawaacha wawe wakaidi’ au ‘anaifanya mioyo yao iwe migumu.’ Mwishowe anapoamua kulipiza kisasi dhidi ya wakaidi, matokeo ni kwamba anaonyesha nguvu zake nyingi na kufanya jina lake litangazwe.—Linganisha Kut 4:21; Yoh 12:40; Ro 9:14-18.

it-2 1181 ¶3-5

Uovu

Isitoshe, Yehova Mungu hutumia hali mbalimbali na kufanya waovu watimize makusudi yake bila kujua. Ingawa wanampinga Mungu, anaweza kuwazuia kwa kadiri inayohitajika ili kuwalinda watumishi wake wanapodumisha utimilifu wao, na hata anaweza kufanya matendo ya watu kama hao yaonyeshe wazi uadilifu wake. (Ro 3:3-5, 23-26; 8:35-39; Zb 76:10) Wazo hilo linatajwa kwenye Methali 16:4: “Yehova amefanya kila kitu kitimize kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya msiba.”

Mfano mmoja ni Farao ambaye Yehova, kupitia Musa na Haruni, alimwagiza awaachilie Waisraeli waliokuwa utumwani. Mungu hakumfanya mtawala huyo wa Misri awe mwovu, lakini alimruhusu aendelee kuishi na pia akaleta hali zilizofanya Farao athibitishe kwamba alikuwa mwovu na alistahili kufa. Kusudi la Mungu kufanya hivyo linaonyeshwa kwenye Kutoka 9:16: “Lakini nimekuacha uendelee kuishi kwa sababu hii hasa: ili nikuonyeshe nguvu zangu na ili jina langu litangazwe katika dunia yote.”

Mapigo Kumi yaliyoletwa juu ya Misri, yalifikia kilele Farao alipoangamizwa pamoja na jeshi lake kwenye Bahari Nyekundu, na hivyo nguvu za Yehova zikaonekana kwa njia yenye kustaajabisha. (Kut 7:14–12:30; Zb 78:43-51; 136:15) Kwa miaka mingi baada ya hapo, mataifa yaliyokuwa jirani yaliendelea kuzungumza kuhusu jambo hilo, na hivyo jina la Mungu likatangazwa duniani kote. (Yos 2:10, 11; 1Sa 4:8) Kama Yehova angemuua Farao papo hapo, hangepata fursa ya kuonyesha nguvu na utukufu Wake na kuwakomboa watu wake kwa njia hiyo.

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-1 878

Nzi

Haijulikani wazi mdudu ambaye hasa anarejelewa na neno la awali la Kiebrania linalopatikana kwenye Maandiko kuhusiana na pigo la nne juu ya Misri, pigo la kwanza ambalo halikuwapata Waisraeli huko Gosheni. (Kut 8:21, 22, 24, 29, 31; Zb 78:45; 105:31) Nzi waliowavamia Wamisri katika pigo la nne huenda walikuwa aina inayochoma ngozi ya wanyama na pia binadamu na kisha kufyonza damu yao. Aina fulani ya nzi wanapokuwa kwenye hatua ya kiwavi huishi katika miili ya wanyama na binadamu; nzi wanaovamia binadamu wanapatikana katika maeneo ya tropiki. Basi pigo la nzi kama hao lilisababisha mateso makubwa kwa Wamisri na wanyama wao, na katika visa fulani, lilisababisha kifo.

JULAI 20-26

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 10-11

it-2 436 ¶4

Musa

Alihitaji ujasiri na imani ili kwenda mbele ya Farao. Ilikuwa tu kwa nguvu za Yehova na utendaji wa roho yake takatifu kwamba Musa na Haruni walifanikiwa kutimiza jukumu walilopewa. Wazia ua wa makao ya Farao, mfalme aliyetawala serikali kuu zaidi ya ulimwengu wakati huo. Farao mwenye kiburi alikuwa na ukuu usio na kifani, alionwa kuwa Mungu, alizungukwa na washauri, makamanda wa kijeshi, walinzi, na watumwa. Isitoshe, kulikuwa na viongozi wa kidini, makuhani wachawi, ambao waliongoza katika kumpinga Musa. Mbali na Farao, wanaume hao walikuwa watu wenye mamlaka zaidi katika utawala huo. Wonyesho huo wote wa mamlaka ulikusudiwa kumchochea Farao kuitukuza miungu ya Misri. Na Musa na Haruni hawakwenda mbele ya Farao mara moja tu bali mara nyingi, na kila pindi moyo wa Farao ulizidi kuwa mgumu hata zaidi, kwa sababu alikuwa ameazimia kuwamiliki watumwa wake Waebrania waliokuwa na thamani kwake. Baada ya Musa na Haruni kutangaza pigo la nane, walifukuzwa kutoka mbele ya Farao, na baada ya pigo la tisa waliamriwa wasithubutu tena kuutazama uso wa Farao la sivyo wangeuawa.—Kut 10:11, 28.

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-1 783 ¶5

Kutoka

Kupitia wonyesho wenye kustaajabisha wa nguvu zake Yehova alitukuza jina lake na kuwakomboa Waisraeli. Wakiwa salama upande wa Mashariki wa Bahari Nyekundu, Musa aliwaongoza Waisraeli kuimba wimbo, huku Miriamu dada yake, aliyekuwa nabii wa kike, akachukua matari na kuwaongoza wanawake kucheza dansi wakiwa na matari, wakiitikia wimbo ulioimbwa na wanaume. (Kut 15:1, 20, 21) Waisraeli walikuwa kuwa wametenganishwa kabisa na adui zao. Walipotoka Misri hawangepatwa na madhara yoyote kutoka kwa binadamu au mnyama; hata hakuna mbwa aliyewakaribia Waisraeli wala kuwabwekea. (Kut 11:7) Ingawa simulizi la Kutoka halisemi ikiwa Farao aliingia baharini pamoja na jeshi lake na kuangamizwa, Zaburi 136:15 inasema kwamba Yehova “alimkung’uta Farao na jeshi lake ndani ya Bahari Nyekundu.”

JULAI 27–AGOSTI 2

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | KUTOKA 12

“Pasaka—Inawahusuje Wakristo”

it-2 583 ¶6

Pasaka

Yesu alitimiza baadhi ya mambo yaliyohusiana na Pasaka. Mojawapo ya mambo hayo ni damu iliyopakwa kwenye nyumba nchini Misri ili kuwakomboa wazaliwa wa kwanza wasiangamizwe na malaika. Paulo anataja Wakristo watiwa-mafuta kuwa kutaniko la wazaliwa wa kwanza (Ebr 12:23), na Kristo kuwa mkombozi wao kupitia damu yake. (1Th 1:10; Efe 1:7) Mifupa ya mwanakondoo wa Pasaka haikupaswa kuvunjwa. Ilitabiriwa kwamba hakuna mfupa wa Yesu ambao ungevunjwa, na hilo lilitimia wakati wa kifo chake. (Zb 34:20; Yoh 19:36) Basi Pasaka iliyoadhimishwa na Wayahudi kwa karne nyingi ni mojawapo ya mambo ambayo Sheria ilikuwa kivuli cha mambo ambayo yangekuja na ambayo yalihusiana na Yesu Kristo, “Mwanakondoo wa Mungu.”—Ebr 10:1; Yoh 1:29.

Kutafuta Hazina za Kiroho

it-2 582 ¶2

Pasaka

Mapigo yote Kumi juu ya Misri yalikuwa hukumu dhidi ya miungu ya Misri, hasa pigo la kumi, kuuawa kwa wazaliwa wa kwanza. (Kut 12:12) Kondoo dume alikuwa kitu kitakatifu kwa mungu Ra, basi kunyunyizwa kwa damu ya mwanakondoo wa Pasaka kwenye kizingiti cha juu cha mlango kulikuwa kufuru mbele ya Wamisri. Vilevile, ng’ombe dume alionwa kuwa mtakatifu, na kuuawa kwa wazaliwa wa kwanza wa ng’ombe dume kungekuwa pigo kwa mungu Osirisi. Farao aliabudiwa kama mwana wa Ra. Basi kuuawa kwa mzaliwa wa kwanza wa Farao kungeonyesha kwamba Ra na Farao hawakuwa na nguvu zozote.

it-1 504 ¶1

Kusanyiko

Mojawapo ya mambo ya pekee kuhusiana na “makusanyiko matakatifu” ni kwamba wakati wa makusanyiko hayo watu hawakupaswa kufanya kazi ngumu. Kwa mfano, katika siku ya kwanza na ya saba ya Sherehe ya Mikate Isiyo na Chachu kulikuwa na “makusanyiko matakatifu,” na Yehova alisema hivi kuyahusu: “Hampaswi kufanya kazi yoyote siku hizo. Mtatayarisha tu chakula kitakacholiwa na kila mtu.” (Kut 12:15, 16) Hata hivyo, wakati wa “makusanyiko matakatifu” makuhani walifanya kazi nyingi ya kumtolea Yehova dhabihu (Law 23:37, 38), bila shaka hawakuvunja amri ya kutofanya kazi za kawaida za kila siku. Katika pindi hizo watu hawakukaa tu bila kufanya chochote bali zilikuwa pindi za kunufaika sana kiroho. Siku ya Sabato ya kila juma, watu walikutana ili kuabudu na kufundishwa hadharani. Kisha walinufaika Neno la Mungu liliposomwa hadharani na kufafanuliwa, zoea ambalo baadaye liliendelea katika masinagogi. (Mdo 15:21) Basi, ingawa watu hawakufanya kazi ngumu siku ya Sabato au pindi nyingine za “makusanyiko matakatifu,” walijitoa kusali na kutafakari kuhusu Muumba na makusudi yake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki