Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rr uku. 206
  • Kijito Kinakuwa Mto Mkubwa!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kijito Kinakuwa Mto Mkubwa!
  • Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mto Unaoleta Baraka
  • Maji Yanayoleta Uhai
  • Miti kwa Ajili ya Chakula na Kuponya
  • “Mahali Ambapo Kijito Hicho Kinapita, Kila Kitu Kitaishi”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Baraka ya Yehova Juu ya “Nchi” Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Furaha ya Kibinadamu Chini ya Serikali ya Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2024
Pata Habari Zaidi
Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
rr uku. 206

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 19B

Kijito Kinakuwa Mto Mkubwa!

Ezekieli anaona kijito kinachotiririka kutoka katika hekalu la Yehova na baada ya kilomita mbili hivi kijito hicho kinakuwa mto wenye kina kirefu! Kwenye kingo za mto anaona miti yenye lishe na inayoponya iliyo na majani mengi. Mambo hayo yanamaanisha nini?

Kijito kinatiririka kutoka hekalu la Yehova na kuwa mto mkubwa. Ishara zinaonyesha kina cha maji. Mikono 1,000: kufikia vifundo vya miguu. Mikono 2,000: kufikia magoti. Mikono 3,000: kufikia kiunoni. Mikono 4,000: kina kirefu kisichoweza kuvukwa kwa miguu.

Mto Unaoleta Baraka

ZAMANI: Baada ya wahamishwa kurudi kwenye nchi yao, walibarikiwa sana waliposhiriki katika kurudisha ibada safi hekaluni

NYAKATI ZETU: Mwaka wa 1919 ibada safi ilirudishwa, na hivyo kufungua njia ili watumishi waaminifu wa Yehova wapate baraka nyingi sana za kiroho

WAKATI UJAO: Baada ya Har–Magedoni, Yehova atatubariki sana kimwili na kiroho

Maji Yanayoleta Uhai

ZAMANI: Yehova aliwabariki sana watu wake watiifu, na walisitawi kiroho hata idadi yao ilipozidi kuongezeka

NYAKATI ZETU: Katika paradiso ya sasa ya kiroho inayoendelea kukua, watu wanaozidi kuongezeka wamefaidika na baraka za kiroho kutoka kwa Yehova zinazozidi kuongezeka na wamekuwa hai kwa njia ya kiroho

WAKATI UJAO: Wale watakaookoka Har–Magedoni wataungana na mamilioni ya watu watakaofufuliwa, na watu wote watapata baraka nyingi za Yehova

Miti kwa Ajili ya Chakula na Kuponya

ZAMANI: Kwa njia ya kiroho, Yehova aliwalisha watu wake waaminifu katika nchi yao iliyorudishwa; pia aliwaponya ugonjwa wa kiroho waliokuwa nao kwa muda mrefu

NYAKATI ZETU: Chakula kingi cha kiroho kinawasaidia watu wakabiliane na ugonjwa na njaa ya kiroho iliyoenea ulimwenguni leo

WAKATI UJAO: Kristo na watawala wenzake 144,000 watawasaidia wanadamu watiifu wafikie ukamilifu na kufurahia afya bora na nguvu milele!

Angalia sura ya 19, fungu la 4-21

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki