SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 19B
Kijito Kinakuwa Mto Mkubwa!
Ezekieli anaona kijito kinachotiririka kutoka katika hekalu la Yehova na baada ya kilomita mbili hivi kijito hicho kinakuwa mto wenye kina kirefu! Kwenye kingo za mto anaona miti yenye lishe na inayoponya iliyo na majani mengi. Mambo hayo yanamaanisha nini?
Mto Unaoleta Baraka
ZAMANI: Baada ya wahamishwa kurudi kwenye nchi yao, walibarikiwa sana waliposhiriki katika kurudisha ibada safi hekaluni
NYAKATI ZETU: Mwaka wa 1919 ibada safi ilirudishwa, na hivyo kufungua njia ili watumishi waaminifu wa Yehova wapate baraka nyingi sana za kiroho
WAKATI UJAO: Baada ya Har–Magedoni, Yehova atatubariki sana kimwili na kiroho
Maji Yanayoleta Uhai
ZAMANI: Yehova aliwabariki sana watu wake watiifu, na walisitawi kiroho hata idadi yao ilipozidi kuongezeka
NYAKATI ZETU: Katika paradiso ya sasa ya kiroho inayoendelea kukua, watu wanaozidi kuongezeka wamefaidika na baraka za kiroho kutoka kwa Yehova zinazozidi kuongezeka na wamekuwa hai kwa njia ya kiroho
WAKATI UJAO: Wale watakaookoka Har–Magedoni wataungana na mamilioni ya watu watakaofufuliwa, na watu wote watapata baraka nyingi za Yehova
Miti kwa Ajili ya Chakula na Kuponya
ZAMANI: Kwa njia ya kiroho, Yehova aliwalisha watu wake waaminifu katika nchi yao iliyorudishwa; pia aliwaponya ugonjwa wa kiroho waliokuwa nao kwa muda mrefu
NYAKATI ZETU: Chakula kingi cha kiroho kinawasaidia watu wakabiliane na ugonjwa na njaa ya kiroho iliyoenea ulimwenguni leo
WAKATI UJAO: Kristo na watawala wenzake 144,000 watawasaidia wanadamu watiifu wafikie ukamilifu na kufurahia afya bora na nguvu milele!