Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwbr22 Septemba kur. 1-2
  • Marejeo ya “Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Marejeo ya “Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha”
  • Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2022
  • Vichwa vidogo
  • SEPTEMBA 26–OKTOBA 2
  • OKTOBA 17-23
  • OKTOBA 31–NOVEMBA 6
Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2022
mwbr22 Septemba kur. 1-2

Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha

SEPTEMBA 26–OKTOBA 2

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 1 WAFALME 15-16

“Asa Alitenda kwa Ujasiri​—Namna Gani Wewe?”

it-1 184-185

Asa

Licha ya kwamba pindi fulani Asa alitenda bila hekima na ufahamu wa kiroho, ni wazi kwamba alikuwa na sifa nyingi nzuri na aliepuka kujihusisha katika ibada ya uwongo, na hivyo anaonwa kuwa mmoja wa wafalme waaminifu wa kabila la Yuda. (2Nya 15:17) Asa alitawala kwa miaka 41 kipindi ambacho wafalme wanane wa Israeli walitawala: Yeroboamu, Nadabu, Baasha, Ela, Zimri, Omri, Tibni (ambaye alitawala sehemu fulani ya Israeli kwa kumpinga Omri), na Ahabu. (1Fa 15:9, 25, 33; 16:8, 15, 16, 21, 23, 29) Asa alipokufa, Yehoshafati mwana wake akawa mfalme.​—1Fa 15:24.

OKTOBA 17-23

HAZINA ZA NENO LA MUNGU | 1 WAFALME 21-22

“Iga Jinsi Yehova Anavyotumia Mamlaka Yake”

it-2 21

Yehova wa Majeshi

Yoshua alipomwona malaika karibu na Yeriko na kumuuliza ikiwa alikuwa upande wa Waisraeli au upande wa maadui wao, malaika huyo alimjibu: “Hapana, mimi ni mkuu wa jeshi la Yehova.” (Yos 5:13-15) Nabii Mikaya alimwambia hivi Mfalme Ahabu na Mfalme Yehoshafati, akiwarejelea wana wa roho wa Yehova: “Nilimwona Yehova akiwa ameketi kwenye kiti chake cha ufalme na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kando yake, upande wake wa kulia na upande wake wa kushoto.” (1Fa 22:19-21) Inafaa kwamba maneno “Yehova wa majeshi” yanarejelea wingi, kwa sababu mbali na kwamba tunasoma malaika wamegawanywa kuwa makerubi, maserafi, na malaika (Isa 6:2, 3; Mwa 3:24; Ufu 5:11) wanafafanuliwa pia kuwa wamepangwa katika vikundi, hivi kwamba Yesu Kristo angeweza kusema kwamba anaweza kuita “vikosi zaidi ya 12 vya malaika.” (Mt 26:53) Hezekia alipokuwa akimsihi Yehova amsaidie, alimwita “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, unayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya makerubi.” Ni wazi kwamba alikuwa akirejelea sanduku la agano na makerubi waliokuwa juu ya kifuniko chake, wakiwakilisha kiti cha ufalme cha Yehova kilicho mbinguni. (Isa 37:16; linganisha 1Sa 4:4; 2Sa 6:2) Mtumishi wa Elisha aliacha kuwa na hofu baada ya kuona kimuujiza milima iliyozunguka jiji ambalo Elisha aliishi ikiwa ‘imejaa farasi na magari ya vita ya moto,’ ambayo ni sehemu ya jeshi la Yehova la malaika.​—2Fa 6:15-17.

it-2 245

Uwongo

Yehova Mungu anaacha watu wanaopenda uwongo “wapotoshwe kupitia udanganyifu, na hivyo waamini uwongo” badala ya habari njema kumhusu Yesu Kristo. (2Th 2:9-12) Kanuni hiyo inaonekana katika kisa cha Mfalme Ahabu wa Israeli kilichotokea karne nyingi mapema. Manabii waongo walimhakikishia Ahabu kwamba angeshinda vita dhidi ya Ramothi-gileadi. Lakini Mikaya nabii wa Yehova alitabiri kwamba wangeshindwa. Kama Mikaya alivyoona katika maono, Yehova alimruhusu malaika mmoja kuwa “roho ya udanganyifu” katika vinywa vya manabii wa Ahabu. Hilo linamaanisha kwamba malaika huyo alitumia nguvu zake kuwadhibiti hivi kwamba hawakusema kweli, bali walisema kile ambacho wao wenyewe walitaka na kile ambacho Ahabu alitaka kusikia. Ingawa Ahabu alikuwa ameonywa kuhusu hilo, alikubali kudanganywa na maneno yao ya uwongo na kwa sababu hiyo akapoteza uhai wake.​—1Fa 22:1-38; 2Nya 18.

OKTOBA 31–NOVEMBA 6

Hazina za Kiroho

it-2 697 ¶2

Nabii

“Wana wa Manabii.” Kitabu Gesenius’ Hebrew Grammar kinaeleza (Oxford, 1952, p. 418), neno la Kiebrania ben (mwana wa) au benehʹ (wana wa) linaweza kurejelea “kuwa mshiriki wa kikundi au jamii (au wa kabila, au wa tabaka hususa).” (Linganisha Ne 3:8, ambapo “mmoja wa watengenezaji wa marashi” kihalisi ni “mwana wa wachanganyaji wa manukato.”) Hivyo, huenda “wana wa manabii” wakawa ni kikundi cha kuwazoeza wale walioteuliwa kufanya kazi hiyo au labda tu ni washiriki wa kikundi cha manabii. Vikundi hivyo vya manabii vinatajwa kuwa vilikuwa Betheli, Yeriko, na Gilgali. (2Fa 2:3, 5; 4:38; linganisha 1Sa 10:5, 10.) Samweli alisimamia kikundi kimoja huko Rama (1Sa 19:19, 20), na inaonekana kwamba Elisha alisimamia kikundi fulani pia katika siku zake. (2Fa 4:38; 6:1-3; linganisha 1Fa 18:13) Biblia inataja kwamba walijenga makao yao wenyewe na kwamba waliazima kifaa fulani, jambo linaloonyesha waliishi maisha rahisi. Ingawa mara nyingi waliishi na kula pamoja, huenda kila mmoja wao alitumwa sehemu mbalimbali ili kutimiza mgawo fulani akiwa nabii.​—1Fa 20:35-42; 2Fa 4:1, 2, 39; 6:1-7; 9:1, 2.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki