Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb22 Novemba uku. 11
  • Endelea Kutarajia Mwisho kwa Uhakika

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea Kutarajia Mwisho kwa Uhakika
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
  • Habari Zinazolingana
  • Endelea Kuwa Mwaminifu Wakati wa “Dhiki Kuu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Ufalme wa Mungu Unaondoa Maadui Wake
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Har–Magedoni Ni Habari Njema!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Jinsi Ulimwengu Huu Utakavyofikia Mwisho Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2022
mwb22 Novemba uku. 11
Ndugu akijifunza kitabu “Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!” Anawazia malaika wa Yehova akilinda kikundi cha watu wa Mungu wakati wa Har–Magedoni.

MAISHA YA MKRISTO

Endelea Kutarajia Mwisho kwa Uhakika

Hivi karibuni sana subira ya Yehova kuelekea ulimwengu huu itafikia kikomo. Dini ya uwongo itaharibiwa, muungano wa mataifa utawashambulia watu wa Mungu, na Yehova atawaangamiza waovu kwenye Har–Magedoni. Wakristo wanatazamia kwa hamu matukio hayo yenye kusisimua.

Bila shaka, hatujui mambo yote kuhusu dhiki kuu. Kwa mfano, hatujui itaanza lini kihususa. Hatujui serikali zitatumia sababu zipi ili kutetea shambulio lao dhidi ya dini. Hatujui mataifa yatawashambulia watu wa Mungu kwa muda mrefu kadiri gani wala hatujui mambo yatakayohusika. Pia hatujui njia hususa ambayo Yehova atatumia kuwaangamiza waovu kwenye Har–Magedoni.

Hata hivyo, Maandiko yanatupa habari zote tunazohitaji ili kuukabili wakati ujao tukiwa na uhakika na ujasiri. Kwa mfano, tunajua kwamba tunaishi katika kipindi cha mwisho cha “siku za mwisho.” (2Ti 3:1) Tunajua kwamba shambulizi dhidi ya dini ‘litafupishwa’ ili dini ya kweli isiharibiwe. (Mt 24:22) Tunajua kwamba Yehova atawakomboa watu wake. (2Pe 2:9) Pia, tunajua kwamba Yule ambaye Yehova amemchagua kuwaangamiza waovu na kuwaokoa umati mkubwa wakati wa Har–Magedoni ni mwadilifu na mwenye nguvu.​—Ufu 19:11, 15, 16.

Bila shaka, matukio ya wakati ujao yatawafanya watu ‘wazimie kwa woga.’ Hata hivyo, kwa kusoma na kutafakari matendo ya Yehova ya wokovu ya wakati uliopita na mambo ambayo amefunua kuhusu wakati ujao, tutaweza ‘kusimama wima na kuinua vichwa vyetu,’ tukiwa na uhakika kwamba ukombozi wetu unakaribia.​—Lu 21:26, 28.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki