SOMO LA 16
Uwe Mwenye Kujenga na Mwenye Kutia Moyo
Ayubu 16:5
MUHTASARI: Kazia fikira mambo yanayoweza kuboresha hali na yanayowachochea wasikilizaji.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Uwe na mtazamo mzuri kuelekea wasikilizaji wako. Jikumbushe kwamba waabudu wenzako wanataka kumpendeza Yehova. Hata ukilazimika kutoa shauri, kwanza jitahidi kuwapongeza kutoka moyoni.
Usizungumzie sana matatizo. Zungumzia mambo yasiyopendeza ikiwa tu mambo hayo ni muhimu katika hotuba. Kwa ujumla, hotuba yako inapaswa kuwa yenye kutia moyo.
Tumia vizuri Neno la Mungu. Kazia kile ambacho Yehova amefanya, anachofanya, na atakachofanya kwa ajili ya wanadamu. Wachochee wasikilizaji wawe na tumaini na ujasiri.