SOMO LA 17
Habari Inayoeleweka
1 Wakorintho 14:9
MUHTASARI: Wasaidie wasikilizaji waelewe maana ya ujumbe wako.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
- Jifunze kwa makini habari unayotayarisha. Jitahidi kuelewa kabisa habari ili uweze kuieleza kwa njia rahisi na kwa maneno yako. 
- Tumia sentensi fupi na maneno rahisi. Ingawa unaweza kutumia sentensi ndefu, wasilisha mawazo makuu ukitumia maneno machache na sentensi fupi. 
- Fafanua maneno yasiyojulikana. Usitumie maneno mengi ambayo wasikilizaji wako hawayaelewi. Ikiwa ni lazima utumie neno lisilojulikana, mhusika katika Biblia, vipimo au utamaduni wa kale, wafafanulie wasikilizaji mambo hayo.