Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lmd somo la 3
  • Fadhili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fadhili
  • Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yesu Alifanya Nini?
  • Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?
  • Mwige Yesu
  • Kupendezwa na Watu
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
  • Acha “Sheria ya Fadhili” Ikuchochee
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Kujitahidi Kuonyesha Fadhili Katika Ulimwengu Wenye Uadui
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Pendeza Yehova kwa Kuonyesha Fadhili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
lmd somo la 3

KUANZISHA MAZUNGUMZO

Yesu akimsogelea mwanamume kipofu ili amponye.

Yohana 9:​1-7

SOMO LA 3

Fadhili

Kanuni: “Upendo ni wenye . . . fadhili.”—1 Kor. 13:4.

Yesu Alifanya Nini?

Jesus gently approaching a blind man in order to heal him.

VIDEO: Yesu Anamponya Mwanamume Kipofu

1. Tazama VIDEO, au soma Yohana 9:​1-7. Kisha fikiria maswali yafuatayo:

  1. Yesu alifanya nini kwanza—alimponya mwanamume kipofu au alimhubiria habari njema?—Ona Yohana 9:​35-38.

  2. Unafikiri kwa nini mwanamume huyo alikuwa tayari kumsikiliza Yesu alipomhubiria habari njema?

Tunajifunza Nini Kutoka kwa Yesu?

2. Huenda mtu akawa tayari kusikiliza ujumbe wetu ikiwa atahisi kwamba tunamjali.

Mwige Yesu

3. Uwe mwenye huruma. Jaribu kuwazia jinsi mtu huyo anavyohisi.

  1. Jiulize: ‘Anahangaishwa na mambo gani? Ni mambo gani yanayoweza kumsaidia na kumvutia?’ Kufanya hivyo kutakusaidia uonyeshe fadhili kwa njia ya kawaida na ya unyofu.

  2. Onyesha kwamba unajali mambo yanayomhangaisha mtu kwa kumsikiliza. Akikueleza jinsi anavyohisi kuhusu jambo fulani au tatizo analokabili, usibadili mazungumzo.

4. Zungumza kwa fadhili na heshima. Jinsi unavyozungumza itaonyesha unamhurumia mtu huyo na kwa kweli unataka kumsaidia. Uwe mwangalifu kuhusu kile unachosema na jinsi unavyosema, epuka kusema mambo yanayoweza kumkasirisha.

5. Toa msaada. Tafuta nafasi zinazofaa za kumsaidia mtu huyo kwa njia hususa. Tunapomwonyesha mtu fadhili, itakuwa rahisi kuanzisha mazungumzo.

SOMA PIA

Rom. 12:​15, 16; Gal. 6:10; Ebr. 13:16

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki