Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • nwt uku. 8-uku. 9
  • Swali la 2: Unawezaje kujifunza kumhusu Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Swali la 2: Unawezaje kujifunza kumhusu Mungu?
  • Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Swali la 2: Unawezaje kujifunza kumhusu Mungu?

SWALI LA 2

Unawezaje kujifunza kumhusu Mungu?

“Kitabu hiki cha Sheria kisiondoke kinywani mwako, ni lazima ukisome kwa sauti ya chini mchana na usiku ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yaliyoandikwa humo; ndipo utakapofanikisha njia yako na kutenda kwa hekima.”

Yoshua 1:8

“Wakaendelea kusoma kwa sauti kubwa kitabu hicho cha Sheria ya Mungu wa kweli, nao wakafafanua, na kueleza maana yake; hivyo wakawasaidia watu kuelewa mambo yaliyokuwa yakisomwa.”

Nehemia 8:8

“Mwenye furaha ni mtu ambaye hatembei katika mashauri ya waovu . . . , lakini anapendezwa na sheria ya Yehova, naye huisoma sheria Yake kwa sauti ya chini mchana na usiku. . . . Kila jambo analofanya litafanikiwa.”

Zaburi 1:​1-3

“Filipo akakimbia kandokando na kumsikia akimsoma kwa sauti kubwa nabii Isaya, akamuuliza: ‘Je, kweli unajua unayosoma?’ Akajibu: ‘Kwa kweli, ninawezaje kuyaelewa mtu fulani asiponiongoza?’”

Matendo 8:​30, 31

“Sifa zake zisizoonekana, zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea, kwa sababu zinaeleweka kupitia vitu vilivyoumbwa, yaani, nguvu zake za milele na Uungu, hivi kwamba hawana sababu ya kujitetea.”

Waroma 1:​20

“Tafakari mambo haya; zama katika hayo, ili maendeleo yako yaonekane wazi kwa watu wote.”

1 Timotheo 4:​15

“Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukutana pamoja.”

Waebrania 10:​24, 25

“Ikiwa yeyote kati yenu anakosa hekima, na aendelee kumwomba Mungu, kwa maana yeye huwapa wote kwa ukarimu na bila kushutumu, naye atapewa.”

Yakobo 1:5

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki