Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 10/12 uku. 5
  • Omba Msaada

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Omba Msaada
  • Amkeni!—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Ninawezaje Kuwa na Uhusiano Mzuri na Mwalimu Wangu?
    Vijana Huuliza
  • Ninaweza Kufanya Nini ili Nielewane na Mwalimu Wangu?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • Kwa Nini Tunahitaji Walimu?
    Amkeni!—2002
  • Funguo za Elimu Nzuri
    Amkeni!—1995
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2012
g 10/12 uku. 5
[Picha katika ukurasa wa 5]

Omba Msaada

Kuwa na watu wanaoweza kukushauri na kukutegemeza ni muhimu sasa ukiwa shuleni na pia itakuwa muhimu hata zaidi utakapokuwa mtu mzima.

NI NANI wanaoweza kukusaidia ufanikiwe shuleni?

Familia.

“Nilipohitaji kusaidiwa kufanya kazi zangu za shuleni,” anasema Bruna, msichana mwenye umri wa miaka 18 anayeishi Brazili, “Baba yangu alinifafanulia habari hiyo, kisha akaniuliza maswali ambayo yalinisaidia kufikiri na kujipatia jibu mimi mwenyewe.”a

Dokezo: Anza kwa kumwuliza mzazi wako alifanyaje katika somo unaloliona kuwa gumu. Ikiwa alifanya vizuri, huenda akakusaidia.

Walimu.

Walimu wengi hufurahi kujua kwamba mwanafunzi anataka kufanikiwa, na hawatasita kumsaidia.

Dokezo: Unaweza kumwambia hivi mwalimu wako, “Naona somo hili kuwa gumu, na ninataka kufanikiwa. Ungependekeza nifanye nini?”

Washauri.

Labda rafiki wa familia mwenye kutegemeka anaweza kukusaidia. Kuwa na mshauri kunaweza kuwa na manufaa mara mbili: Kwanza, utapata msaada unaohitaji; na pili, utajifunza kutafuta msaada kutoka kwa watu wengine unapouhitaji—jambo ambalo litakusaidia hata katika maisha ya utu uzima. Kwa kweli, ili mtu afanikiwe katika mambo mengi, badala ya kujitegemea tu, anahitaji msaada wa watu wengine.​—Methali 15:22.

Dokezo: Waulize wazazi wako ni nani anayeweza kuwa mshauri mzuri.

Jambo kuu: Usiogope kuomba msaada!

Anza sasa! Andika majina ya watu wawili au watatu ambao ungependa kuwaiga—watu ambao unawaheshimu. Je, kuna yeyote kati yao anayeweza kukusaidia na kazi zako za shule?

[Maelezo ya Chini]

a Kaka au dada yako mkubwa anaweza kukusaidia pia.

[Sanduku katika ukurasa wa 5]

“Mwalimu niliyempenda zaidi”

“Mwalimu niliyempenda zaidi alikuwa mkali sana, lakini kila mtu alimheshimu. Alikuwa mchangamfu. Alizungumza huku akitoa ishara na kutembea kutoka upande mmoja wa darasa hadi mwingine. Aliwahusisha wanafunzi wote katika mazungumzo ya darasani. Ikiwa mwanafunzi hakuelewa jambo fulani, alilieleza kwa subira hadi alipolielewa kabisa. Mara kwa mara alituambia kwamba yuko tayari kujibu maswali yetu. Alisema kwamba maswali hayangemsaidia tu kujua mambo ambayo hatukuelewa bali pia yangemsaidia kuwa mwalimu bora. Alipendezwa kibinafsi na kila mwanafunzi. Wanafunzi wengi waliamua kusomea uhasibu​—somo alililofundisha—​baada ya kuwa katika darasa lake kwa mwaka mmoja tu!”​—Alana, Australia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki