Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 11/12 kur. 5-6
  • 2 Jifunze Kuwasiliana Vizuri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 2 Jifunze Kuwasiliana Vizuri
  • Amkeni!—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Wazazi Na Watoto—wasilianeni Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Mzazi Mmoja, Matatizo Mengi
    Amkeni!—2002
  • Familia za Mzazi Mmoja Zaweza Kufanikiwa!
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Kuendelea Kupashana Habari
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2012
g 11/12 kur. 5-6

2 Jifunze Kuwasiliana Vizuri

[Picha katika ukurasa wa 5]

Jaribu kuwa tayari kumsikiliza mtoto wako anapokuwa tayari kuzungumza

“Nimejifunza kusikiliza kwa makini sana. Haidhuru nimechoka kiasi gani.”​—MIRANDA, AFRIKA KUSINI.

Tatizo.

“Tatizo langu,” anasema Cristina, “si tu kupata wakati wa kuwa pamoja na binti yangu, bali pia ni kujihusisha kabisa kiakili na kihisia licha ya uchovu na majukumu yangu mengi.”

Mapendekezo.

Fanya iwe rahisi kwa watoto kuzungumza nawe kwa uhuru. “Mimi hujaribu kuwawekea watoto wangu mfano mzuri,” anasema Elizabeth, mama ya watoto watano, “na watoto wangu hujihisi huru kuzungumza nami. Mimi pia huwatia moyo wazungumze pamoja na pia wasiende kulala wakiwa wamekasirikiana. Isitoshe, wanajua kwamba siwezi kuvumilia tabia ya kunyamaziana.”

Usiwapuuze watoto wako wanapoongea. “Mwana wangu alipokuwa mchanga,” anaandika Lyanne, “alikuwa akizungumza kama kasuku na nilimpuuza mara nyingi. Kisha alipokuwa tineja, aliacha kuzungumza, nami nikatambua kwamba nilikuwa nimefanya kosa kubwa kumpuuza awali. Nilifanya kazi ngumu, ngumu sana, ya kumlazimisha azungumze nami. Nilizungumza na mzee fulani katika kutaniko letu kuhusu jambo hilo. Alinishauri nitulie na nizungumze na mwana wangu pole kwa pole. Nilifuata shauri lake, na pole kwa pole mambo yakaanza kubadilika.”

Uwe na subira. Andiko la Mhubiri 3:7 linasema kuna “wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema.” Dulce, mama ya watoto watatu anasema, “Wakati watoto wangu walipokataa kuzungumza, niliwaambia kwamba niko tayari kuwasikiliza watakapokuwa tayari kuzungumza.” Badala ya kuwalazimisha watoto wazungumze, kwa subira, waache wajihisi huru kufanya hivyo. Hivyo ndivyo Biblia inavyopendekeza. “Fikra za mtu zimefichika kama kilindi cha maji; lakini mtu mwenye busara ajua kuzichota humo.”​—Methali 20:5, Biblia Habari Njema.

Uwe “mwepesi kuhusu kusikia, si mwepesi wa kusema.” (Yakobo 1:19) Lizaan, aliyenukuliwa katika makala iliyotangulia, anasema hivi: “Nilijifunza kudhibiti ulimi wangu watoto waliponieleza matatizo yao. Pia ilinibidi nijizuie kutoa mashauri haraka-haraka bali nizungumze kwa utulivu niliposhughulikia mambo yanayowasumbua.” Leasa, mama ya wavulana wawili, anaandika hivi: “Haijawa rahisi kwangu kuwa msikilizaji mzuri. Nyakati nyingine hata niliyaona matatizo ya wana wangu kuwa ya kipuuzi, kwa hiyo ilinibidi nijifunze kuonyesha fadhili zaidi.”

“Maneno yenu na yawe yenye neema sikuzote.” (Wakolosai 4:6) “Ili nisizuie mazungumzo,” anasema Lyanne, “nimejitahidi sana kuwa mtulivu hata wakati ambapo mambo mazito yanatokea.”

Ikiwa hutajitahidi kuwa mtulivu, huenda ukapandwa na hasira na kufoka, na hilo litafanya mambo yawe mabaya hata zaidi! (Waefeso 4:31) Kwa mfano, kumfokea mtoto kunaweza kukatiza mawasiliano na kutokeza matatizo zaidi.

Wajue watoto wako. “Wana wangu wawili wanatofautiana kabisa,” anasema Yasmin, aliyenukuliwa hapo awali. “Mmoja ni mzungumzaji; na yule mwingine ni mnyamavu. Ninaposhughulika na yule mnyamavu, nimejifunza kwamba ni afadhali nisimwulize jambo moja kwa moja. Badala yake, mimi huzungumza naye tunapokuwa tukifanya jambo fulani pamoja kama vile kucheza mchezo fulani, au anapozungumza kuhusu jambo linalompendeza. Tunapofanya mambo pamoja, kwa busara mimi humwuliza maoni yake kuhusu jambo fulani.”

Namna gani ikiwa mvulana hajihisi huru kuzungumza na mama yake kuhusu mambo fulani ya kibinafsi, kama vile alivyohisi mwana anayebalehe wa Misao? Kijana huyo alisema, “Wewe hunielewi hata kidogo.” Mama huyo alitafuta msaada kutoka kwa mwanamume mkomavu, anayetegemeka katika kutaniko lake. Misao anasema hivi: “Mwanamume huyo amekuwa mshauri wa mwana wangu, na sasa mwana wangu ana moyo mtulivu.”

Usisahau kwamba wewe ni mzazi, si rafiki tu. “Nilimfanya binti yangu tineja kuwa msiri wangu,” anasema Iwona, mama ya watoto wawili. “Ingawa nilijua si sawa kufanya hivyo, nilifanya kosa hilo na ilibidi nirekebishe hali hiyo.” Ingawa unataka kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na mtoto wako, kumbuka kwamba wewe ukiwa mzazi, wewe ndiye uliye na mamlaka. Unapodumisha hadhi yako na kuonyesha ukomavu na uimara, unafanya iwe rahisi kwa watoto wako kukuheshimu na kutii amri hii ya Biblia: “Enyi watoto, watiini wazazi wenu.”​—Waefeso 6:1, 2.

‘Wapende watoto wako.’ (Tito 2:4) Watoto wanahitaji upendo kama vile tu wanavyohitaji chakula na kinywaji! Kwa hiyo, kila mara, kwa maneno na matendo, wahakikishie kwamba unawapenda! Ukifanya hivyo, watajihisi wakiwa salama na pia watakuwa tayari kuzungumza nawe na kukutii.

Je, Unaweza Kumsaidia Mzazi Asiye na Mwenzi?

Maki, mama asiye na mwenzi na mwenye watoto wawili anaandika hivi: “Ninaporudi nyumbani nikiwa mchovu sana na kujihisi siwezi kufanya chochote, nyakati nyingine mimi hupata chakula na kadi mlangoni. Kadi moja ilisema hivi, ‘Karibu nyumbani. Pole kwa uchovu.’ Nilitiririkwa na machozi, na kumshukuru Mungu.” Ikiwa unamjua mzazi asiye na mwenzi ambaye anajitahidi sana kuwalea watoto wake, mbona usimpongeze kwa jitihada zake na ujitolee kumsaidia ukiweza? Kwa mfano, mara kwa mara, jitolee kuwatunza watoto wake au kuwapeleka shuleni.

Mara nyingi, wazazi wasio na wenzi hujihisi wapweke. Kwa hiyo, unaweza kualika familia yenye mzazi mmoja kwa mlo au kwa tafrija pamoja na familia yako. Familia zenye mzazi mmoja huhitaji kujaza pengo fulani, na huenda ukajaza pengo hilo. Pia watoto wa familia iliyo na mama asiye na mwenzi wanaweza kufaidika na mfano mzuri wa baba wa familia nyingine.

Mbona usiandike orodha ya majina ya familia zenye mzazi mmoja unazojua na mjadiliane na familia yako kuhusu jinsi mnavyoweza kuzisaidia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki