Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 11/12 uku. 8
  • 4 Weka Mipaka Iliyo Wazi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 4 Weka Mipaka Iliyo Wazi
  • Amkeni!—2012
  • Habari Zinazolingana
  • Wasaidie Watoto Wako Wasitawi
    Amkeni!—1997
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Ubora wa Kutia Adabu katika Upendo
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Unawezaje Kuwatia Nidhamu Watoto Wako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2012
g 11/12 uku. 8

4 Weka Mipaka Iliyo Wazi

[Picha katika ukurasa wa 8]

Uwe thabiti, na usiwe kigeugeu

“Kulea watoto ukiwa peke yako si jambo rahisi​—hasa wanapofikia umri wa kubalehe na kutaka kuasi wazazi wao kama vijana wengine wengi.”​—DULCE, AFRIKA KUSINI.

Tatizo.

Biblia ilitabiri kwamba “katika siku za mwisho,” watoto kwa ujumla wangekuwa “wasiotii wazazi.”​—2 Timotheo 3:1, 2.

Mapendekezo.

Tambua kwamba “ili wakue vizuri, watoto wanahitaji kujua sheria na matarajio ya wazazi.” (The Single Parent Resource, cha Brook Noel) Barry G. Ginsberg ambaye ni mwanasaikolojia wa watoto na familia anasema hivi: “Mahusiano huwa mazuri na yasiyo na mkazo kunapokuwa na mipaka iliyo wazi.” Aliongezea hivi: “Mipaka hiyo inapokuwa ya wazi na inapoeleweka vizuri, inakuwa rahisi kufanya familia iwe na furaha.” Unaweza kuwekaje mipaka iliyo wazi?

Uwe thabiti. Uchunguzi mmoja uliofanywa nchini Australia ulionyesha kwamba watoto huwa watundu wazazi wao wanaposhindwa kuwakataza jambo fulani na wanapowaruhusu wafanye watakavyo. Kama Biblia inavyosema: “Mvulana [au msichana] aliyeachiliwa atamletea mama yake aibu.”​—Methali 29:15.

Usiache hisia za hatia kuhusu hali yako ukiwa mzazi mmoja zikufanye uwaendekeze watoto wako. Yasmin, aliyenukuliwa hapo awali anasema: “Nyakati nyingine, mimi huanza kuwahurumia wana wangu wawili kwa sababu wanalelewa na mzazi mmoja.” Lakini kama tutakavyoona, hakuruhusu hisia hizo, ambazo hazikuwa na ubaya wowote, zimfanye abatilishe uamuzi wake.

Usibadili-badili sheria, na usiwe kigeugeu. (Mathayo 5:37) “Watoto wanapojua kwamba bila shaka watatiwa nidhamu kwa sababu ya tabia fulani isiyofaa, hilo litawazuia wasiwe na matatizo ya kihisia na tabia zisizofaa,” linasema jarida American Journal of Orthopsychiatry. Yasmin anasema: “Niliketi pamoja na wavulana wangu na tukazungumza kuhusu nidhamu. Wakifanya makosa, ninajaribu kutoa nidhamu bila kubadilika-badilika. Hata hivyo, nimejifunza kwanza kuwasikiliza na kisha kuwaeleza kwa utulivu jinsi ambavyo jambo walilofanya limeathiri familia yetu. Baada ya kufanya hivyo, mimi hutoa nidhamu kama nilivyosema.”

Uwe na usawaziko; usitoe nidhamu ukiwa na hasira. Ingawa unahitaji kuwa thabiti kwa lililo sawa, unahitaji pia kubadilikana kulingana na hali inapohitajika. “Hekima inayotoka juu”​—yaani, kutoka kwa Mungu—​ni “yenye usawaziko,” linasema andiko la Yakobo 3:17. Watu wenye usawaziko hawafanyi mambo bila kufikiri au kwa hasira. Wala hawashikilii sheria kupita kiasi. Badala yake, wao hufikiri kwanza, huenda hata wakasali kuhusu jambo hilo, kisha wanaweza kutenda kwa utulivu na kwa njia inayofaa.

Kutobadili-badili sheria, kuwa thabiti, na kuwa na usawaziko, pamoja na kuweka mfano mzuri, kutakusaidia kuweka mipaka ambayo itafanya nyumba yako iwe kimbilio la kweli kwa ajili ya watoto wako.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki