Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 12/13 uku. 3
  • Kuutazama Ulimwengu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuutazama Ulimwengu
  • Amkeni!—2013
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Marekani
  • Nigeria
  • Hispania
  • ULIMWENGU
  • Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawatumii Msalaba Katika Ibada?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Je, Kweli Yesu Alikufa Juu ya Msalaba?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Je! Msalaba Ni kwa Ajili ya Wakristo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Kwa Nini Wakristo wa Kweli Hawatumii Msalaba Katika Ibada?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2013
g 12/13 uku. 3

Kuutazama Ulimwengu

Marekani

Uchunguzi mmoja ulionyesha kwamba asilimia 33 hivi ya watu waliokuwa wakitembea kwa miguu walikengeushwa walipokuwa wakivuka barabara zenye shughuli nyingi—kwa sababu walikuwa wakisikiliza muziki, wakiongea kwenye simu na kufanya mambo mengine. Kikengeusha fikira hatari zaidi kilikuwa ni kutuma ujumbe mfupi. Watu waliokuwa wakituma ujumbe walichukua muda mrefu zaidi kuvuka barabara, wengi wao hawakutii taa za barabarani, walivukia mahali pasipofaa, au bila kuangalia pande zote mbili za barabara.

Nigeria

Wanawake kutoka Nigeria wanaosafirishwa Ulaya na watu wanaofanya biashara ya kuuza watu hulazimishwa kula kiapo cha kutunza siri katika mahekalu ya wachawi. Ili kuwadhibiti wanawake hao na kuhakikisha kwamba wanatii wakiwa watumwa wa ngono, wafanya-biashara hao huwatisha kwamba wataadhibiwa na roho waovu.

Hispania

Kati ya asilimia 5 na 10 ya watu ambao wamekaa muda mrefu bila kuajiriwa huondoa habari kuhusu shahada za chuo kikuu na habari za ujuzi wao wanapotuma maombi ya kazi kwa sababu habari hizo zinawafanya waonekane wanastahili mshahara mkubwa kuliko kazi wanayotafuta.

ULIMWENGU

Moshi unaotokezwa na majiko ya kuni au mkaa unaonwa kuwa ndio kisababishi kikubwa cha vifo katika nchi zinazoendelea. Katika nchi hizo, watu milioni nne hufa kila mwaka kutokana na magonjwa ya mfumo wa kupumua yanayosababishwa na moshi. Watafiti wanasema kwamba kemikali zenye sumu zinazotolewa na majiko hayo ni hatari kama sumu iliyo katika moshi wa sigara.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki