Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 2/15 uku. 3
  • Je, Biblia Ina Faida Leo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Biblia Ina Faida Leo?
  • Amkeni!—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Ushauri wa Biblia Unaweza Kutumika Leo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
  • Kufurahisha Mioyo ya Wazazi Wako
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Maadili Yanayoboresha Maisha
    Amkeni!—2013
  • Utangulizi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2015
g 2/15 uku. 3
Biblia iliyofunguliwa

HABARI KUU

Je, Biblia Ina Faida Leo?

‘Kwa mara ya kwanza maishani mwangu, nilipata furaha.’

HILTON alipenda mchezo wa ndondi. Akiwa na umri wa miaka saba alikuwa akipigana na watu si tu kwenye jukwaa la ndondi bali pia mitaani. Alipojiunga na shule ya upili (sekondari) yeye na rafiki zake walizurura wakitafuta mtu wa kumpiga. Anasimulia hivi: “Nilikuwa mwizi, nilicheza kamari, niliwanyanyasa wanawake, nilitazama ponografia, na kuwatukana wazazi wangu. Tabia yangu iliharibika hivi kwamba wazazi wangu walifikiri nisingeweza kubadilika. Baada ya kumaliza shule ya upili, niliondoka nyumbani.”

Aliporudi nyumbani baada ya miaka 12, wazazi wake hawakuamini macho yao! Hilton alikuwa mtulivu, mpole, na mwenye heshima. Ni nini kilichomfanya abadilike? Alipokuwa mbali na nyumbani, alitafakari sana kuhusu maisha yake. Pia, alianza kuichunguza Biblia ili imsaidie kubadilisha mwenendo wake. Anasema hivi: “Nilitumia mambo niliyojifunza katika Biblia. Mambo hayo yalitia ndani kuuvua utu wangu wa zamani na kutii amri inayopatikana kwenye andiko la Waefeso 6:2, 3 linalosema kwamba ninapaswa kuwatii wazazi wangu. Kwa mara ya kwanza maishani mwangu, nilipata furaha ya kweli na kuwafurahisha wazazi wangu.”

Simulizi la Hilton linaonyesha jinsi Biblia ilivyo na nguvu ya kumbadili mtu na jinsi viwango vyake vilivyo na faida. (Waebrania 4:12) Acheni tuchunguze baadhi ya viwango hivyo, kama vile: unyoofu, kujizuia, uaminifu, na upendo—na tuone jinsi vinavyoweza kuboresha maisha yetu.

JE, NI KITABU KILICHOPITWA NA WAKATI?

Kompyuta iliyopitwa na wakati ikiwa imetupwa kwenye pipa la takataka

Watu wengine husema kwamba Biblia imepitwa na wakati. Wanafananisha Biblia na mwongozo wa kompyuta ambao umepitwa na wakati. Lakini jambo hilo si kweli. Muundo wa kompyuta hubadilika na kusababisha mwongozo wake kupitwa na wakati. Hata hivyo, tabia za asili za wanadamu hazibadiliki. Kwa mfano, leo watu hupendana au kuchukiana, huaminiana au kusalitiana, hutendeana kwa fadhili au kwa ukatili kama tu ilivyokuwa katika enzi za mababu zetu. Kwa hiyo inapohusu mambo ya msingi ya wanadamu, “hakuna jambo jipya chini ya jua.”—Mhubiri 1:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki