Watu wengi wameruhusu bila kutambua mahusiano yao yaharibike, kwa sababu ya mahangaiko yanayosababishwa na hali za ulimwengu zinazozidi kuwa mbaya.
Watu wamejitenga na marafiki zao.
Wenzi wa ndoa hawatendeani kwa fadhili.
Wazazi hawajali mahangaiko ya watoto wao.
Unachopaswa Kujua
Ni muhimu kuwa na marafiki kwa sababu watakusaidia kuwa na afya njema ya kimwili na kihisia hasa unapokabili hali ngumu.
Mkazo unaoletwa na hali mbaya za ulimwengu, unaweza kusababisha matatizo katika familia yako katika njia zisizotarajiwa.
Taarifa za habari zinazoshtua, zinaweza kuwaathiri watoto wako kwa kiasi kikubwa kuliko unavyoweza kutarajia.
Unachoweza Kufanya Sasa
Biblia inasema hivi: “Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote naye ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.”—Methali 17:17.
Mfikirie mtu ambaye anaweza kukusaidia na kukupa ushauri unaofaa. Kuwa na marafiki wanaokujali, kutakusaidia kupata nguvu za kuvumilia changamoto za kila siku.