Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g22 Na. 1 kur. 13-15
  • 4 | Linda Tumaini Lako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 4 | Linda Tumaini Lako
  • Amkeni!—2022
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KWA NINI NI MUHIMU?
  • Unachopaswa Kujua
  • Unachoweza Kufanya Sasa
  • Biblia Inatoa Tumaini la Kweli
  • Ninaweza Kupata Wapi Tumaini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Biblia Inatupatia Tumaini
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Biblia Inatupatia Tumaini
    Furahia Maisha Milele—Masomo ya Kwanza ya Biblia
  • Kupata Tumaini Mwaka wa 2024​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2022
g22 Na. 1 kur. 13-15
Biblia iliyofunguliwa ikiwa karibu na chupa yenye maua.

ULIMWENGU WENYE MISUKOSUKO

4 | Linda Tumaini Lako

KWA NINI NI MUHIMU?

Mahangaiko kuhusu matatizo ya ulimwengu leo, yanaweza kuwaathiri watu kimwili na kihisia. Watu wengi walioathiriwa na matatizo hayo, hawana tumaini kwamba mambo yatakuwa sawa wakati ujao. Wanatendaje?

  • Baadhi yao hata wamekataa kufikiria kuhusu wakati ujao.

  • Wengine hutumia kileo au dawa za kulevya ili kuepuka kufikiria kuhusu matatizo yao.

  • Baadhi ya watu wamefikia mkataa kwamba ni afadhali wafe kuliko kuwa hai. Hata wamesema kwamba hakuna faida ya kuishi.

Unachopaswa Kujua

  • Huenda baadhi ya matatizo unayokabili ni ya muda mfupi na mambo yanaweza kuwa bora bila wewe kutarajia.

  • Hata kama hali yako haitabadilika, unaweza kufanya mambo yatakayokusaidia kukabiliana na hali hiyo.

  • Biblia inaahidi suluhisho la kudumu la matatizo ya wanadamu.

Unachoweza Kufanya Sasa

Biblia inasema hivi: “Msihangaike kamwe kuhusu kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe. Kila siku ina matatizo yake ya kutosha.”​—Mathayo 6:34.

Shughulikia matatizo ya leo. Usiruhusu mahangaiko ya kesho yakuzuie kutimiza majukumu yako ya leo.

Kuhofia mambo mabaya ambayo huenda yakatokea wakati ujao, kutakuongezea mkazo na kudhoofisha tumaini lako kwamba mambo yatakuwa mazuri wakati ujao.

JINSI YA KUKABILIANA NA HALI​—Madokezo Yanayofaa

KAZIA FIKIRA MAMBO MAZURI

Mwanamke akitafakari huku akitazama nje ya dirisha.

Biblia inasema hivi: “Siku zote za mtu anayeteseka ni mbaya, lakini mtu aliye na moyo mchangamfu huwa na karamu daima.” (Methali 15:15) Mtazamo usiofaa unaweza kukufanya usione suluhisho la tatizo lako, lakini mtazamo mzuri utakusaidia kufikiria njia za kukabiliana nalo.

  • Punguza wakati na kiasi cha habari unazosikiliza.

  • Mwishoni mwa kila siku, orodhesha mambo mawili au matatu ambayo ungependa kushukuru kuyahusu.

  • Panga kazi utakazofanya siku hiyo. Ikiwa una kazi kubwa ya kufanya, igawe katika sehemu ndogondogo ili iwe rahisi kuona matokeo ya jitihada zako mwishoni mwa siku.

OMBA MSAADA

Mwanamume mwenye umri mkubwa akimtia moyo kijana.

Biblia inasema hivi: “Anayejitenga na wengine. . . hukataa hekima yote inayotumika.” (Methali 18:1) Huwezi kutoka ndani ya shimo refu bila msaada wa watu wengine

  • Omba msaada kutoka kwa watu wa familia au marafiki.

  • Pia, tafuta njia ambazo wewe unaweza kuzitumia ili kuwasaidia. Kuwasaidia wengine kutakusaidia uwe na maoni yenye usawaziko kuhusu matatizo yako.

  • Ikiwa umekata tamaa au unahisi kwamba uhai hauna thamani, nenda kamwone daktari. Mara nyingine, kulemewa na hisia ni dalili ya ugonjwa kama vile kushuka moyo. Watu wengi wamepata nafuu baada ya kutibiwa.a

a Gazeti la Amkeni! halipendekezi matibabu fulani hususa.

Biblia Inatoa Tumaini la Kweli

Zamani, mtunga-zaburi alisali hivi kwa Mungu: “Neno lako ni taa ya mguu wangu, na nuru ya njia yangu.” (Zaburi 119:105) Ona jinsi Neno la Mungu, Biblia, lilivyo kama taa:

Taa hutusaidia kutambua mahali pa kukanyaga tunapotembea usiku. Vivyo hivyo, Biblia ina ushauri wenye hekima unaoweza kutuongoza tunapohitaji kufanya uamuzi mgumu.

Taa inaweza kutusaidia kujua njia tunayopita ili tuweze kuona kilicho mbele yetu. Kwa njia hiyohiyo, Biblia inaweza kutusaidia kuona mambo yatakayotokea wakati ujao.

Biblia ni kitabu kitakatifu kinachoelezea historia ya wanadamu na kutoa tumaini la kweli la wakati ujao. Inajibu maswali yafuatayo:

Jinsi gani?

Jinsi kuteseka kulivyoanza: Biblia inasema kwamba “kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, basi kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.”​—Waroma 5:12.

Kwa nini?

Kwa nini utawala wa wanadamu umeshindwa kutatua matatizo yetu? Biblia inasema kwamba “mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Matatizo yaliyopo ulimwenguni leo yanathibitisha ukweli wa andiko hilo.

Jambo litakalofanyika

Mungu atafanya nini ili kurekebisha hali hiyo? Biblia inaonyesha kwamba “atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”​—Ufunuo 21:4.

Sehemu ya video yenye kichwa, “Kwa Nini Ujifunze Biblia?” Mke akimweleza mume wake jambo alilosoma kwenye Biblia.

JIFUNZE MENGI ZAIDI. Tazama video yenye kichwa, Kwa Nini Ujifunze Biblia?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki