Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g24 Na. 1 kur. 13-15
  • Kwa Nini Watu Wengi Hawajiheshimu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Watu Wengi Hawajiheshimu?
  • Amkeni!—2024
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KWA NINI NI MUHIMU KUJIHESHIMU
  • JAMBO UNALOWEZA KUFANYA
  • MAMBO TUNAYOFANYA
  • Unaweza Kupata Msaada
    Amkeni!—2020
  • Kwa Nini Hakuna Heshima Katika Familia?
    Amkeni!—2024
  • Mikutano ya Mashahidi wa Yehova Inaweza Kukunufaishaje?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Nifanye Nini Ili Nijiamini Zaidi?
    Amkeni!—2010
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2024
g24 Na. 1 kur. 13-15
Mwanamke mwenye huzuni akijitazama kwenye kioo.

Kwa Nini Watu Wengi Hawajiheshimu?

KWA NINI NI MUHIMU KUJIHESHIMU

Watu wanaojiheshimu wanaweza kukabiliana kwa ujasiri na changamoto za maisha. Hawakati tamaa kirahisi.

  • Utafiti unaonyesha kwamba, watu wasiojiheshimu huenda wakapatwa na mahangaiko, mshuko moyo, na matatizo ya kutokula chakula vizuri. Huenda pia wakawa waraibu wa pombe na dawa za kulevya.

  • Watu wanaojiheshimu hawajilinganishi na wengine, na hilo hufanya iwe rahisi kwao kuwa na uhusiano mzuri na watu wengine na kupata marafiki wa kudumu. Kwa upande mwingine, watu wasiojiheshimu, mara nyingi wanapenda kukosoa mambo na hilo linaweza kuharibu mahusiano yao na watu.

  • Hata wanapokabili changamoto, watu wanaojiheshimu huendelea kuwa imara; hawaruhusu matatizo yawazuie kufikia lengo lao. Hata hivyo, watu wasiojiheshimu mara nyingi wanaona matatizo madogo kuwa vikwazo vikubwa. Hilo linaweza kuwafanya wakate tamaa kirahisi.

JAMBO UNALOWEZA KUFANYA

Chagua marafiki watakaokusaidia. Fanya urafiki na watu wenye heshima, wanaokujali kikweli, na watakaokutia moyo.

“Rafiki wa kweli hupenda nyakati zote naye ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.”— Methali 17:17.

Wasaidie wengine. Ukiwa mwenye fadhili na uwafanyie wengine mambo mazuri, hata wale ambao hawana cha kukupatia, utapata furaha ya kweli inayotokana na kutoa. Na hata watu wasipotambua mambo mazuri unayofanya, bado utakuwa na furaha.

“Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.”—Matendo 20:35.

Wafundishe watoto wako kujiheshimu. Njia moja ya kufanya hivyo ni kuwapa nafasi ya kusuluhisha matatizo yao wenyewe kadiri wawezavyo. Kufanya hivyo kunawasaidia watoto kujua jinsi ya kupambana na hali ngumu, na kutatua matatizo bila kukata tamaa. Wanapojifunza kufanya hivyo wanajiheshimu si sasa tu, bali hata wanapokuwa watu wazima.

“Mzoeze mtoto njia anayopaswa kuifuata; hata atakapozeeka hataiacha.”—Methali 22:​6, maelezo ya chini.

Shahidi wa Yehova akijifunza Biblia na mwanamke kwenye mgahawa.
Shahidi wa Yehova akijifunza Biblia na mwanamke kwenye mgahawa.

MAMBO TUNAYOFANYA

Mikutano ya Mashahidi wa Yehova pamoja na programu yao ya kujifunza Biblia inaweza kuwasaidia watu waboreshe maisha yao na kujiheshimu zaidi.

MIKUTANO YETU YA KILA JUMA

Katika mikutano yetu ya kila juma tunafurahia kusikiliza hotuba zinazotegemea Biblia. Hotuba hizo zina madokezo mazuri yanayotusaidia kujiheshimu. Hakuna kiingilio kinachotozwa kwenye mikutano yetu na watu wote wanakaribishwa. Kwa mfano, kwenye mikutano yetu utajifunza . . .

  • kwa nini sisi ni wenye thamani kwa Mungu

  • jinsi ya kupata kusudi la kweli maishani

  • jinsi ya kusitawisha urafiki imara na unaodumu

Utapata pia marafiki ‘wanaotunzana.’—1 Wakorintho 12:​25, 26.

Ili kujua mengi kuhusu mikutano yetu, tafuta video fupi yenye kichwa Ni Nini Hutendeka Katika Jumba la Ufalme? kwenye jw.org/sw.

MASOMO YA BIBLIA

Tunakualika ujifunze Biblia pamoja na mwalimu kupitia kitabu Furahia Maisha Milele! Kitabu hicho cha kujifunzia kina maandiko muhimu, maswali yanayofaa, video zenye kuchochea, picha maridadi, na kinatoa sababu zilizo wazi. Masomo yetu ya Biblia yanawasaidia watu kujiheshimu na kuboresha maisha yao.

Ili kuona jinsi kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova kunavyoweza kukunufaisha tafuta video fupi yenye kichwa Kwa Nini Ujifunze Biblia? kwenye jw.org/sw.

Israel Martínez.

JIFUNZE MENGI ZAIDI

Israel Martínez alijiona kuwa duni kwa sababu hakuwa na pesa na hakuwa na elimu kubwa. Tafuta makala “Sasa Sioni Aibu Tena” kwenye jw.org/sw ili kujua jinsi kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova na kujifunza Biblia pamoja nao kulivyomsaidia ajiheshimu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki