Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rr uku. 220
  • “Mchango Mtakaoweka Kando”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mchango Mtakaoweka Kando”
  • Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • A. “Mchango”
  • B. “Mchango Mzima”
  • C. “Eneo la Kiongozi”
  • D. “Mchango Mtakatifu”
  • “Eneo Linalobaki”
  • EZE. 45:6; 48:15-19
  • Furaha ya Kibinadamu Chini ya Serikali ya Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • “Jina la Jiji Hilo . . . Litakuwa, Yehova Yupo Hapo”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Lile “Hekalu” na Yule “Mkuu” Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kitabu Cha Biblia Namba 28—Ezekieli
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
Pata Habari Zaidi
Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
rr uku. 220

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 21A

“Mchango Mtakaoweka Kando”

Ezekieli 48:8

Acheni tujiunge na Ezekieli anapochunguza kwa undani eneo ambalo Yehova aliliweka kando. Lina sehemu tano. Ni sehemu gani hizo? Na zinatimiza kusudi gani?

Ramani ya nchi ambayo Yehova aliliweka kando na kuliita ‘mchango’ na ramani ndogo iliyo ndani inaonyesha eneo la mraba la nchi hiyo lenye upana wa mikono 25,000 (kilomita 13) kutoka kaskazini hadi kusini na mikono 25,000 kutoka mashariki hadi magharibi. Eneo hilo la mraba la nchi hiyo linaitwa ‘mchango mzima’ na limegawanywa katika sehemu tatu zilizo sambamba, ambazo ni sehemu ya juu, sehemu ya katikati iliyo na hekalu, na sehemu ya chini lenye jiji linaloitwa ‘Yehova Yupo Hapo.’

A. “Mchango”

Ni eneo kwa ajili ya utawala na linaitwa “eneo la usimamizi.”

EZE. 48:8

B. “Mchango Mzima”

Ni sehemu iliyowekwa kando kwa ajili ya makuhani, Walawi, na jiji. Pia, watu kutoka makabila yote 12 wanaingia kwenye sehemu hii ili kumwabudu Yehova na kuunga mkono mpango wa usimamizi.

EZE. 48:20

C. “Eneo la Kiongozi”

“Ardhi hii itakuwa mali yake katika Israeli.” “Itakuwa mali ya kiongozi.”

EZE. 45:7, 8; 48:21, 22

D. “Mchango Mtakatifu”

Eneo hili linafafanuliwa pia kuwa “sehemu takatifu.” Sehemu ya juu ni kwa ajili ya “Walawi.” Ni “kitu kitakatifu.” Sehemu ya katikati ni “mchango mtakatifu kwa ajili ya makuhani.” Ni “mahali kwa ajili ya nyumba zao, na mahali patakatifu kwa ajili ya patakatifu,” au hekalu.

EZE. 45:1-5; 48:9-14

“Eneo Linalobaki”

Litakuwa la “watu wote wa nyumba ya Israeli” na “litakuwa la matumizi ya kawaida ya jiji, kwa ajili ya makao na malisho.”

EZE. 45:6; 48:15-19

Angalia sura ya 21, fungu la 3

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki