Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 27
  • Kifo cha Yesu Kinawezaje Kutuokoa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kifo cha Yesu Kinawezaje Kutuokoa?
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Fidia​—Zawadi Bora Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Fidia—Zawadi Bora Zaidi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Fidia ya Kristo Njia ya Mungu ya Wokovu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kifo cha Yesu Kina Maana Gani Kwetu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 27
Somo la 27. Mwili wa Yesu unashushwa kutoka kwenye mti.

SOMO LA 27

Kifo cha Yesu Kinawezaje Kutuokoa?

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Sisi hutenda dhambi, tunateseka, na tunakufa kwa sababu wanadamu wa kwanza Adamu na Hawa hawakumtii Mungu.a Lakini tuna tumaini. Yehova ameandaa njia ya kutuweka huru kutoka kwenye laana ya dhambi na kifo kupitia Mwana wake, Yesu Kristo. Biblia inafundisha kwamba Yesu alitoa fidia kupitia kifo chake. Fidia ni malipo yanayotolewa ili kumweka mtu huru. Yesu alilipa fidia kwa kutoa uhai wake mkamilifu wa kibinadamu. (Soma Mathayo 20:28.) Yesu alipodhabihu kwa hiari haki yake ya kuishi milele duniani, alitufungulia njia ya kupata tena uhai mkamilifu ambao Adamu na Hawa walipoteza. Pia, Yesu alionyesha kwamba yeye na Yehova wanatupenda sana. Somo hili litakusaidia kuthamini zaidi kifo cha Yesu.

1. Kifo cha Yesu kinaweza kutunufaishaje leo?

Kwa kuwa sisi ni watenda dhambi, tunafanya mambo mengi yasiyompendeza Yehova. Hata hivyo, ikiwa tunajuta sana kwa sababu ya dhambi tulizofanya na kumwomba Yehova kupitia Yesu Kristo atusamehe na kujitahidi kabisa kutorudia makosa hayo, tunaweza kufurahia urafiki wa karibu pamoja na Mungu. (1 Yohana 2:1) Biblia inasema hivi: “Kristo alikufa mara moja kwa wakati wote kwa ajili ya dhambi, mtu mwadilifu kwa ajili ya wasio waadilifu, ili awaongoze ninyi kwa Mungu.”​—1 Petro 3:18.

2. Kifo cha Yesu kitatunufaishaje wakati ujao?

Yehova alimtuma Yesu atoe uhai wake mkamilifu wa kibinadamu “ili kila mtu anayemwamini [Yesu] asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Kupitia dhabihu ya Yesu, Yehova ataondoa madhara yote yaliyosababishwa na Adamu alipokosa kutii. Hilo linamaanisha kwamba tukionyesha imani katika dhabihu ya Yesu, tutapata nafasi ya kufurahia maisha milele katika dunia paradiso!​—Isaya 65:21-23.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze mengi kuhusu sababu iliyofanya Yesu atoe uhai wake, na uchunguze jinsi unavyoweza kunufaika.

3. Kifo cha Yesu kinatuweka huru kutoka kwenye dhambi na kifo

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

VIDEO: Kwa Nini Yesu Alikufa?​—Sehemu ya 1 (2:01)

  • Adamu alipoteza fursa gani alipokosa kumtii Mungu?

Soma Waroma 5:12, kisha mzungumzie swali hili:

  • Dhambi ambayo Adamu alifanya imeathirije maisha yako?

Soma Yohana 3:16, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kwa nini Yehova alimtuma Mwana wake duniani?

A. Picha: 1. Adamu baada ya kukosa kumtii Mungu. 2. Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza. Picha: A. Adamu baada ya kukosa kumtii Mungu. B. Yesu Kristo. B. Picha: 1. Yesu Kristo. 2. Watu wa umri, jamii, tamaduni, na malezi mbalimbali.
  1. Adamu alikuwa mwanamume mkamilifu aliyekosa kumtii Mungu na hivyo akawasababishia wanadamu wote dhambi na kifo

  2. Yesu alikuwa mwanamume mkamilifu aliyemtii Mungu na kuwafungulia wanadamu njia ya kuwa wakamilifu na kupata uzima wa milele

4. Kifo cha Yesu kinaweza kuwanufaisha watu wote

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

VIDEO: Kwa Nini Yesu Alikufa?​—Sehemu ya 2 (2:00)

  • Kifo cha mtu mmoja kingewezaje kuwanufaisha watu wote?

Soma 1 Timotheo 2:5, 6, kisha mzungumzie swali hili:

  • Adamu alikuwa mwanadamu mkamilifu ambaye aliwasababishia wanadamu wote dhambi na kifo. Yesu pia alikuwa mwanadamu mkamilifu. Yesu alitoa jinsi gani “fidia inayolingana” na uhai ambao Adamu alipoteza?

5. Fidia ni zawadi ambayo Yehova amekupatia

Rafiki za Yehova huona fidia kuwa zawadi waliyopewa kibinafsi. Kwa mfano, soma Wagalatia 2:20, kisha mzungumzie swali hili:

  • Mtume Paulo alionyeshaje kwamba aliona fidia kuwa zawadi aliyopewa kibinafsi?

Adamu alipotenda dhambi, yeye na wazao wake wote walihukumiwa kifo. Lakini Yehova alimtuma Mwana wake afe, ili wewe upate nafasi ya kuishi milele.

Unaposoma mistari ifuatayo, wazia jinsi Yehova alivyohisi alipomwona Mwana wake akiteseka. Soma Yohana 19:1-7, 16-18, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unahisije kuhusu jambo ambalo Yehova na Yesu wamekufanyia?

HUENDA MTU AKAULIZA: “Inawezekanaje mtu mmoja afe kwa ajili ya watu wote?”

  • Wewe ungejibuje swali hilo?

MUHTASARI

Kupitia kifo cha Yesu, Yehova anaweza kutusamehe dhambi zetu, na tunapata fursa ya kuishi milele.

Ungejibuje?

  • Kwa nini Yesu alikufa?

  • Ni kwa njia gani uhai mkamilifu wa Yesu ulikuwa fidia inayolingana?

  • Kifo cha Yesu kinawezaje kukunufaisha?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze kwa nini uhai mkamilifu wa Yesu unaitwa fidia.

“Ni kwa Njia Gani Dhabihu ya Yesu Ilikuwa ‘Fidia kwa Ajili ya Wengi’?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Chunguza mambo tunayopaswa kufanya ili tuokolewe.

“Yesu Huokoa​—Jinsi Gani?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Je, Yehova anaweza kusamehe hata dhambi nzito?

“Majibu ya Maswali ya Biblia” (Mnara wa Mlinzi, Mei 1, 2013)

Ona jinsi kujifunza kuhusu dhabihu ya Kristo kulivyomsaidia mwanamume kubadili utu wake.

“Mimi Si Mtumwa wa Jeuri Tena” (Makala iliyo kwenye mtandao)

a Dhambi haimaanishi tu kufanya jambo baya. Dhambi pia inarejelea madhara ambayo tumerithi kutoka kwa Adamu na Hawa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki