Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • scl kur. 69-74
  • Ndoa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ndoa
  • Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
Maandiko kwa Ajili ya Maisha ya Mkristo
scl kur. 69-74

Ndoa

Mpango wa ndoa ulianzaje?

Mwa 1:​27, 28; 2:​22-24; Mt 19:​4-6

Mkristo anapaswa kumchagua nani awe mwenzi wake wa ndoa?

Kwa nini Mkristo wa kweli hapaswi kukubali mwana au binti yake aliyebatizwa afunge ndoa na mtu ambaye si mtumishi wa Yehova aliyejiweka wakfu na kubatizwa?

1Ko 7:39; 2Ko 6:​14, 15

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 24:​1-4, 7—Abrahamu aliyezeeka anaazimia kumtafutia mke, Isaka, mwana wake, kutoka kwa watu wanaomtumikia Yehova, si kutoka kwa Wakanaani, wanaoabudu miungu mingine

    • Mwa 28:​1-4—Isaka anamwongoza Yakobo, mwana wake, akatafute mke kwa waabudu wenzake, wala si kutoka kwa Wakanaani

Yehova anahisije kuhusu wale wanaofunga ndoa na watu wasiomwabudu?

Kum 7:​3, 4

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Fa 11:​1-6, 9-11—Yehova anamkasirikia Mfalme Sulemani kwa kupuuza onyo kutoka kwake, kwa kuoa wanawake wa kigeni, na kuwaruhusu waupotoshe moyo wake

    • Ne 13:​23-27—Kama Yehova, Gavana Nehemia anakasirika sana Waisraeli wanapooa wanawake wa kigeni ambao hawamtumikii Yehova, hivyo Nehemia anawatia nidhamu na kuwarekebisha

Kwa nini ni jambo la hekima kuchagua mwenzi wa ndoa mwenye sifa nzuri na anayemtumikia Yehova kwa uaminifu?

Met 18:22; 31:​10, 28

Tazama pia Efe 5:​28-31, 33

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • 1Sa 25:​2, 3, 14-17—Nabali ni mwanamume tajiri, lakini ni mkali na mkatili, na hilo linafanya awe mume mbaya kwa Abigaili

    • Met 21:9—Kuchagua mwenzi wa ndoa asiyefaa kunaweza kutufanya tusiwe na furaha na kutunyang’anya amani yetu

    • Ro 7:2—Mtume Paulo anaeleza kwamba mwanamke anapoolewa anakuwa chini ya mamlaka ya kadiri ya mume wake asiye mkamilifu; kwa hiyo mwanamke mwenye hekima anakuwa mwangalifu anapochagua mwenzi wa ndoa

Kujitayarisha kwa ajili ya ndoa

Kwa nini mwanamume anapaswa kujitayarisha kwa ajili ya jukumu la kutegemeza familia kabla ya kufunga ndoa?

1Ti 5:8

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Met 24:27—Kabla mwanamume hajaoa au kupata watoto, anapaswa kufanya kazi kwa bidii ili awe tayari kutegemeza familia

Kwa nini watu wawili wanaochumbiana wanapaswa kukazia fikira kutafuta ushauri wenye hekima na kufahamiana vizuri, badala ya kuangalia tu mwonekano wa nje?

Met 13:10; 1Pe 3:​3-6

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Ru 2:​4-7, 10-12—Boazi anamfahamu zaidi Ruthu kwa kuchunguza mazoea yake ya kufanya kazi, na kwa kuzingatia ripoti zinazotegemeka kuhusu sifa zake, jinsi anavyoshughulika na familia yake, na hali yake ya kiroho

    • Ru 2:​8, 9, 20—Ruthu anamfahamu vizuri Boazi kwa kuchunguza jinsi alivyo mwenye fadhili, mkarimu, na upendo wake kwa Yehova

Kwa nini Yehova anataka tudumishe usafi wa kiadili wakati wa urafiki wa kimapenzi na uchumba?

Gal 5:19; Kol 3:5; 1Th 4:4

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Met 5:​18, 19—Baadhi ya matendo ya kimahaba yanapaswa kufanywa na wenzi wa ndoa tu

    • Wim 1:2; 2:6—Wakati wa uchumba, kijana mchungaji na msichana Mshulami wanaelezana upendo wao kwa njia safi, si kwa maneno machafu ya kimahaba

    • Wim 4:12; 8:​8-10—Msichana Mshulami anadumisha usafi wa kiadili na anaonyesha sifa ya kujizuia; yeye ni kama bustani iliyofungwa

Kwa nini wanaopanga kufunga ndoa wanapaswa kufunga ndoa kisheria?

Mt 22:21; Ro 13:1; Tit 3:1

Majukumu ya waume

Ni majukumu gani mazito aliyopewa mume?

Efe 5:​23, 25, 28-31, 33

Waume wanapaswa kuiga mfano wa nani wanapotimiza jukumu lao la ukichwa?

1Ko 11:3; Efe 5:23

Kwa nini ni muhimu kwa mume kumwonyesha upendo mke wake na kuelewa mahitaji na hisia zake?

Kol 3:19; 1Pe 3:7

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 21:​8-12—Yehova anamwagiza Abrahamu amsikilize Sara, mke wake, hata ingawa mapendekezo ya Sara hayakumpendeza

    • Met 31:​10, 11, 16, 28—Mume mwenye hekima wa mke mwema anayetajwa kwenye mistari hii, hamtawali mke wake au kutafuta makosa yake; bali anamwamini mke wake na kumsifu

    • Efe 5:33—Maneno ya mtume Paulo yaliyoongozwa na roho yanadokeza kwamba mke ana uhitaji wa pekee wa kuhisi kwamba anapendwa na mume wake

Jukumu la mke

Ni jukumu gani la pekee kutoka kwa Yehova ambalo mke Mkristo anatimiza?

Mwa 2:18; Kol 3:18; Tit 2:​4, 5

Je, jukumu la mke linamshushia heshima?

Mwa 1:​26-28, 31; 2:18

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Met 1:8; 1Ko 7:4—Katika ndoa na maisha ya familia, mke na mama wamepewa mamlaka ya kadiri na Mungu

    • 1Ko 11:3—Mtume Paulo anaeleza kwamba kulingana na mpango wa Yehova, sisi sote tupo chini ya ukichwa isipokuwa Mungu Mweza-Yote

    • Ebr 13:​7, 17—Katika kutaniko, wanaume na wanawake wanapaswa kujitiisha na kuwatii wale wanaoongoza

Mke Mkristo ambaye ana mume asiyeamini anawezaje kumfurahisha Yehova?

1Ko 7:​13-16; 1Pe 3:​1, 2

Kwa nini mke Mkristo anapaswa kudumisha mtazamo wa heshima kuelekea mume wake?

Efe 5:33

  • Simulizi la Biblia linalohusika:

    • Mwa 18:12; 1Pe 3:​5, 6—Sara anamheshimu sana mume wake hata katika mawazo yake, akimwona kama “bwana” wake au kichwa cha kiroho

Ni mke wa aina gani anayesifiwa katika Biblia?

Met 19:14; 31:​10, 13-31

  • Masimulizi ya Biblia yanayohusika:

    • Mwa 24:​62-67—Rebeka anamsaidia Isaka, mume wake, kupata faraja baada ya kifo cha mama yake

    • 1Sa 25:​14-24, 32-38—Abigaili anamlinda mume wake mpumbavu na kuokoa nyumba yake kwa kumwomba kwa unyenyekevu Daudi aonyeshe rehema

    • Est 4:​6-17; 5:​1-8; 7:​1-6; 8:​3-6—Malkia Esta anahatarisha uhai wake mara mbili kwa kwenda kwa mume wake, mfalme, bila kuitwa, ili amwombe awalinde watu wa Mungu

Kutatua hali ya kutoelewana

Ni kanuni gani zinazoweza kuwasaidia wenzi wa ndoa kutatua matatizo yanayotokea katika ndoa?

1Ko 13:​4-8; Efe 5:33; Kol 3:​12-14

Ni kanuni gani zinazoweza kuwasaidia wenzi wa ndoa kuwa na maoni yenye usawaziko kuhusu pesa?

Lu 12:15; Flp 4:5; 1Ti 6:​9, 10; Ebr 13:5

Tazama pia “Pesa”

Ni kanuni gani zinazoweza kuwasaidia wenzi wa ndoa kusuluhisha matatizo yanayohusu ndugu wa ukoo na wakwe?

Zb 34:14; Mt 19:​5, 6; 1Ko 13:​4, 5

Ni kanuni gani zinazoweza kuwaongoza wenzi wa ndoa inapohusu mahusiano ya kingono?

Met 5:​15-20; Mt 5:​27, 28; 1Ko 7:​3-5; 10:24; Flp 2:4; Ebr 13:4

Kwa nini ni muhimu kukazia fikira sifa nzuri za mwenzi wako badala ya makosa yake?

Zb 103:14; 130:​3, 4; Met 17:9; 1Pe 4:8

Kwa nini ni muhimu kusuluhisha matatizo mapema na kwa upendo badala ya kuendelea kukasirika au kuweka kinyongo?

Zb 37:8; Met 14:29; Efe 4:​26, 27; Yak 1:​19, 20

Kwa nini milipuko ya hasira, kufoka, matusi, na kumuumiza mwingine kimwili kwa njia yoyote si mwenendo unaokubalika hata kidogo kwa Mkristo?

Zb 11:5; Gal 5:​19-21; Efe 4:​31, 32; Tit 3:2

Kunapokuwa na hali ya kutoelewana, mume na mke wanapaswa kuwa na lengo gani?

Zb 34:14; Mt 5:9; Ro 12:​17, 18, 21

Ndoa ambayo msingi wake ni Yehova inapata baraka gani?

Mhu 4:​9-12

Viwango kwa ajili ya ndoa

Biblia inasema nini kuhusu viwango vya Yehova inapohusu mahusiano ya kingono na ndoa?

Met 6:32; Mt 5:​27, 28; 1Ko 6:​9, 10; Ebr 13:4

Wakristo wana maoni gani kuhusu ndoa ya wake wengi?

Mt 19:​8, 9; 1Ko 7:2; 1Ti 3:​2, 12

Tunajuaje kwamba ndoa inapaswa kuwa kati ya mwanamume na mwanamke?

Mwa 2:​18, 22, 24; Mt 19:​4-6; Ro 1:​23-27

Kwa nini wenzi wa ndoa wanapaswa kuendelea kuwa pamoja?

Mk 10:​6-9; Ro 7:​2, 3; 1Ko 7:​10, 11

Ni nini msingi pekee wa Kimaandiko wa talaka kati ya Wakristo?

Mt 5:32; 19:9

Yehova anahisije kuhusu talaka isiyo na msingi unaofaa?

Mal 2:​13-16

Mwenzi wa ndoa anapokufa, je, mwenzi aliyebaki yuko huru kufunga ndoa tena?

Ro 7:​2, 3; 1Ko 7:39

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki